Habari Zenye Kuwa Katika Zaburi
Zaburi 113:1
Zaburi 113:3
Musaada wa Kutafuta Habari
Munara wa Mulinzi,
1/9/2006, uku. 14
Zaburi 113:6
Musaada wa Kutafuta Habari
Munara wa Mulinzi,
1/9/2006, uku. 14
15/6/2006, uku. 31
15/10/2005, uku. 27
1/11/2004, uku. 29
Zaburi 113:7
Musaada wa Kutafuta Habari
Munara wa Mulinzi,
1/9/2006, uku. 14
113 Mumusifu Yah!
Mumusifu, ninyi watumishi wa Yehova,
Musifu jina la Yehova.
2 Jina la Yehova lisifiwe
Kuanzia sasa na milele.+
3 Kuanzia mahali jua linatokea mupaka mahali jua linashukia,
Jina la Yehova lisifiwe.+
4 Yehova iko juu sana ya mataifa yote;+
Utukufu wake uko juu ya mbingu.+
5 Ni nani mwenye kuwa kama Yehova Mungu wetu,+
Mwenye anakaa kule juu?
6 Anainama ili aangalie mbingu na dunia,+
7 Anainua mutu wa hali ya chini kutoka katika mavumbi.
Anainua maskini kutoka kwenye rundo la majivu+
8 Ili kumufanya akae pamoja na watu wenye vyeo,
Pamoja na watu wenye vyeo kati ya watu wake.
9 Anapatia makao mwanamuke tasa
Kama mama mwenye furaha mwenye kuwa na watoto.+
Mumusifu Yah!