Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 13
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Samweli

      • Sauli anachagua jeshi (1-4)

      • Sauli anatenda kwa kimbelembele (5-9)

      • Samweli anamukaripia Sauli (10-14)

      • Israeli hawakukuwa na silaha (15-23)

1 Samweli 13:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Hesabu ya miaka yake haipatikane katika maandishi ya Kiebrania.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 13:21

1 Samweli 13:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 18:1; 2 Sa. 1:4; 21:7
  • +Yosh. 18:28; 1 Sa. 10:26

1 Samweli 13:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 13:2, 3; 1 Sa. 9:16
  • +Yosh. 21:8, 17
  • +Amu 3:26, 27; 6:34; 2 Sa. 2:28

1 Samweli 13:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 5:9; 1 Sa. 11:14

1 Samweli 13:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 20:1
  • +Yosh. 7:2; 18:11, 12; 1 Sa. 14:23

1 Samweli 13:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 14:11

1 Samweli 13:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 32:1, 33; Yosh. 13:24, 25

1 Samweli 13:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “uliwekwa.”

1 Samweli 13:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 15:22, 23

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo),

    1/2017, uku. 17

1 Samweli 13:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 13:6, 8
  • +1 Sa. 13:5

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/8/2000, uku. 12-13

1 Samweli 13:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “sijatuliza uso.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/8/2000, uku. 12-13

1 Samweli 13:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 15:11

1 Samweli 13:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 15:28
  • +1 Sa. 16:1; 2 Sa. 7:15; Zab 78:70; Mdo 13:22
  • +Mwa 49:10; 2 Sa. 5:2; 7:8; 1Nya 28:4
  • +Mez. 11:2

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/9/2011, uku. 26-29

    “Kila Andiko,” uku. 63

1 Samweli 13:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 13:7; 14:2

1 Samweli 13:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 13:3
  • +1 Sa. 13:2

1 Samweli 13:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 10:11

1 Samweli 13:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “piki.”

1 Samweli 13:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Kipimo cha zamani, chenye ni karibu sehemu mbili za tatu za shekeli.

  • *

    Ao “piki.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, uku. 1964

    Munara wa Mulinzi,

    15/3/2005, uku. 29

1 Samweli 13:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 17:47, 50

1 Samweli 13:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kambi ya mbele.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 13:2; 14:4, 5

Maandiko ingine

1 Sam. 13:1Mdo 13:21
1 Sam. 13:21 Sa. 18:1; 2 Sa. 1:4; 21:7
1 Sam. 13:2Yosh. 18:28; 1 Sa. 10:26
1 Sam. 13:3Yosh. 13:2, 3; 1 Sa. 9:16
1 Sam. 13:3Yosh. 21:8, 17
1 Sam. 13:3Amu 3:26, 27; 6:34; 2 Sa. 2:28
1 Sam. 13:4Yosh. 5:9; 1 Sa. 11:14
1 Sam. 13:5Kum 20:1
1 Sam. 13:5Yosh. 7:2; 18:11, 12; 1 Sa. 14:23
1 Sam. 13:61 Sa. 14:11
1 Sam. 13:7Hes 32:1, 33; Yosh. 13:24, 25
1 Sam. 13:91 Sa. 15:22, 23
1 Sam. 13:111 Sa. 13:6, 8
1 Sam. 13:111 Sa. 13:5
1 Sam. 13:131 Sa. 15:11
1 Sam. 13:141 Sa. 15:28
1 Sam. 13:141 Sa. 16:1; 2 Sa. 7:15; Zab 78:70; Mdo 13:22
1 Sam. 13:14Mwa 49:10; 2 Sa. 5:2; 7:8; 1Nya 28:4
1 Sam. 13:14Mez. 11:2
1 Sam. 13:151 Sa. 13:7; 14:2
1 Sam. 13:161 Sa. 13:3
1 Sam. 13:161 Sa. 13:2
1 Sam. 13:18Yosh. 10:11
1 Sam. 13:221 Sa. 17:47, 50
1 Sam. 13:231 Sa. 13:2; 14:4, 5
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Samweli 13:1-23

Cha Kwanza cha Samweli

13 Sauli alikuwa na miaka . . .* wakati alikuwa mufalme,+ na kwa miaka mbili alitawala juu ya Israeli. 2 Sauli alichagua wanaume elfu tatu (3 000) katika Israeli; elfu mbili (2 000) katikati yao walikuwa pamoja na Sauli kule Mikmashi na katika eneo lenye milima la Beteli, na elfu moja (1 000) walikuwa pamoja na Yonatani+ katika muji wa Gibea+ wa Benyamini. Aliwaruhusu wenye walibakia waende zao, kila mumoja kwenye hema yake. 3 Kisha Yonatani akapiga na kuua kambi ya kijeshi ya Wafilisti+ yenye ilikuwa Geba,+ na Wafilisti wakasikia habari hiyo. Na Sauli akaagiza baragumu ipigwe+ katika inchi yote, na kusema: “Waebrania wasikie!” 4 Israeli wote wakasikia habari hii: “Sauli amepiga na kuua kambi ya kijeshi ya Wafilisti, na sasa Israeli wamenuka mubaya kati ya Wafilisti.” Kwa hiyo watu wakaitwa ili wamufuate Sauli kule Gilgali.+

5 Wafilisti pia wakakusanyika pamoja ili wapigane na Israeli, walikuwa na magari ya vita elfu makumi tatu (30 000) na wapanda-farasi elfu sita (6 000) na wanajeshi wengi kama chembe za muchanga pembeni ya bahari;+ na wakapanda na kupiga kambi kule Mikmashi upande wa mashariki wa Bet-aveni.+ 6 Na wanaume wa Israeli wakaona kwamba walikuwa katika hatari, kwa sababu watu walikuwa wenye kubanwa sana; kwa hiyo watu wakajificha ndani ya mapango,+ mashimo, miamba, vyumba vya chini ya udongo, na matangi. 7 Hata wamoja kati ya Waebrania walivuka Yordani na kuingia katika inchi ya Gadi na Gileadi.+ Lakini Sauli alikuwa angali Gilgali, na watu wote wenye walimufuata walikuwa wanatetemeka. 8 Aliendelea kungojea kwa siku saba (7) mupaka wakati wenye ulichaguliwa* wenye Samweli alikuwa ameweka, lakini Samweli hakukuja Gilgali, na watu walikuwa wanatawanyika kutoka kwake. 9 Mwishowe Sauli akasema: “Muniletee zabihu ya kuteketezwa na zabihu za ushirika.” Na akatoa ile zabihu ya kuteketezwa.+

10 Lakini wakati tu alikuwa amemaliza kutoa zabihu ya kuteketezwa, Samweli akafika. Kwa hiyo Sauli akatoka ili kukutana naye na kumubariki. 11 Kisha Samweli akasema: “Umefanya nini?” Sauli akajibu: “Niliona kwamba watu walikuwa wananiacha,+ na haukukuja kwa wakati wenye ulichaguliwa, na Wafilisti walikuwa wanakusanyika pamoja kule Mikmashi.+ 12 Kwa hiyo nikasema katika moyo wangu, ‘Sasa Wafilisti watashuka kunishambulia Gilgali, na sijatafuta wema* wa Yehova.’ Kwa hiyo nilijisikia kuwa ninalazimika kutoa zabihu ya kuteketezwa.”

13 Basi Samweli akamuambia Sauli: “Umetenda kwa upumbavu. Haukutii amri yenye Yehova Mungu wako alikupatia.+ Kama ungetii, Yehova angefanya ufalme wako ukuwe imara juu ya Israeli milele. 14 Lakini sasa ufalme wako hautadumu.+ Yehova atatafuta mutu mwenye kufurahisha moyo wake,+ na Yehova atamuweka kuwa kiongozi juu ya watu wake,+ kwa sababu haukutii mambo yenye Yehova alikuamuru.”+

15 Kisha Samweli akasimama na kupanda kuenda zake kutoka Gilgali mupaka muji wa Gibea wa Benyamini, na Sauli akahesabia watu; wale wenye walibakia pamoja naye walikuwa wanaume karibu mia sita (600).+ 16 Sauli, Yonatani mwana wake, na watu wenye walibakia pamoja nao walikuwa wanakaa katika muji wa Geba+ wa Benyamini, na Wafilisti walikuwa wamepiga kambi kule Mikmashi.+ 17 Na vikundi vya washambuliaji vilikuwa vinatoka katika kambi ya Wafilisti katika makundi tatu (3). Kundi moja lilikuwa linageuka kuelekea kwenye barabara yenye inaenda Ofra, mupaka katika inchi ya Shuali; 18 kundi lingine lilikuwa linageuka kuelekea kwenye barabara ya Bet-horoni;+ na kundi la tatu (3) lilikuwa linageuka kuelekea kwenye barabara yenye inapeleka kwenye mupaka wenye kuangaliana na bonde la Seboimu, kuelekea jangwa.

19 Sasa hapakupatikana fundi yeyote wa chuma katika inchi yote ya Israeli, kwa sababu Wafilisti walikuwa wamesema: “Ili Waebrania wasitengeneze upanga wala mukuki.” 20 Na Israeli wote walilazimika kushuka kuenda kwa Wafilisti ili majembe yao, sururu,* mashoka, ao miundu yao inolewe. 21 Bei ya kunoa ilikuwa pimu* moja kwa ajili ya majembe, kwa ajili ya sururu,* kwa ajili ya vyombo vyenye meno tatu (3), kwa ajili ya mashoka, na pia kwa ajili ya kuimarisha muchokoo wa kuongozea ngombe. 22 Na siku ya pigano, hakuna upanga wala mukuki wenye ulipatikana katika mukono wa mutu yeyote katikati ya watu wenye walikuwa pamoja na Sauli na Yonatani;+ ni Sauli na Yonatani mwana wake tu ndio walikuwa na silaha.

23 Sasa kambi ya kijeshi* ya Wafilisti ilikuwa imeenda kwenye njia ya bonde la Mikmashi.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine