Ezekieli
20 Sasa katika mwaka wa saba (7), mwezi wa tano (5), siku ya kumi (10) ya mwezi huo, wamoja kati ya wazee wa Israeli walikuja na kukaa mbele yangu ili kumuuliza Yehova. 2 Basi neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema: 3 “Mwana wa binadamu, sema na wazee wa Israeli, na uwaambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Je, munakuja kuniuliza? ‘Kama vile hakika ninaishi, sitajibu maulizo yenu,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”’
4 “Je, uko tayari kuwahukumu?* Mwana wa binadamu je, uko tayari kuwahukumu? Uwajulishe mambo yenye kuchukiza yenye mababu zao walifanya.+ 5 Uwaambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Siku yenye nilichagua Israeli,+ pia niliapia* uzao wa* nyumba ya Yakobo, na kujijulisha kwao katika inchi ya Misri.+ Ndiyo, niliwaapia na kusema, ‘Mimi ni Yehova Mungu wenu.’ 6 Katika siku hiyo niliapa kwamba nitawatosha katika inchi ya Misri na kuwapeleka katika inchi yenye nilikuwa nimechunguza* kwa ajili yao, inchi yenye kutiririka maziwa na asali.+ Inchi hiyo ilikuwa ya muzuri sana kuliko* inchi zote. 7 Kisha nikawaambia, ‘Kila mumoja wenu anapaswa kutupa vitu vyenye kuchukiza vyenye viko mbele ya macho yenu, musijichafue kwa sanamu zenye kuchukiza* za Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’+
8 “‘“Lakini wakaniasi na hawakutaka kunisikiliza. Hawakutupa vitu vyenye kuchukiza vyenye vilikuwa mbele yao, nao hawakuacha sanamu zenye kuchukiza za Misri.+ Kwa hiyo nikaahidi kumwanga kasirani yangu kali juu yao na kuleta hasira yangu kwa ukamili juu yao katika inchi ya Misri. 9 Lakini nilitenda kwa ajili ya jina langu ili lisichafuliwe mbele ya mataifa yenye waliishi kati yake.+ Kwa maana nilijijulisha kwao* mbele ya mataifa hayo wakati niliwatosha* katika inchi ya Misri.+ 10 Kwa hiyo nikawatosha katika inchi ya Misri na kuwaingiza katika jangwa.+
11 “‘“Kisha nikawapatia sheria zangu na kuwajulisha maamuzi yangu ya hukumu,+ ili mutu mwenye kuyafuata apate uzima kupitia hayo.+ 12 Pia nikawapatia sabato zangu+ ili zikuwe alama kati yangu nao,+ kusudi wajue kwamba mimi, Yehova ndiye ninawatakasa.
13 “‘“Lakini nyumba ya Israeli waliniasi katika jangwa.+ Hawakutembea katika sheria zangu, nao walikataa maamuzi yangu ya hukumu, yenye kama mutu anayafuata, atapata uzima kupitia hayo. Walichafua kabisa sabato zangu. Kwa hiyo nikaahidi kumwanga kasirani yangu kali juu yao katika jangwa ili niwamalize.+ 14 Lakini nilitenda kwa ajili ya jina langu mwenyewe ili lisichafuliwe mbele ya mataifa, yenye niliwatosha* mbele ya macho yao.+ 15 Pia, nikawaapia katika jangwa kwamba sitawaingiza katika inchi yenye nilikuwa nimewapatia+—inchi yenye kutiririka maziwa na asali,+ inchi ya muzuri sana kuliko* inchi zote— 16 kwa sababu walikataa maamuzi yangu ya hukumu na hawakutembea katika sheria zangu, nao walichafua sabato zangu, kwa maana moyo wao ulikuwa unafuata sanamu zao zenye kuchukiza.+
17 “‘“Lakini niliwasikilia huruma,* na sikuwaharibu; sikuwaangamiza katika jangwa. 18 Niliambia wana wao katika jangwa,+ ‘Musitembee katika masharti ya mababu zenu+ wala musishike hukumu zao wala musijichafue kwa sanamu zao zenye kuchukiza. 19 Mimi ni Yehova Mungu wenu. Mutembee katika sheria zangu, na mushike maamuzi yangu ya hukumu, na muyafuate.+ 20 Na mutakase sabato zangu,+ na zitakuwa alama kati yangu na ninyi ili mujue kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu.’+
21 “‘“Lakini wana hao wakaanza kuniasi.+ Hawakutembea katika sheria zangu, na hawakushika na kufuata maamuzi yangu ya hukumu, yenye kama mutu anayafuata, atapata uzima kupitia hayo. Sabato zangu walizichafua. Kwa hiyo nikaahidi kumwanga kasirani yangu kali juu yao na kuleta hasira yangu kwa ukamili juu yao katika jangwa.+ 22 Lakini nilijizuia+ na kutenda kwa ajili ya jina langu mwenyewe,+ ili lisichafuliwe mbele ya mataifa, yenye yaliona wakati niliwatosha* Misri. 23 Pia, niliwaapia katika jangwa kwamba nitawasambaza kati ya mataifa na kuwatawanya katika inchi mbalimbali,+ 24 kwa sababu hawakushika maamuzi yangu ya hukumu na walikataa sheria zangu,+ walichafua sabato zangu, nao wakafuata* sanamu zenye kuchukiza za mababu zao.+ 25 Pia, niliwaruhusu wafuate masharti yenye hayakukuwa ya muzuri na maamuzi ya hukumu yenye hayangewasaidia kupata uzima.+ 26 Niliwaacha wachafuliwe kupitia zabihu zao—wakati walipitisha kila muzaliwa wa kwanza katika moto+—ili kuwafanya ukiwa, kusudi wajue kwamba mimi ni Yehova.”’
27 “Kwa hiyo sema na nyumba ya Israeli, Ee mwana wa binadamu, na uwaambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Ni kwa njia hii pia, mababu zenu walinitukana kwa kunitendea kwa ukosefu wa uaminifu. 28 Niliwaingiza katika inchi yenye niliapa kwamba nitawapatia.+ Wakati waliona vilima vyote vya murefu na miti yenye majani mengi,+ walianza kutoa zabihu zao na matoleo yao yenye kuchukiza. Walitoa harufu za muzuri* za zabihu zao na kumwanga matoleo yao ya vinywaji pale. 29 Kwa hiyo nikawauliza, ‘Mahali hapa pa juu penye munaenda panamaanisha nini? (Pangali panaitwa Mahali pa Juu mupaka leo.)’”’+
30 “Sasa ambia nyumba ya Israeli, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Je, munajichafua kama vile mababu zenu walifanya kwa kufuata sanamu zao zenye kuchukiza ili kufanya ukahaba wa kiroho pamoja nazo?+ 31 Na je, mungali munajichafua mupaka leo kwa kutolea zabihu sanamu zenu zote zenye kuchukiza, na kupitisha wana wenu katika moto?+ Je, wakati huohuo ninapaswa kujibu maulizo yenu, Ee nyumba ya Israeli?”’+
“‘Kama vile hakika ninaishi,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘Sitajibu maulizo yenu.+ 32 Na jambo lenye munafikiria* wakati munasema, “Tukuwe kama mataifa, kama familia za inchi zingine, zenye kuabudu* miti na majiwe,”+ jambo hilo halitatimia hata kidogo.”’”
33 “‘Kama vile hakika ninaishi,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘Nitatawala nikiwa mufalme juu yenu kwa mukono wenye nguvu, kwa mukono wenye kunyooshwa, na kwa kasirani kali yenye kumwangwa.+ 34 Nitawatosha kati ya vikundi vya watu na kuwakusanya pamoja kutoka katika inchi kwenye mumesambazwa kwa mukono wenye nguvu, kwa mukono wenye kunyooshwa, na kwa kasirani kali yenye kumwangwa.+ 35 Nitawaingiza katika jangwa la vikundi vya watu na kuingia katika hukumu pamoja na ninyi kule uso kwa uso.+
36 “‘Kama vile niliingia katika hukumu pamoja na mababu zenu katika jangwa la inchi ya Misri, ni vile nitaingia katika hukumu pamoja na ninyi,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema. 37 ‘Nitawapitisha ninyi chini ya fimbo ya muchungaji+ na kuwaleta chini ya masharti ya* agano. 38 Lakini nitaondoa waasi katikati yenu na wale wenye kunikosea.+ Kwa maana nitawatosha katika inchi yenye wanakaa ndani wakiwa wageni, lakini hawataingia katika inchi ya Israeli;+ na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
39 “Sasa ninyi, Ee nyumba ya Israeli, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Kila mumoja wenu aende na atumikie sanamu zake zenye kuchukiza.+ Lakini kisha, kama hamunisikilize, hamutaweza tena kuchafua jina langu takatifu kupitia zabihu zenu na sanamu zenu zenye kuchukiza.’+
40 “‘Kwa maana katika mulima wangu mutakatifu, kwenye mulima murefu wa Israeli,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘ni pale nyumba yote ya Israeli, wao wote, watanitumikia katika inchi.+ Nitafurahishwa nao kule, na nitaomba michango yenu na matunda ya kwanza ya matoleo yenu, vitu vyenu vyote vitakatifu.+ 41 Kwa sababu ya harufu ya muzuri,* nitafurahishwa na ninyi wakati nitawatosha kati ya vikundi vya watu na kuwakusanya pamoja kutoka katika inchi mbalimbali kwenye mumesambazwa;+ na nitatakaswa kati yenu mbele ya macho ya mataifa.’+
42 “‘Na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova+ wakati nitawaleta katika inchi ya Israeli,+ katika inchi yenye niliapa kwamba nitapatia mababu zenu. 43 Na kule mutakumbuka mwenendo wenu na matendo yenu yote yenye mulijichafua kupitia hayo,+ na ninyi mutajichukia* kwa sababu ya mambo yote ya mubaya yenye mulifanya.+ 44 Basi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova wakati nitawatendea kwa ajili ya jina langu,+ haiko kulingana na mwenendo wenu muovu ao kulingana na matendo yenu yenye kupotoka, Ee nyumba ya Israeli,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”
45 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 46 “Mwana wa binadamu, elekeza uso wako upande wa eneo la kusini na utangaze kuelekea kusini, na utolee unabii pori la eneo la mashamba la kusini. 47 Ambia pori la kusini, ‘Sikia neno la Yehova. Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Angalia, ninawasha moto juu yako,+ nao utateketeza kila muti mubichi na kila muti wenye kukauka ndani yako. Mwali wa moto wenye kuwaka hautazimwa,+ na utachoma kila uso, kuanzia kusini mupaka kaskazini. 48 Na miili yote itaona* kwamba Mimi mwenyewe, Yehova, nimewasha moto, ili usizimishwe.”’”+
49 Na mimi nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova! Wanasema kunihusu, ‘Je, yeye hazungumuze tu kwa vitendawili?’”*