Kumbukumbu la Torati
28 “Na kama kwa kweli unasikiliza sauti ya Yehova Mungu wako kwa kuwa muangalifu ili kutenda amri zake zote zenye ninakuamuru leo, hakika Yehova Mungu wako atakuweka juu ya mataifa mengine yote ya dunia.+ 2 Baraka hizi zote zitakuja juu yako na kukufikia,+ kwa sababu unaendelea kusikiliza sauti ya Yehova Mungu wako:
3 “Utabarikiwa katika muji na utabarikiwa katika eneo la mashamba.+
4 “Watoto wako watabarikiwa*+ na pia mazao ya udongo wako na uzao wa mifugo yako, kitoto chako cha ngombe na kitoto chako cha kondoo.+
5 “Kitunga chako+ na bakuli lako la kufinyangia unga+ vitabarikiwa.
6 “Utabarikiwa wakati utaingia ndani, na utabarikiwa wakati utaenda inje.
7 “Yehova atafanya maadui wako wenye kukushambulia washindwe mbele yako.+ Watakushambulia kutoka upande mumoja, lakini watakukimbia kuelekea pande saba (7) tofauti.+ 8 Yehova ataagiza baraka kwa ajili yako juu ya madepo yako+ na kila kazi yako, na hakika atakubariki katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia. 9 Yehova atakufanya kuwa kikundi chake cha watu watakatifu,+ kama vile alikuapia,+ kwa sababu unaendelea kushika amri za Yehova Mungu wako na kutembea katika njia zake. 10 Vikundi vyote vya watu vya dunia vitalazimika kuona kwamba jina la Yehova limeitwa juu yako,+ na vitakuogopa.+
11 “Yehova atakufanya ukuwe na watoto wengi sana na mifugo mingi sana na udongo wenye kuzaa sana+ katika inchi yenye Yehova aliapia mababu zako kwamba atakupatia.+ 12 Yehova atakufungulia depo yake ya muzuri, mbingu, ili kupatia inchi yako mvua kwa wakati wake+ na ili kubariki mambo yote yenye unafanya. Utakopesha mataifa mengi, lakini wewe mwenyewe hautahitaji kukopa.+ 13 Yehova atakufanya kuwa kichwa, hapana mukia; na utakuwa juu,+ hapana chini, kama unaendelea kutii amri za Yehova Mungu wako zenye ninakuamuru leo ili ushike na kutenda. 14 Haupaswe kugeuka na kuacha maneno yote yenye ninakuamuru leo, kwa kuenda kuume ao kushoto,+ kwa kufuata miungu mingine ili kuitumikia.+
15 “Lakini kama hautasikiliza sauti ya Yehova Mungu wako kwa kuwa muangalifu ili kutenda amri zake zote na sheria zake zenye ninakuamuru leo, laana hizi zote zitakuja juu yako na kukufikia:+
16 “Utalaaniwa katika muji, na utalaaniwa katika eneo la mashamba.+
17 “Kitunga chako+ na bakuli lako la kufinyangia unga+ vitalaaniwa.
18 “Watoto wako*+ na mazao ya udongo wako na kitoto chako cha ngombe na kitoto chako cha kondoo+ kitalaaniwa.
19 “Utalaaniwa wakati utaingia ndani, na utalaaniwa wakati utaenda inje.
20 “Yehova atatuma laana juu yako, muvurugo na azabu katika kila kazi yako mupaka wakati utakuwa umeharibiwa na kumalizika haraka, kwa sababu ya mazoea yako mabaya na kuniacha mimi.+ 21 Yehova atafanya ugonjwa ukuandame mupaka wakati utakuwa umeharibiwa katika inchi yenye unaenda kuriti.+ 22 Yehova atakupiga kwa kifua kikubwa, homa kali,+ kuvimba, homa yenye kuchoma, upanga,+ ugonjwa wenye kukausha mimea, na kuvu;+ na vitakuandama mupaka wakati utakuwa umemalizika. 23 Anga zenye kuwa juu ya kichwa chako zitakuwa shaba, na dunia yenye kuwa chini yako, itakuwa chuma.+ 24 Yehova atafanya mvua ya inchi yako kuwa ungaunga na mavumbi yenye yatakunyeshea kutoka mbinguni mupaka wakati utakuwa umeharibiwa kabisa. 25 Yehova atafanya ushindwe mbele ya maadui wako.+ Utawashambulia kutoka upande mumoja, lakini utawakimbia kuelekea pande saba (7) tofauti; na utakuwa kitu cha kuogopesha sana kwa falme zote za dunia.+ 26 Na mizoga yako itakuwa chakula kwa ajili ya kila ndege wa anga na munyama wa inchi, bila mutu wa kuwaogopesha.+
27 “Yehova atakupiga kwa majipu ya Misri, emoroide,* ukurutu wa ngozi,* na vipele vya ngozi, hautaweza kupona magonjwa hayo. 28 Yehova atakupiga kwa ugonjwa wa wazimu na upofu+ na kukufanya uvurugike.* 29 Utapapasa-papasa katikati ya muchana, kama vile kipofu anapapasa-papasa katika giza,+ na hautapata matokeo ya muzuri katika jambo lolote lenye unafanya; na kila mara watu watakupunja na kukuiba vitu, na hakuna mwenye atakuokoa.+ 30 Utachumbia mwanamuke, lakini mwanaume mwingine atamulala kinguvu. Utajenga nyumba, lakini hautaishi ndani yake.+ Utapanda shamba la mizabibu, lakini hautaanza kutumia matunda yake.+ 31 Ngombe-dume wako atachinjwa mbele ya macho yako, lakini hautakula nyama yake. Punda wako ataibiwa mbele ya macho yako, lakini hatarudishwa kwako. Maadui wako watapewa kondoo wako, lakini hakuna mwenye atakuokoa. 32 Watu wengine watapewa watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke+ wakati utakuwa unaangalia, na sikuzote utatamani kuwaona, lakini mikono yako haitakuwa na nguvu za kufanya kitu chochote. 33 Mavuno ya udongo wako na mazao yako yote yatakuliwa na watu wenye haujue,+ na sikuzote watu watakupunja na kukuponda-ponda. 34 Utapata ugonjwa wa wazimu kwa sababu ya mambo yenye macho yako yataona.
35 “Yehova atakupiga kwa majipu yenye maumivu makali na yenye hayawezi kupona kwenye magoti na miguu yako, kuanzia kikanyangio cha muguu wako mupaka kwenye sehemu ya juu ya katikati ya kichwa chako. 36 Yehova atakupeleka wewe na mufalme mwenye uliweka juu yako kwenye taifa lenye wewe na mababu zako hamukujua,+ na kule utatumikia miungu mingine, miungu ya miti na ya majiwe.+ 37 Na utakuwa kitu cha kuogopesha sana na cha kuzarauliwa,* na kitu cha kuchekelewa kati ya vikundi vyote vya watu kwenye Yehova atakupeleka.+
38 “Utapeleka mbegu nyingi katika shamba, lakini utavuna kidogo,+ kwa sababu nzige watazimeza. 39 Utapanda na kupalilia mashamba ya mizabibu, lakini hautakunywa divai yoyote wala kukusanya zabibu zozote,+ kwa sababu kidudu kitazikula. 40 Utakuwa na miti ya zeituni katika eneo lako lote, lakini hautajipakaa mafuta yoyote, kwa sababu zeituni zako zitaanguka. 41 Utazaa watoto wanaume na watoto wanamuke, lakini hawataendelea kuwa wako, kwa sababu wataenda katika utekwa.+ 42 Makundi ya vidudu yatavamia* miti yako yote na mazao ya udongo wako. 43 Mukaaji mugeni mwenye kuwa katikati yako ataendelea kupanda juu yako zaidi na zaidi, wakati wewe utaendelea kushuka chini zaidi na zaidi. 44 Atakukopesha, lakini wewe hautamukopesha.+ Atakuwa kichwa, lakini wewe mwenyewe utakuwa mukia.+
45 “Laana hizi zote+ hakika zitakuja juu yako na kukufuatilia na kukufikia mupaka wakati utakuwa umeharibiwa,+ kwa sababu haukusikiliza sauti ya Yehova Mungu wako kwa kushika amri zake na sheria zake zenye alikuamuru.+ 46 Na zitaendelea kubakia juu yako na uzao wako kama alama na jambo la ajabu la kudumu,+ 47 kwa sababu haukumutumikia Yehova Mungu wako kwa furaha na shangwe ya moyo wakati ulikuwa na kila kitu kwa wingi.+ 48 Yehova atatuma maadui wako wakushambulie, na utawatumikia+ wakati uko na njaa+ na kiu na wakati unakosewa nguo na wakati unakosewa kila kitu. Atatia nira ya chuma kwenye shingo yako mupaka wakati atakuwa amekuharibu.
49 “Yehova atainua juu yako taifa la mbali,+ kutoka mwisho wa dunia; litakurukia kama tai,+ taifa lenye hautaelewa luga yake,+ 50 taifa lenye uso mukali lenye haliheshimie muzee wala kumuonyesha kijana wema.+ 51 Watakula uzao wa mifugo yako na mazao ya udongo wako mupaka wakati utakuwa umeharibiwa. Hawatakuachia nafaka yoyote, divai mupya wala mafuta, kitoto cha ngombe wala kitoto cha kondoo mupaka wakati watakuwa wamekuharibu.+ 52 Watakuzunguka kwa ajili ya vita, na hivyo kukufungia ndani ya miji yako yote* katika inchi yako yote mupaka wakati kuta zako za murefu na zenye ngome zenye unategemea zitaanguka. Ndiyo, hakika watakuzunguka kwa ajili ya vita katika miji yako yote, katika inchi yako yote yenye Yehova Mungu wako amekupatia.+ 53 Halafu utalazimika kula watoto wako* mwenyewe, nyama ya watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke+ wenye Yehova Mungu wako amekupatia, kwa sababu ya kuzungukwa sana kwa ajili ya vita na kwa sababu ya taabu yenye adui yako atakuletea.
54 “Hata mwanaume mupole* sana na mwenye hisia nyingi kati yako hatamusikilia huruma ndugu yake ao bibi yake mupendwa ao wana wake wenye wanabakia, 55 na hatawapatia hata kidogo sehemu yoyote ya nyama ya wana wake yenye atakula, kwa maana hana kitu kingine chochote cha kula kwa sababu ya kuzungukwa sana kwa ajili ya vita na kwa sababu ya taabu yenye adui yako ataleta katika miji yako.+ 56 Na mwanamuke mupole* sana na mwenye hisia nyingi kati yako mwenye hawezi hata kufikiria kutia kikanyangio cha muguu wake chini kwa sababu ni mupole sana+ hatakuwa na huruma kuelekea bwana yake mupendwa wala mutoto wake mwanaume wala mutoto wake mwanamuke, 57 hata kuelekea vitu vyenye kutoka katikati ya miguu yake kisha kuzaa na kuelekea wana wenye anazaa, kwa maana atawakula kwa uficho kwa sababu ya kuzungukwa sana kwa ajili ya vita na kwa sababu ya taabu yenye adui yako ataleta katika miji yako.
58 “Kama hautashika kwa uangalifu maneno yote ya Sheria hii yenye kuandikwa katika kitabu hiki+ na kama hauogope jina hili lenye utukufu na lenye kuogopesha sana,+ la Yehova+ Mungu wako, 59 Yehova atakupiga wewe na uzao wako kwa mapigo makali sana, mapigo makubwa na yenye kuendelea,+ na magonjwa hatari na yenye kuendelea. 60 Atakuletea tena magonjwa yote ya Misri yenye ulikuwa unaogopa, na hakika yatashikamana na wewe. 61 Tena, Yehova atakuletea pia kila ugonjwa ao pigo lenye haliandikwe katika kitabu hiki cha Sheria mupaka wakati utakuwa umeharibiwa. 62 Hata kama mumekuwa wengi sana kama vile nyota za mbinguni,+ ni watu kidogo katikati yenu ndio watabakia,+ kwa sababu haukusikiliza sauti ya Yehova Mungu wako.
63 “Na kama vile Yehova alifurahia wakati fulani kuwafanya mufanikiwe na kuongezeka, ni vile Yehova atafurahia kuwaharibu na kuwaangamiza; na mutaongolewa kutoka katika inchi yenye unakaribia kuriti.
64 “Yehova atakusambaza kati ya mataifa yote, kutoka mwisho mumoja wa dunia mupaka mwisho mwingine wa dunia,+ na kule utalazimika kutumikia miungu ya miti na ya majiwe, yenye wewe na mababu zako hamukujua.+ 65 Hautakuwa na amani katika mataifa hayo+ wala mahali pa kupumuzishia kikanyangio cha muguu wako. Lakini, ukiwa kule Yehova atakupatia moyo wenye wasiwasi+ na macho yenye kuwa zaifu na hisia ya kupoteza tumaini.*+ 66 Uzima wako utakuwa katika hatari kubwa, na utasikia woga usiku na muchana; na hautakuwa hakika kama utaokoka. 67 Asubui utasema, ‘Ingekuwa muzuri kama ilikuwa mangaribi!’ na mangaribi utasema, ‘Ingekuwa muzuri kama ilikuwa asubui!’ kwa sababu ya woga wenye utasikia katika moyo wako na kwa sababu ya mambo yenye macho yako yataona. 68 Na hakika Yehova atakurudisha Misri kwa mashua,* kupitia ile njia yenye nilikuambia: ‘Hautaiona tena hata kidogo,’ na kule mutalazimika kujiuzisha kwa maadui wenu ili kuwa watumwa wanaume na watumwa wanamuke, lakini hakutakuwa mutu wa kuwauza.”