Zaburi
2 Sababu gani mataifa yako na musukosuko
Na vikundi vya watu vinasema kwa sauti ya chini-chini* jambo lenye halina maana?+
3 Wanasema: “Tukate pingu zao
Na kutupa kamba zao!”
4 Ule mwenye kukaa akiwa mufalme kule mbinguni atacheka;
Yehova atawachekelea.
5 Wakati huo atasema nao katika kasirani yake
Na kuwaogopesha sana katika kasirani yake yenye kuwaka,
6 Kwa kusema: “Mimi mwenyewe nimemuweka mufalme wangu+
Juu ya Sayuni,+ mulima wangu mutakatifu.”
11 Mumutumikie Yehova kwa woga,
Na mushangilie mukitetemeka.
12 Mumuheshimie* mwana,+ kama hamufanye vile Mungu* atakasirika sana
Na ninyi mutaangamia kutoka katika njia,+
Kwa maana kasirani Yake inawaka haraka.
Wenye furaha ni wale wote wenye wanamukimbilia Yeye.