Zekaria
9 Tangazo:
“Neno la Yehova liko juu ya inchi ya Hadraki,
Na Damasko ndio shabaha yake*+
—Kwa maana jicho la Yehova linaangalia wanadamu+
Na linaangalia makabila yote ya Israeli—
2 Na juu ya Hamati,+ yenye kuwa kwenye mupaka wake
Na juu ya Tiro+ na Sidoni,+ kwa maana ni wenye hekima sana.+
3 Tiro ilijijengea boma.*
Na ilikusanya feza kama mavumbi
Na zahabu kama uchafu wenye kuwa katika barabara.+
4 Angalia! Yehova atachukua mali zake,
Na atapiga na kuua jeshi lake katika bahari;*+
Na itateketezwa ndani ya moto.+
5 Ashkeloni itaona jambo hilo na itaogopa;
Gaza itasikia uchungu mukubwa,
Ekroni pia, kwa sababu tumaini lake limepatishwa haya.
Mufalme ataangamia kutoka Gaza,
Na Ashkeloni haitakuwa na wakaaji.+
6 Na mwana-haramu atakaa katika Ashdodi,
Na nitamaliza kiburi cha Wafilisti.+
7 Nitaondoa vitu vyenye kuwa na madoa ya damu katika kinywa chake
Na vitu vyenye kuchukiza kutoka katika meno yake,
Na atabakia kwa ajili ya Mungu wetu;
Na atakuwa kama shehe* katika Yuda,+
Na Ekroni kama Muyebusi.+
8 Nitapiga kambi kama mulinzi* kwa ajili ya nyumba yangu,+
Na hivyo hakutakuwa mutu mwenye anapita na mwenye anarudia;
Na hakuna musimamizi wa kazi* mwenye atapita tena,+
Kwa maana sasa nimeiona* kwa macho yangu.
9 Furahi sana, Ee binti ya Sayuni.
Piga vigelegele vya ushindi, Ee binti ya Yerusalemu.
Angalia! Mufalme wako anakuja kwako.+
10 Nitaondoa gari la vita kutoka Efraimu
Na farasi kutoka Yerusalemu.
Upinde wa mapigano utachukuliwa.
Na atatangaza amani kwa mataifa;+
Utawala wake utakuwa kutoka bahari mupaka bahari
11 Sasa wewe, Ee mwanamuke, kwa damu ya agano lako,
Nitatosha wafungwa wako ndani ya shimo lenye halina maji.+
12 Murudie kwenye ngome, ninyi wafungwa wenye tumaini.+
Leo ninakuambia,
‘Nitakulipa, Ee mwanamuke, fungu lenye liko mara mbili.+
13 Kwa maana nitamukunja* Yuda kama upinde wangu.
Nitajaza Efraimu katika upinde,*
Na nitaamusha wana wako, Ee Sayuni,
Wapigane na wana wako, Ee Ugiriki,
Na nitakufanya ukuwe kama upanga wa mupiganaji-vita.’
14 Yehova ataonekana juu yao,
Na mushale wake utaenda kama umeme wa radi.
Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova atapiga baragumu,+
Na ataenda pamoja na zoruba zenye upepo mukali za kusini.
15 Yehova wa majeshi atawalinda,
Na watameza na kutiisha majiwe ya kombeo.+
Watakunywa na kufanya makelele, kama wenye walikunywa divai;
Na watajazwa kama bakuli,
Kama pembe za mazabahu.+
16 Yehova Mungu wao atawaokoa katika siku hiyo
Kama kundi la watu wake;+
Kwa maana watakuwa kama majiwe yenye samani ya taji, yenye kungaa juu ya udongo wake.+
17 Kwa maana wema wake ni mukubwa kabisa,+
Na uzuri wake ni mukubwa kabisa!
Nafaka itafanya vijana wakuwe na nguvu,
Na divai mupya itafanya mabikira wakuwe na nguvu.”+