Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 23
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Mambo ya Walawi

      • Siku takatifu na sikukuu (1-44)

        • Sabato (3)

        • Pasaka (4, 5)

        • Sikukuu ya Mikate Yenye Haina Chachu (6-8)

        • Kutoa matunda ya kwanza (9-14)

        • Sikukuu ya Majuma (15-21)

        • Namna ya muzuri ya kuvuna (22)

        • Sikukuu ya Kupiga Tarumbeta (23-25)

        • Siku ya Kufunika Zambi (26-32)

        • Sikukuu ya Vibanda (33-43)

Mambo ya Walawi 23:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 23:14; Law. 23:37
  • +Hes 10:10

Mambo ya Walawi 23:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 16:30; 20:10; Mdo 15:21
  • +Ne 13:22

Mambo ya Walawi 23:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “katikati ya zile mangaribi mbili.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 9:2, 3; 28:16
  • +Kut 12:3, 6; Kum 16:1; 1 Kor. 5:7

Mambo ya Walawi 23:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 28:17; 1 Kor. 5:8
  • +Kut 12:15; 13:6; 34:18

Mambo ya Walawi 23:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 12:16

Mambo ya Walawi 23:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 18:8, 12; Mez. 3:9; Eze 44:30
  • +1 Kor. 15:20, 23

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    15/7/2007, uku. 26

Mambo ya Walawi 23:11

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    15/7/2007, uku. 26

Mambo ya Walawi 23:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Sehemu mbili za kumi za efa zilikuwa sawa na litre 4.4 (vibaba 4). Angalia Nyongeza B14.

  • *

    Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”

  • *

    Hini ilikuwa sawa na litre 3.67 (painti 7.75). Angalia Nyongeza B14.

Mambo ya Walawi 23:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 34:22; Kum 16:9, 10

Mambo ya Walawi 23:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 2:1
  • +Hes 28:26-31; Kum 16:16

Mambo ya Walawi 23:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Sehemu mbili za kumi za efa zilikuwa sawa na litre 4.4 (vibaba 4). Angalia Nyongeza B14.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 7:11, 13
  • +Kut 23:16; 34:22

Mambo ya Walawi 23:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 28:26, 27

Mambo ya Walawi 23:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 4:23
  • +Law. 3:1

Mambo ya Walawi 23:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 7:34; 10:14; Hes 18:9; Kum 18:4; 1 Kor. 9:13

Mambo ya Walawi 23:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 10:10

Mambo ya Walawi 23:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wenye kuteseka.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 19:9; Kum 24:19; Ru 2:2, 3
  • +Isa 58:7
  • +Law. 19:33

Mambo ya Walawi 23:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 10:10; 29:1

Mambo ya Walawi 23:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kutesa nafsi zenu.” Kwa ujumla inaeleweka kuwa “kujitesa” kunamaanisha njia mbalimbali za kujinyima, kutia ndani kufunga.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 30:10; Law. 25:9
  • +Law. 16:29, 30; Hes 29:7

Mambo ya Walawi 23:28

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 16:34; Ebr 9:12, 24-26; 10:10; 1 Yo. 2:1, 2

Mambo ya Walawi 23:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Nafsi yoyote yenye haitajitesa.” Ao pengine, “Mutu yeyote mwenye hatafunga.”

  • *

    Ao “atauawa kutoka.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 9:13; 15:30

Mambo ya Walawi 23:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nafsi.”

Mambo ya Walawi 23:32

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mutatesa nafsi zenu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 16:29-31; 23:27; Hes 29:7

Mambo ya Walawi 23:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Makao ya Muda.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 23:16; Hes 29:12; Kum 16:13; Ezr 3:4; Ne 8:14-18; Yoh 7:2

Mambo ya Walawi 23:36

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ne 8:18

Mambo ya Walawi 23:37

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 23:14; Kum 16:16
  • +Hes 28:26; 29:7
  • +Law. 1:3
  • +Law. 2:1, 11
  • +Hes 15:5; 28:6, 7

Mambo ya Walawi 23:38

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 16:23; 20:8; 31:13
  • +Kut 28:38; Hes 18:29
  • +Kum 12:11
  • +Hes 29:39; Kum 12:6; 1Nya 29:9; 2Nya 35:8; Ezr 2:68

Mambo ya Walawi 23:39

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 16:13
  • +Hes 29:12

Mambo ya Walawi 23:40

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “bonde la muto.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ne 8:15; Ufu 7:9
  • +Ne 8:10
  • +Kum 16:15

Mambo ya Walawi 23:41

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 29:12

Mambo ya Walawi 23:42

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 31:10, 11

Mambo ya Walawi 23:43

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 31:13; Zab 78:6
  • +Kut 12:37, 38; Hes 24:5

Maandiko ingine

Mambo ya walawi 23:2Kut 23:14; Law. 23:37
Mambo ya walawi 23:2Hes 10:10
Mambo ya walawi 23:3Kut 16:30; 20:10; Mdo 15:21
Mambo ya walawi 23:3Ne 13:22
Mambo ya walawi 23:5Hes 9:2, 3; 28:16
Mambo ya walawi 23:5Kut 12:3, 6; Kum 16:1; 1 Kor. 5:7
Mambo ya walawi 23:6Hes 28:17; 1 Kor. 5:8
Mambo ya walawi 23:6Kut 12:15; 13:6; 34:18
Mambo ya walawi 23:7Kut 12:16
Mambo ya walawi 23:10Hes 18:8, 12; Mez. 3:9; Eze 44:30
Mambo ya walawi 23:101 Kor. 15:20, 23
Mambo ya walawi 23:15Kut 34:22; Kum 16:9, 10
Mambo ya walawi 23:16Mdo 2:1
Mambo ya walawi 23:16Hes 28:26-31; Kum 16:16
Mambo ya walawi 23:17Law. 7:11, 13
Mambo ya walawi 23:17Kut 23:16; 34:22
Mambo ya walawi 23:18Hes 28:26, 27
Mambo ya walawi 23:19Law. 4:23
Mambo ya walawi 23:19Law. 3:1
Mambo ya walawi 23:20Law. 7:34; 10:14; Hes 18:9; Kum 18:4; 1 Kor. 9:13
Mambo ya walawi 23:21Hes 10:10
Mambo ya walawi 23:22Law. 19:9; Kum 24:19; Ru 2:2, 3
Mambo ya walawi 23:22Isa 58:7
Mambo ya walawi 23:22Law. 19:33
Mambo ya walawi 23:24Hes 10:10; 29:1
Mambo ya walawi 23:27Kut 30:10; Law. 25:9
Mambo ya walawi 23:27Law. 16:29, 30; Hes 29:7
Mambo ya walawi 23:28Law. 16:34; Ebr 9:12, 24-26; 10:10; 1 Yo. 2:1, 2
Mambo ya walawi 23:29Hes 9:13; 15:30
Mambo ya walawi 23:32Law. 16:29-31; 23:27; Hes 29:7
Mambo ya walawi 23:34Kut 23:16; Hes 29:12; Kum 16:13; Ezr 3:4; Ne 8:14-18; Yoh 7:2
Mambo ya walawi 23:36Ne 8:18
Mambo ya walawi 23:37Kut 23:14; Kum 16:16
Mambo ya walawi 23:37Hes 28:26; 29:7
Mambo ya walawi 23:37Law. 1:3
Mambo ya walawi 23:37Law. 2:1, 11
Mambo ya walawi 23:37Hes 15:5; 28:6, 7
Mambo ya walawi 23:38Kut 16:23; 20:8; 31:13
Mambo ya walawi 23:38Kut 28:38; Hes 18:29
Mambo ya walawi 23:38Kum 12:11
Mambo ya walawi 23:38Hes 29:39; Kum 12:6; 1Nya 29:9; 2Nya 35:8; Ezr 2:68
Mambo ya walawi 23:39Kum 16:13
Mambo ya walawi 23:39Hes 29:12
Mambo ya walawi 23:40Ne 8:15; Ufu 7:9
Mambo ya walawi 23:40Ne 8:10
Mambo ya walawi 23:40Kum 16:15
Mambo ya walawi 23:41Hes 29:12
Mambo ya walawi 23:42Kum 31:10, 11
Mambo ya walawi 23:43Kum 31:13; Zab 78:6
Mambo ya walawi 23:43Kut 12:37, 38; Hes 24:5
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
  • 44
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Mambo ya Walawi 23:1-44

Mambo ya Walawi

23 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Sikukuu za Yehova za vipindi+ zenye munapaswa kutangaza+ ni mikusanyiko mitakatifu. Hizi ni sikukuu zangu za vipindi vya hali ya hewa:

3 “‘Siku sita (6) kazi inaweza kufanywa, lakini siku ya saba (7) ni sabato ya pumuziko kamili,+ mukusanyiko mutakatifu. Hamutafanya kazi yoyote. Itakuwa sabato kwa ajili ya Yehova kila mahali kwenye mutaishi.+

4 “‘Hizi ni sikukuu za Yehova za vipindi, mikusanyiko mitakatifu yenye munapaswa kutangaza katika nyakati zenye ziliwekwa kwa ajili ya vipindi hivyo: 5 Katika mwezi wa kwanza, siku ya kumi na ine (14) ya mwezi huo,+ mangaribi wakati giza linaanza* ni Pasaka+ ya Yehova.

6 “‘Siku ya kumi na tano (15) ya mwezi huo ni Sikukuu ya Yehova ya Mikate Yenye Haina Chachu.+ Kwa siku saba (7) munapaswa kula mikate yenye haina chachu.+ 7 Siku ya kwanza, mutafanya mukusanyiko mutakatifu.+ Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu. 8 Lakini kwa siku saba (7) mutamutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto. Kutakuwa mukusanyiko mutakatifu siku ya saba. Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu.’”

9 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 10 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Wakati mutaingia mwishowe katika inchi yenye ninawapatia na kuvuna mavuno yake, munapaswa kumuletea kuhani+ fungu la matunda ya kwanza+ ya mavuno yenu. 11 Na kuhani atatikisa fungu hilo mbele na nyuma mbele ya Yehova ili mukubaliwe. Kuhani atalitikisa siku yenye inafuata siku ya Sabato. 12 Siku yenye fungu hilo linatikiswa, munapaswa kutoa mwana-kondoo dume katika mwaka wake wa kwanza mwenye hana kasoro, ili akuwe toleo la kuteketezwa kwa Yehova. 13 Toleo lake la nafaka litakuwa sehemu mbili za kumi (2/10) za efa* ya unga muzuri wenye kuchanganywa na mafuta, ili kuwa toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, harufu ya muzuri.* Toleo lake la kinywaji litakuwa sehemu moja ya ine (1/4) ya hini* ya divai. 14 Hamupaswe kula mukate wowote, nafaka yoyote yenye kukaangwa, ao nafaka mupya mupaka siku hiyo, mupaka wakati mutaleta toleo la Mungu wenu. Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote kila mahali kwenye mutaishi.

15 “‘Munapaswa kuhesabu sabato saba (7) kuanzia siku yenye inafuata siku ya Sabato, kuanzia siku yenye munaleta fungu la mbegu la toleo la kutikiswa.+ Yanapaswa kuwa majuma ya kuenea. 16 Mutahesabu siku makumi tano (50)+ mupaka siku yenye inafuata Sabato ya saba (7), na kisha mutamutolea Yehova toleo mupya la nafaka.+ 17 Munapaswa kuleta mikate mbili kutoka mahali kwenye munaishi ili ikuwe toleo la kutikiswa. Mikate hiyo inapaswa kutengenezwa na sehemu mbili za kumi (2/10) za efa* ya unga muzuri. Inapaswa kupikwa na chachu,+ ni matunda ya kwanza yenye kukomaa yenye yanatolewa kwa Yehova.+ 18 Na munapaswa kutoa mikate hiyo pamoja na wana-kondoo dume saba (7) wenye hawana kasoro, kila mumoja anapaswa kuwa na mwaka mumoja, na ngombe-dume mumoja mudogo na kondoo-dume wawili.+ Watakuwa toleo la kuteketezwa kwa ajili ya Yehova pamoja na toleo lao la nafaka na matoleo yao ya vinywaji, ili kuwa toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto, lenye harufu ya kumupendeza* Yehova. 19 Na munapaswa kutoa mwana-mbuzi mumoja kwa ajili ya toleo la zambi+ na wana-kondoo dume wawili, kila mumoja anapaswa kuwa na mwaka mumoja, ili wakuwe zabihu ya ushirika.+ 20 Kuhani atawatikisa mbele na nyuma pamoja na ile mikate ya matunda ya kwanza yenye kukomaa, ili kuwa toleo la kutikiswa mbele ya Yehova, pamoja na wale wana-kondoo dume wawili. Ni vitu vitakatifu vyenye vinatolewa kwa Yehova kwa ajili ya kuhani.+ 21 Siku hiyo mutafanya tangazo+ kwa ajili ya mukusanyiko mutakatifu kwa ajili yenu. Hamutafanya kazi yoyote ya nguvu. Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote kila mahali kwenye mutaishi.

22 “‘Wakati munavuna mavuno ya inchi yenu, haupaswe kuvuna mavuno yote ya mipaka ya shamba lako na haupaswe kuokota masalio ya mavuno yako.+ Unapaswa kuyaachia maskini*+ na mukaaji mugeni.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”

23 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 24 “Waambie Waisraeli, ‘Katika mwezi wa saba (7), siku ya kwanza ya mwezi huo, mutakuwa na pumuziko kamili, ukumbusho wenye utatangazwa kwa kupiga tarumbeta,+ mukusanyiko mutakatifu. 25 Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu, na mutamutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto.’”

26 Yehova akasema tena na Musa, na kumuambia: 27 “Lakini, siku ya kumi (10) ya mwezi huo wa saba (7) ni Siku ya Kufunika Zambi.+ Mutafanya mukusanyiko mutakatifu, na munapaswa kujitesa*+ na kumutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto. 28 Hamupaswe kufanya kazi yoyote siku hiyo ya pekee kwa sababu ni siku ya kufunika zambi ili kufunika zambi+ kwa ajili yenu mbele ya Yehova Mungu wenu. 29 Mutu yeyote mwenye hatajitesa* siku hiyo ataondolewa* katikati ya watu wake.+ 30 Na kila mutu* mwenye atafanya kazi yoyote siku hiyo, nitamuharibu kutoka kati ya watu wake. 31 Hamupaswe kufanya kazi yoyote. Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote kila mahali kwenye mutaishi. 32 Ni sabato ya pumuziko kamili kwa ajili yenu, na mutajitesa*+ siku ya kenda (9) ya mwezi huo wakati wa mangaribi. Mutafanya sabato kuanzia mangaribi hiyo mupaka mangaribi yenye inafuata.”

33 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 34 “Waambie Waisraeli, ‘Siku ya kumi na tano (15) ya mwezi huo wa saba (7) ni Sikukuu ya Vibanda* ya siku saba kwa ajili ya Yehova.+ 35 Kutakuwa mukusanyiko mutakatifu siku ya kwanza, na hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu. 36 Kwa siku saba (7) munapaswa kumutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto. Siku ya munane (8), mutafanya mukusanyiko mutakatifu,+ na munapaswa kumutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto. Ni mukusanyiko mukubwa. Hamupaswe kufanya kazi yoyote ya nguvu.

37 “‘Hizi ni sikukuu za Yehova za vipindi+ zenye mutatangaza kuwa mikusanyiko mitakatifu+ ya kumutolea Yehova toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto: toleo la kuteketezwa+ na toleo la nafaka+ la zabihu na matoleo ya vinywaji+ kulingana na programu ya kila siku. 38 Matoleo hayo yanaongezwa juu ya matoleo yenye yanatolewa wakati wa sabato za Yehova,+ na zawadi zenu,+ matoleo yenu ya naziri,+ na matoleo yenu ya kujipendea,+ yenye munapaswa kumutolea Yehova. 39 Lakini, siku ya kumi na tano (15) ya mwezi wa saba (7), wakati mutakuwa mumekusanya mazao ya inchi, mutafanya sikukuu ya Yehova kwa siku saba.+ Siku ya kwanza ni pumuziko kamili na siku ya munane (8) ni pumuziko kamili.+ 40 Siku ya kwanza, mutakamata matunda ya miti yenu mikubwa na yenye kupendeza, matawi ya miti ya mitende,+ matawi ya miti yenye majani mengi na miti ya mierebi ya bonde,* na mutashangilia+ mbele ya Yehova Mungu wenu kwa siku saba (7).+ 41 Mutamufanyia Yehova sikukuu hiyo kwa siku saba (7) katika mwaka.+ Kwa kuwa ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote, munapaswa kuifanya katika mwezi wa saba. 42 Mutakaa katika vibanda kwa siku saba (7).+ Wote wenye walizaliwa katika Israeli watakaa katika vibanda, 43 ili vizazi vyenu vya wakati wenye kuja vijue+ kwamba nilifanya Waisraeli wakae katika vibanda wakati nilikuwa ninawatosha katika inchi ya Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”

44 Kwa hiyo Musa akaambia Waisraeli juu ya sikukuu za Yehova za vipindi.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine