Zaburi
94 Ee Mungu wa kisasi, Yehova,+
Ee Mungu wa kisasi, angaza!
2 Simama, Ee Muamuzi wa dunia.+
Lipa wenye majivuno kile wanastahili.+
3 Waovu wataendelea mupaka wakati gani, Ee Yehova,
Waovu wataendelea kushangilia mupaka wakati gani?+
4 Wanasema maneno mengi yenye hayana maana na kuongea kwa kiburi;
Wakosaji wote wanajisifu.
5 Wanaponda watu wako, Ee Yehova,+
Na kukandamiza uriti wako.
6 Wanaua mujane na mukaaji mugeni,
Na kuua watoto wenye hawana baba.
8 Muelewe jambo hili, ninyi wenye hamuna akili;
Ninyi wapumbavu, ni wakati gani mutaonyesha ufahamu?+
9 Ule mwenye alifanya* sikio, je, hawezi kusikia?
Ule mwenye aliumba jicho, je, hawezi kuona?+
10 Ule mwenye kurekebisha mataifa, je, hawezi kukaripia?+
Yeye Ndiye anafundisha watu ujuzi!+
11 Yehova anajua mawazo ya wanadamu,
Kwamba ni pumuzi tu.+
12 Mwenye furaha ni mutu mwenye unarekebisha, Ee Yah,+
Mwenye unafundisha mambo yenye kuwa katika sheria yako,+
13 Ili kumupatia utulivu katika siku za musiba,
Mupaka wakati shimo litachimbwa kwa ajili ya waovu.+
15 Kwa maana hukumu itakuwa tena yenye haki,
Na wote wenye kuwa wanyoofu katika moyo wataifuata.
16 Ni nani atasimama ili kushambulia waovu kwa ajili yangu?
Ni nani atanitetea juu ya wakosaji?
18 Wakati nilisema: “Muguu wangu unatereza,”
Upendo wako mushikamanifu, Ee Yehova, uliendelea kunitegemeza.+
20 Je, kiti cha ufalme chenye upotovu kinaweza* kuungana na wewe
23 Atafanya matendo yao maovu yawarudilie.+
Atawaharibu* kupitia uovu wao wenyewe.