Ezekieli
43 Kisha akanipeleka kwenye mulango mukubwa wenye unaelekea mashariki.+ 2 Pale nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukikuja kutoka mashariki,+ na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji yenye kuteremuka haraka;+ na dunia ilingaa kupitia utukufu wake.+ 3 Mambo yenye niliona yalikuwa kama maono ambayo nilikuwa nimeona wakati nilikuja* kuharibu muji, na yalionekana kama mambo yenye nilikuwa nimeona karibu na muto Kebari;+ na nikaanguka uso chini.
4 Kisha utukufu wa Yehova ukaingia katika hekalu* kupitia mulango mukubwa wenye unaelekea mashariki.+ 5 Kisha roho ikaniinua na kuniingiza katika kiwanja cha ndani, na nikaona kwamba hekalu lilikuwa limejaa utukufu wa Yehova.+ 6 Kisha nikasikia mutu akizungumuza na mimi kutoka katika lile hekalu, na mutu huyo akakuja na kusimama pembeni yangu.+ 7 Akaniambia:
“Mwana wa binadamu, hapa ndipo mahali pa kiti changu cha ufalme+ na mahali pa vikanyangio vya miguu yangu,+ kwenye nitakaa kati ya watu wa Israeli milele.+ Nyumba ya Israeli haitachafua tena jina langu takatifu,+ wao na wafalme wao, kupitia ukahaba wao wa kiroho na kupitia mizoga ya wafalme wao wakati wanakufa. 8 Kwa kutia kizingiti* chao karibu na kizingiti changu na mwimo wa mulango wao pembeni ya mwimo wa mulango wangu, tukitenganishwa tu na ukuta kati yangu na wao,+ walichafua jina langu takatifu kupitia mambo yenye kuchukiza yenye walifanya, kwa hiyo nikawaharibu katika kasirani yangu.+ 9 Sasa acha watie ukahaba wao wa kiroho na mizoga ya wafalme wao mbali na mimi, na nitakaa kati yao milele.+
10 “Sasa wewe, mwana wa binadamu, fasiria nyumba ya Israeli kuhusu hekalu+ ili wasikie haya kwa sababu ya makosa yao,+ nao wanapaswa kujifunza plani yake.* 11 Kama watasikia haya kwa sababu ya mambo yote yenye wamefanya, utawajulisha plani ya hekalu, mupangilio wake, na njia zake za kutokea, na miingilio yake.+ Uwaonyeshe plani zake zote na maagizo yake, plani zake na sheria zake, na uziandike mbele ya macho yao, ili waone ramani zake na kushika maagizo yake.+ 12 Hii ndiyo sheria ya hekalu. Eneo lote kuzunguka kichwa cha mulima pande zote ni takatifu zaidi.+ Angalia! Hii ndiyo sheria ya hekalu.
13 “Hivi ni vipimo vya mazabahu kwa kipimo cha mikono+ (kila mukono uliongezewa kiganja kimoja).* Sehemu yake ya chini ni mukono mumoja, na upana wake mukono mumoja. Iko na mupaka wa upana wa shubiri* moja kuzunguka pembeni. Hiyo ndiyo sehemu ya chini ya mazabahu. 14 Kuanzia sehemu ya chini ya sakafu* mupaka kwenye ukingo wa chini wenye unazunguka ni mikono mbili, na upana wake ni mukono mumoja. Kuanzia ukingo mudogo wenye unazunguka mupaka kwenye ule ukingo mukubwa wenye unazunguka ni mikono ine (4), na upana wake ni mukono mumoja. 15 Jiko la mazabahu liko na urefu wa mikono ine (4), na kutoka kwenye jiko la mazabahu kuelekea juu kuko zile pembe ine.+ 16 Jiko la mazabahu liko na pande ine (4) zenye kuwa sawasawa,* urefu wake ni mikono kumi na mbili (12) na upana wake ni mikono kumi na mbili.+ 17 Pande ine (4) za ukingo wenye unazunguka ziko na urefu wa mikono kumi na ine (14) na upana wa mikono kumi na ine; na mupaka wenye unazunguka ni nusu ya mukono, na sehemu yake ya chini ni mukono mumoja pande zote.
“Na vipandio vyake vinaelekea mashariki.”
18 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Hii ndiyo miongozo ya kufuata wakati mazabahu inatengenezwa, ili matoleo mazima ya kuteketezwa yatolewe na damu inyunyizwe* juu yake.’+
19 “‘Unapaswa kutoa ngombe-dume mudogo mwenye kutoka katika mifugo kwa makuhani Walawi wazao wa Sadoki,+ wenye wananikaribia ili kunitolea utumishi kusudi akuwe toleo la zambi,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema. 20 ‘Unapaswa kukamata sehemu fulani ya damu yake na kuitia kwenye zile pembe ine (4) za mazabahu, juu ya kona ine za ukingo wenye unazunguka, na juu ya mupaka kuzunguka pande zote ili kuitakasa kutokana na zambi na kufunika zambi kwa ajili yake.+ 21 Kisha utakamata ule ngombe-dume mudogo, lile toleo la zambi, ili umuteketeze kwa moto katika mahali kwenye kulichaguliwa kwa hekalu, inje ya patakatifu.+ 22 Katika siku ya pili utatoa mbuzi-dume mwenye hana kasoro kuwa toleo la zambi; nao watatakasa mazabahu kutokana na zambi kama vile waliitakasa kutokana na zambi kupitia ule ngombe-dume mudogo.’
23 “‘Wakati utamaliza kuitakasa kutokana na zambi, utatoa ngombe-dume mudogo mwenye hana kasoro kutoka katika mifugo na kondoo-dume mwenye hana kasoro kutoka katika kundi. 24 Utawaleta kwa Yehova, na makuhani watatupa chumvi juu yao+ na kuwatoa kwa Yehova wakiwa toleo nzima la kuteketezwa. 25 Kwa siku saba (7) utatoa mbuzi-dume kuwa toleo la zambi la kila siku,+ pia ngombe-dume mudogo kutoka katika mifugo na kondoo-dume kutoka katika kundi, utatoa wanyama wenye hawana kasoro.* 26 Kwa siku saba (7) watafunika zambi kwa ajili ya mazabahu, nao wataisafisha na kuitayarisha ili ianze kutumiwa. 27 Wakati siku hizo zitakuwa zimemalizika, siku ya munane (8)+ na kisha pale, makuhani watatoa matoleo yenu* mazima ya kuteketezwa na zabihu za ushirika kwenye mazabahu; na nitapendezwa na ninyi,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”