Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 3
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Kumbukumbu la Torati

      • Ushindi juu ya Mufalme Ogu wa Bashani (1-7)

      • Kugawanya inchi upande wa mashariki wa Yordani (8-20)

      • Yoshua anaambiwa asiogope (21, 22)

      • Musa hataingia katika inchi hiyo (23-29)

Kumbukumbu la Torati 3:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 21:33-35

Kumbukumbu la Torati 3:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 32:33; Kum 29:7, 8; Yosh. 13:29, 30

Kumbukumbu la Torati 3:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.

Kumbukumbu la Torati 3:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 27:29
  • +Law. 18:25

Kumbukumbu la Torati 3:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Bonde la Muto la Arnoni.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 32:33
  • +Yosh. 12:1, 2

Kumbukumbu la Torati 3:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 21:33

Kumbukumbu la Torati 3:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao pengine, “jiwe la rangi nyeusi la volkano.”

  • *

    Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.

Kumbukumbu la Torati 3:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Bonde la Muto la Arnoni.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 32:34
  • +Hes 32:33

Kumbukumbu la Torati 3:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 32:39; Yosh. 13:29-31; 1Nya 5:23

Kumbukumbu la Torati 3:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Vijiji vya Mahema vya Yairi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 2:22
  • +Kum 3:4
  • +Yosh. 13:13
  • +Hes 32:40, 41

Kumbukumbu la Torati 3:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 32:39; Yosh. 17:1

Kumbukumbu la Torati 3:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Bonde la Muto la Arnoni.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 32:33; Yosh. 22:9

Kumbukumbu la Torati 3:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, Bahari Yenye Kufa.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 34:11, 12

Kumbukumbu la Torati 3:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 32:20-22

Kumbukumbu la Torati 3:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 1:14, 15; 22:4, 8

Kumbukumbu la Torati 3:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 11:28; 14:30; 27:18
  • +Yosh. 10:25

Kumbukumbu la Torati 3:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 14:14; 15:3; Kum 1:30; 20:4; Yosh. 10:42

Kumbukumbu la Torati 3:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 15:16; Kum 11:2
  • +Kut 15:11; 2 Sa. 7:22; 1 Fal. 8:23; Zab 86:8; Yer 10:6, 7

Kumbukumbu la Torati 3:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 3:8; Kum 1:7; 11:11, 12

Kumbukumbu la Torati 3:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 20:12; 27:13, 14; Kum 4:21; Zab 106:32

Kumbukumbu la Torati 3:27

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 27:12
  • +Kum 34:1, 4

Kumbukumbu la Torati 3:28

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 27:18-20; Kum 1:38; 31:7
  • +Yosh. 1:1, 2

Kumbukumbu la Torati 3:29

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 4:45, 46; 34:5, 6

Maandiko ingine

Kum. 3:1Hes 21:33-35
Kum. 3:4Hes 32:33; Kum 29:7, 8; Yosh. 13:29, 30
Kum. 3:6Law. 27:29
Kum. 3:6Law. 18:25
Kum. 3:8Hes 32:33
Kum. 3:8Yosh. 12:1, 2
Kum. 3:10Hes 21:33
Kum. 3:12Hes 32:34
Kum. 3:12Hes 32:33
Kum. 3:13Hes 32:39; Yosh. 13:29-31; 1Nya 5:23
Kum. 3:141Nya 2:22
Kum. 3:14Kum 3:4
Kum. 3:14Yosh. 13:13
Kum. 3:14Hes 32:40, 41
Kum. 3:15Hes 32:39; Yosh. 17:1
Kum. 3:16Hes 32:33; Yosh. 22:9
Kum. 3:17Hes 34:11, 12
Kum. 3:18Hes 32:20-22
Kum. 3:20Yosh. 1:14, 15; 22:4, 8
Kum. 3:21Hes 11:28; 14:30; 27:18
Kum. 3:21Yosh. 10:25
Kum. 3:22Kut 14:14; 15:3; Kum 1:30; 20:4; Yosh. 10:42
Kum. 3:24Kut 15:16; Kum 11:2
Kum. 3:24Kut 15:11; 2 Sa. 7:22; 1 Fal. 8:23; Zab 86:8; Yer 10:6, 7
Kum. 3:25Kut 3:8; Kum 1:7; 11:11, 12
Kum. 3:26Hes 20:12; 27:13, 14; Kum 4:21; Zab 106:32
Kum. 3:27Hes 27:12
Kum. 3:27Kum 34:1, 4
Kum. 3:28Hes 27:18-20; Kum 1:38; 31:7
Kum. 3:28Yosh. 1:1, 2
Kum. 3:29Kum 4:45, 46; 34:5, 6
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Kumbukumbu la Torati 3:1-29

Kumbukumbu la Torati

3 “Kisha tuligeuka na kupanda kupitia Njia ya Bashani. Na Ogu, mufalme wa Bashani, akatoka pamoja na watu wake wote ili kupigana na sisi kule Edrei.+ 2 Kwa hiyo Yehova akaniambia, ‘Usimuogope, kwa maana nitamutia yeye na watu wake wote na inchi yake katika mukono wako, na utamutendea kama vile ulimutendea Sihoni mufalme wa Waamori, mwenye aliishi Heshboni.’ 3 Kwa hiyo Yehova Mungu wetu akamutia pia Mufalme Ogu wa Bashani pamoja na watu wake wote katika mukono wetu, na tukaendelea kumupiga na tukamuua mupaka hapakukuwa mutu katikati ya watu wake mwenye aliokoka. 4 Kisha tukakamata miji yake yote. Hakuna muji wao hata mumoja wenye hatukuwanyanganya⁠—⁠miji makumi sita (60), eneo lote la Argobu, ufalme wa Ogu katika Bashani.+ 5 Miji hiyo yote ilikuwa yenye ngome kwa sababu ya kuta za murefu, milango mikubwa, na mapingo,* na pia miji mingi sana ya mashambani. 6 Lakini, tuliwaharibu,+ kama vile tulikuwa tumemutendea Mufalme Sihoni wa Heshboni, tuliharibu kila muji, pamoja na wanaume, wanamuke, na watoto.+ 7 Na tukajikamatia mifugo yote na vitu vya miji hiyo.

8 “Wakati huo tulikamata inchi ya wafalme wawili wa Waamori+ wenye walikuwa katika eneo la Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni* mupaka Mulima Hermoni+ 9 (Wasidoni walikuwa wanaita mulima huo Sirioni na Waamori walikuwa wanauita Seniri), 10 miji yote ya eneo tambarare la juu, Gileadi yote, na Bashani yote mupaka Saleka na Edrei,+ miji ya ufalme wa Ogu katika Bashani. 11 Kwa maana Mufalme Ogu wa Bashani ndiye Murefaimu pekee mwenye alikuwa amebakia. Sanduku lake lilitengenezwa na chuma,* na lingali katika muji wa Waamoni wa Raba. Liko na urefu wa mikono* kenda (9) na upana wa mikono ine (4), kwa kipimo cha kawaida cha mukono. 12 Wakati huo tulikamata inchi hii: kuanzia Aroeri,+ muji wenye kuwa karibu na Bonde la Arnoni,* na nusu ya eneo lenye milima la Gileadi, na miji yake nimeipatia Warubeni na Wagadi.+ 13 Na nusu ya kabila la Manase+ nimeipatia sehemu yenye kubakia ya Gileadi na eneo lote la Bashani la ufalme wa Ogu. Eneo lote la Argobu, la Bashani, lilijulikana kuwa inchi ya Warefaimu.

14 “Yairi+ mwana wa Manase alikamata eneo lote la Argobu+ kufikia kwenye mupaka wa Wageshuri na Wamaakati+ na akaita vijiji hivyo vya Bashani kwa jina lake mwenyewe, Hawot-yairi,*+ mupaka leo. 15 Na Makiri+ nimemupatia Gileadi. 16 Na Warubeni na Wagadi+ nimewapatia kuanzia Gileadi mupaka kwenye Bonde la Arnoni,* katikati ya bonde ndio mupaka, kufikia Yaboki, bonde lenye ni mupaka wa Waamoni, 17 na Araba na Yordani na ule mupaka, kuanzia Kinereti kufikia kwenye Bahari ya Araba, Bahari ya Chumvi,* kwenye sehemu ya chini ya miteremuko ya Pisga kuelekea upande wa mashariki.+

18 “Kisha nikawaamuru hivi: ‘Yehova Mungu wenu amewapatia inchi hii ili ikuwe yenu. Wanaume wenu wote hodari watakamata silaha na kuvuka mbele ya ndugu zenu, Waisraeli.+ 19 Ni bibi zenu, watoto wenu, na mifugo yenu tu (ninajua muzuri kwamba muko na mifugo mingi sana) ndio wataendelea kukaa katika miji yenye nimewapatia, 20 mupaka wakati Yehova atapatia ndugu zenu pumuziko, kama vile anawafanyia ninyi, nao pia wakuwe wamekamata inchi yenye Yehova Mungu wenu atawapatia ngambo ya Yordani. Kisha mutarudia, kila mumoja kwenye eneo lake lenye nimewapatia.’+

21 “Wakati huo nilimuamuru Yoshua hivi:+ ‘Umeona na macho yako mwenyewe mambo yenye Yehova Mungu wako ametendea wafalme hao wawili. Ni vile Yehova atatendea falme zote kule kwenye utavuka kuenda.+ 22 Musiwaogope, kwa maana Yehova Mungu wenu ndiye anawapigania ninyi.’+

23 “Wakati huo nilimulilia Yehova, na kusema, 24 ‘Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, umeanza kumuonyesha mutumishi wako ukubwa wako na mukono wako wenye nguvu,+ kwa maana ni mungu gani katika mbingu ao juu ya dunia mwenye anatenda matendo yenye nguvu kama wewe?+ 25 Tafazali uniruhusu nivuke na kuona inchi ya muzuri yenye kuwa ngambo ya Yordani, eneo hili la muzuri lenye milima na Lebanoni.’+ 26 Lakini bado Yehova alikuwa amenikasirikia sana kwa sababu yenu,+ na hakutaka kunisikiliza. Tofauti na hilo, Yehova aliniambia, ‘Achia pale! Usiniambie tena juu ya jambo hili. 27 Panda kwenye kichwa cha Pisga,+ na uangalie mangaribi na kaskazini na kusini na mashariki na uone inchi hiyo na macho yako, kwa maana hautavuka hii Yordani.+ 28 Umuweke Yoshua+ katika madaraka yake na umutie moyo na kumutia nguvu, kwa sababu yeye ndiye atavuka+ mbele ya watu hawa na yeye ndiye atawafanya wariti inchi yenye utaona.’ 29 Mambo hayo yote yalitendeka wakati tulikuwa tunakaa katika bonde mbele ya Bet-peori.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine