Kumbukumbu la Torati
34 Kisha Musa akatoka katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu na kupanda mupaka kwenye Mulima Nebo,+ kwenye kichwa cha Pisga,+ yenye kuangaliana na Yeriko.+ Na Yehova akamuonyesha inchi yote, kuanzia Gileadi mupaka Dani,+ 2 na Naftali yote na inchi ya Efraimu na Manase, na inchi yote ya Yuda mupaka bahari ya mangaribi,*+ 3 na Negebu+ na ile Wilaya,+ bonde tambarare la Yeriko, muji wa miti ya mitende, mupaka Soari.+
4 Kisha Yehova akamuambia: “Hii ndiyo inchi yenye niliapia Abrahamu, Isaka, na Yakobo, na kusema, ‘Nitapatia uzao wako* inchi hii.’+ Nimekuruhusu uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hautavuka kuingia kule.”+
5 Kisha Musa mutumishi wa Yehova akakufa kule katika inchi ya Moabu kama vile Yehova alikuwa amesema.+ 6 Akamuzika katika bonde katika inchi ya Moabu, ngambo ingine ya Bet-peori, na hakuna mwenye anajua kaburi lake liko wapi mupaka leo.+ 7 Musa alikuwa na miaka mia moja makumi mbili (120) wakati alikufa.+ Macho yake hayakukuwa yamefifia, na nguvu zake hazikukuwa zimeisha. 8 Watu wa Israeli wakamulia Musa katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu kwa siku makumi tatu (30).+ Kisha siku za kumulia na kumuombolezea Musa zikaisha.
9 Yoshua mwana wa Nuni alikuwa amejaa roho ya hekima, kwa sababu Musa alikuwa ameweka mukono wake juu yake;+ na Waisraeli wakaanza kumusikiliza, na wakafanya kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.+ 10 Lakini hakujatokea tena nabii mwingine katika Israeli mwenye kuwa kama Musa,+ mwenye Yehova alijua uso kwa uso.+ 11 Alifanya alama zote na miujiza yenye Yehova alikuwa amemutuma afanye katika inchi ya Misri juu ya Farao na juu ya watumishi wake wote na juu ya inchi yake yote,+ 12 pamoja na mukono wenye nguvu na nguvu zenye kuogopesha zenye Musa alionyesha mbele ya macho ya Israeli wote.+