Zaburi
Kwa kiongozi. Wimbo. Muziki.
66 Mumupigie Mungu vigelegele vya ushindi, dunia yote.+
2 Muimbie jina lake lenye utukufu sifa.*
Mutukuze sifa yake.+
3 Muambie Mungu: “Kazi zako ni zenye kuogopesha sana!+
Kwa sababu ya nguvu zako nyingi,
Maadui wako watajikunja kwa woga mbele yako.+
5 Mukuje na muone kazi za Mungu.
Mambo yenye alitendea wana wa binadamu ni yenye kuogopesha sana.+
Kule tulishangilia katika yeye.+
7 Anatawala milele+ kwa nguvu zake.
Macho yake yanachunguza mataifa.+
Wale wenye wako kichwa-nguvu hawapaswe kujiinua.+ (Sela)
8 Mumusifu Mungu wetu, ninyi vikundi vya watu,+
Na sauti ya sifa yake isikike.
10 Kwa maana umetuchunguza, Ee Mungu;+
Umetusafisha kama vile feza inasafishwa.
12 Uliruhusu mwanadamu mwenye anaweza kufa apande juu yetu;*
Tulipita katika moto na katika maji;
Kisha ulituleta mahali kwenye kitulizo.
13 Nitaingia katika nyumba yako nikiwa na matoleo mazima ya kuteketezwa;+
Nitatimiza naziri zenye niliweka kwako+
14 Zenye midomo yangu iliahidi+
Na kinywa changu kilisema wakati nilikuwa katika taabu.
15 Nitakutolea matoleo ya kuteketezwa ya wanyama wenye kunenepa
Pamoja na moshi wa kondoo-dume wa zabihu.
Nitatoa ngombe-dume pamoja na mbuzi-dume. (Sela)
16 Mukuje na musikilize, ninyi wote wenye kumuogopa Mungu,
Na nitawaambia mambo yenye amenitendea.+
17 Nilimuita kwa kinywa changu
Na kumutukuza kwa ulimi wangu.
18 Kama ningeweka katika moyo wangu jambo fulani lenye kuumiza,
Yehova hangenisikia.+
20 Mungu asifiwe, mwenye hakukataa sala yangu
Wala kuniima upendo wake mushikamanifu.