Zaburi
Muziki wa Daudi.
143 Ee Yehova, sikia sala yangu;+
Sikiliza kilio changu cha kuomba musaada.
Unijibu katika uaminifu wako na katika haki yako.
2 Usiingie katika hukumu pamoja na mutumishi wako,
Kwa maana hakuna mutu yeyote mwenye uzima ambaye anaweza kuwa mwenye haki mbele yako.+
3 Kwa maana adui ananifuatilia;*
Ameponda uzima wangu katika udongo.
Amenifanya nikae katika giza kama wale wenye walikufa zamani sana.
5 Ninakumbuka siku za zamani;
Ninafikiri sana* juu ya utendaji wako wote;+
Ninafikiri kwa bidii juu ya* kazi ya mikono yako.
6 Ninakunyooshea mikono yangu;
Niko* kama inchi yenye kukauka yenye kuwa na kiu kwa ajili yako.+ (Sela)
8 Acha nisikie upendo wako mushikamanifu asubui,
Kwa maana ninakutegemea wewe.
9 Uniokoe kutoka kwa maadui wangu, Ee Yehova.
Ninatafuta ulinzi wako.+
10 Unifundishe kufanya mapenzi yako,+
Kwa maana wewe ni Mungu wangu.
Roho yako ni ya muzuri;
Iniongoze kwenye inchi tambarare.*
11 Ee Yehova, linda uzima wangu kwa ajili ya jina lako.