Habakuki
3 Sala ya nabii Habakuki, katika nyimbo za huzuni:*
2 Ee Yehova, nimesikia habari juu yako.
Nimeogopa matendo yako, Ee Yehova.
Uyafanye tena katikati ya miaka!*
Uyafanye yajulikane katikati ya miaka.*
Ukumbuke kuonyesha rehema wakati wa muvurugo.+
Utukufu wake ulifunika mbingu;+
Na dunia ilijaa sifa yake.
4 Kungaa kwake kulikuwa kama vile mwangaza.+
Miali mbili ilitoka kwenye mukono wake,
Kwenye nguvu yake ilifichwa.
6 Alisimama wima na kutikisa dunia.+
Aliangalia, na jambo hilo lilifanya mataifa yaruke.+
Milima ya milele ilivunjwa-vunjwa,
Na vilima vya zamani viliinama.+
Njia zake ni za tangu zamani sana.
7 Niliona taabu katika mahema ya Kushani.
Vitambaa vya hema vya inchi ya Midiani vilitetemeka.+
8 Ee Yehova, je, ni juu ya mito,
Je, kasirani yako imewaka juu ya mito?
Ao je, kasirani yako kali iko juu ya bahari?+
9 Upinde wako haufunikwe na uko tayari.
Fimbo zako zimewekwa* kwa kiapo.* (Sela)
Unapasua dunia kwa mito.
10 Milima ilisumbuka katika maumivu wakati ilikuona.+
Mafuriko ya maji yalipita.
Mahali kwenye maji yenye kuenda chini sana kulinguruma.+
Kuliinua mikono yake juu.
11 Jua na mwezi vilisimama kwenye makao yake ya juu.+
Mishale yako ilienda mbio kama mwangaza.+
Mungao wa mukuki wako ulingaa sana.
12 Ulipita katikati ya dunia ukiwa mwenye kasirani kali.
Ukakanyanga* mataifa kwa hasira.
13 Ulitoka ili kuokoa watu wako, kuokoa mutiwa-mafuta wako.
Uliponda kiongozi wa* nyumba ya waovu.
Iliachwa wazi kuanzia kwenye musingi mupaka juu.* (Sela)
14 Ulitoboa kichwa cha wapiganaji-vita wake kwa silaha zake mwenyewe*
Wakati walinishambulia ili wanisambaze.
Walifurahia sana kumeza kwa uficho mutu mwenye kuteseka.
15 Ulipita katika bahari kwa farasi zako,
Ulipita katika mawimbi makubwa ya bahari.
Mifupa yangu ilianza kuoza;+
Miguu yangu chini ilikuwa inatetemeka.
Lakini ninangojea kimya-kimya siku ya taabu,+
Kwa sababu inakuja juu ya watu wenye kutushambulia.
17 Hata kama muti wa tini hautoe maua,
Na mizabibu ikose matunda;
Hata kama mizeituni haizae matunda,
Na mashamba* hayatoe chakula chochote;
Hata kama kundi linaweza kukosekana katika zizi,*
Na kusikuwe ngombe katika vibanda;
18 Lakini mimi, nitafurahi katika Yehova;
Nitashangilia katika Mungu wa wokovu wangu.+
19 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova ndiye nguvu zangu;+
Atafanya miguu yangu ikuwe kama ile ya paa
Na atanifanya nikanyange mahali pa juu.+
Kwa kiongozi;
utaimbwa kwa vyombo vya kamba.