Zaburi
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Maua ya Mayungiyungi.” Ya Daudi.
69 Uniokoe, Ee Mungu, kwa maana maji yanatia uzima wangu katika hatari.*+
2 Nimezama katika matope yenye kuenda chini sana, mahali kwenye hakuna udongo mugumu.+
Nimeingia katika maji yenye kuenda chini sana,
Na muto mudogo wenye kuteremuka haraka umenifagilia mbali.+
3 Nimechoka kwa sababu ya kuita;+
Koo langu limekauka.
Macho yangu yamechoka wakati ninamungojea Mungu wangu.+
Wale wenye kutaka kuniua,
Maadui wangu wadanganyifu,* wamekuwa wengi.
Nililazimishwa kurudisha kitu chenye sikuiba.
5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu,
Na hatia yangu haifichwe mbele yako.
6 Wale wenye kukutumainia wasipatishwe haya kwa sababu yangu,
Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi.
Wale wenye kukutafuta wasifezeheshwe kwa sababu yangu,
Ee Mungu wa Israeli.
8 Nimekuwa mugeni kwa ndugu zangu,
Mugeni kwa wana wa mama yangu.+
11 Wakati nilifanya magunia kuwa nguo zangu,
Nikakuwa kitu cha kuzarauliwa mbele yao.*
12 Nimekuwa mutu wa kusemwa-semwa na wale wenye kukaa katika mulango mukubwa wa muji,
Na walevi wanaimba juu yangu katika nyimbo zao.
13 Lakini sala yangu ikufikie,
Ee Yehova, kwa wakati wenye kufaa.+
Katika upendo wako mwingi mushikamanifu, Ee Mungu,
Unijibu kwa matendo yako hakika ya wokovu.+
14 Uniokoe katika matope;
Usiache nizame.
Uniokoe kutoka kwa wale wenye kunichukia
Na katika maji yenye kuenda chini sana.+
15 Usiache maji ya garika yenye kuteremuka haraka yanifagilie mbali,+
Wala maji yenye kuenda chini sana yanimeze,
16 Unijibu, Ee Yehova, kwa maana upendo wako mushikamanifu ni mwema.+
Unijibu haraka, kwa maana niko katika taabu.+
18 Unikaribie na uniokoe;*
Unikomboe kwa sababu ya maadui wangu.
19 Unajua lawama yangu na haya yangu na aibu yangu.+
Unaona maadui wangu wote.
20 Lawama imevunja moyo wangu, na kidonda hakiwezi kupona.*
Nilitumaini kwamba nitahurumiwa, lakini sikuhurumiwa hata kidogo,+
Na nilitumaini kupata watu wa kunifariji, lakini sikupata hata mumoja.+
22 Meza yao ikuwe mutego kwao,
Na mafanikio yao yakuwe kitu cha kuwanasa.+
23 Macho yao yatiwe giza ili wasione,
Na ufanye viuno vyao vitetemeke kila wakati.
24 Uwamwangie kasirani yako kali,
Na kasirani yako yenye kuwaka iwapate.+
26 Kwa maana wanamufuatilia ule mwenye ulipiga,
Na wanaendelea kusimulia kuhusu maumivu ya wale wenye uliumiza.
27 Ongeza hatia zaidi juu ya hatia yao,
Na wasikuwe na fungu lolote katika haki yako.
29 Lakini ninateseka, na niko katika maumivu.+
Ee Mungu, nguvu zako za kuokoa zinilinde.
30 Nitaimbia jina la Mungu sifa,
Na nitamutukuza kwa kutoa shukrani.
31 Jambo hilo litamufurahisha Yehova zaidi kuliko ngombe-dume,
32 Wapole wataona jambo hilo na kushangilia.
Mioyo yenu ikuwe tena na uzima, ninyi wenye kumutafuta Mungu.
34 Mbingu na dunia zimusifu,+
Bahari na kila kitu chenye kutembea ndani.