Isaya
65 “Nimejiacha nitafutwe na wale wenye hawakuniuliza;
Nimejiacha nipatwe na wale wenye hawakunitafuta.+
Nimesema, ‘Mimi huyu, mimi huyu!’ kwa taifa lenye halikukuwa linaitia jina langu.+
2 Muchana wote nimenyooshea mikono yangu watu wenye wako kichwa-nguvu,+
Wale wenye kutembea katika njia yenye haiko muzuri,+
Wakifuata mawazo yao wenyewe;+
3 Watu wenye wananikasirisha kila wakati mbele ya uso wangu,+
Wanatoa zabihu katika mabustani+ na kuchoma zabihu juu ya matofali ili zitoe moshi.
Hawa ni moshi katika matundu ya pua yangu, moto wenye kuwaka muchana wote.
6 Angalia! Imeandikwa mbele yangu;
Sitasimama tu,
Lakini nitawalipa,+
Nitawalipa kipimo kamili*
7 Kwa ajili ya makosa yao na kwa ajili ya makosa ya mababu zao pia,”+ ni vile Yehova anasema.
“Kwa sababu wamechoma zabihu juu ya milima ili zitoe moshi
Na wamenilaumu juu ya vilima,+
Kwanza nitawapimia malipo yao kamili.”*
8 Yehova anasema hivi:
“Kama vile wakati divai mupya inapatikana katika kishada cha zabibu
Kisha mutu anasema, ‘Usikiharibu, kwa sababu kuko kitu kizuri* ndani yake,’
Ni vile nitafanya kwa ajili ya watumishi wangu;
Sitawaharibu wote.+
9 Nitatosha uzao* katika Yakobo
Na nitatosha katika Yuda muriti wa milima yangu;+
Watu wangu wenye walichaguliwa watairiti,
Na watumishi wangu watakaa kule.+
10 Sharoni+ itakuwa malisho ya kondoo
Na Bonde* la Akori+ mahali pa kupumuzikia pa ngombe,
Kwa ajili ya watu wangu wenye wananitafuta.
11 Lakini ninyi muko kati ya wale wenye kumuacha Yehova,+
Wale wenye kusahau mulima wangu mutakatifu,+
Wale wenye kupanga meza kwa ajili ya mungu wa Bahati Njema,
Na wale wenye kujaza vikombe vya divai yenye kuchanganywa kwa ajili ya mungu wa Mambo Yenye Kupangwa Mbele ya Wakati.
Na ninyi wote mutainama ili kuuawa;+
Kwa sababu niliita, lakini hamukuitika;
Nilizungumuza lakini hamukusikiliza;+
Muliendelea kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho yangu,
Na mulichagua mambo yenye kunichukiza.”+
13 Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
“Angalia! Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mutakuwa na njaa.+
Angalia! Watumishi wangu watakunywa,+ lakini ninyi mutakuwa na kiu.
Angalia! Watumishi wangu watashangilia,+ lakini ninyi mutapata haya.+
14 Angalia! Watumishi wangu watapiga vigelegele vya shangwe kwa sababu ya hali ya muzuri ya moyo,
Lakini ninyi mutalia kwa sababu ya maumivu ya moyo
Na mutaomboleza kwa sababu ya roho yenye kuvunjika.
15 Mutaacha jina lenye wachaguliwa wangu watatumia kama laana,
Na Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova ataua kila mumoja wenu,
Lakini ataita watumishi wake kwa jina lingine;+
16 Ili kila mutu mwenye anajitafutia baraka katika dunia
Abarikiwe na Mungu wa kweli,*
Na kila mutu mwenye anaapa katika dunia
Aape kwa jina la Mungu wa kweli;*+
Kwa maana taabu* za zamani zitasahauliwa
Zitafichwa ili macho yangu yasizione.+
17 Kwa maana, angalia! Ninaumba mbingu mupya na dunia mupya;+
Na mambo ya zamani hayatakumbukwa,
Wala hayataingia katika moyo.+
18 Basi mufurahi na mukuwe na shangwe milele katika vitu vyenye ninaumba.
Kwa maana angalia! Ninaumba Yerusalemu kuwa kitu cha kuleta shangwe
Na watu wake kuwa kitu cha kuleta furaha.+
19 Na nitashangilia katika Yerusalemu na kufurahi katika watu wangu;+
Sauti ya kulia wala kilio cha taabu havitasikika tena ndani yake.”+
20 “Mahali pale hapatakuwa tena mutoto mudogo mwenye anaishi siku kidogo,
Wala muzee mwenye haishi siku zake zote.
Kwa maana mutu mwenye anakufa na miaka mia moja (100) ataonwa kuwa kijana tu,
Na mutenda-zambi atalaaniwa, hata kama iko* na miaka mia moja.*
22 Hawatajenga ili mutu mwingine akae ndani,
Wala hawatapanda ili wengine wakule.
Kwa maana siku za watu wangu zitakuwa kama siku za muti,+
Na wachaguliwa wangu watafurahia kwa ukamili kazi ya mikono yao.
23 Hawatafanya kazi ya jasho ya* bure,+
Wala hawatazaa watoto ili kupata taabu,
Kwa sababu wao ni uzao wa* watu wenye kubarikiwa na Yehova,+
Na wazao wao pamoja nao.+
24 Hata mbele waite, nitajibu;
Wakati wangali wanasema, nitasikia.
25 Imbwa wa pori na mwana-kondoo watakula pamoja,
Simba atakula majani kama vile ngombe-dume,+
Na chakula cha nyoka kitakuwa mavumbi.
Hawatafanya jambo lolote lenye kuumiza wala kutokeza uharibifu wowote katika mulima wangu wote mutakatifu,”+ ni vile Yehova anasema.