YONA
1 Neno la Yehova likakuja kwa Yona*+ mwana wa Amitai, na kusema: 2 “Simama, uende Ninawi+ ule muji mukubwa, na utangaze hukumu juu yake, kwa sababu nimeona uovu wao.”
3 Lakini Yona akasimama kuenda Tarshishi ili amukimbie Yehova; akashuka mupaka Yopa na akakuta mashua* ya kuenda Tarshishi. Basi akalipa malipo ya kusafiri na kuingia ndani ya mashua ili asafiri nao kuenda Tarshishi, mbali na Yehova.
4 Kisha Yehova akatokeza upepo mukali katika bahari, na kukakuwa zoruba kali sana mupaka mashua* ikakuwa karibu kuvunjika. 5 Wafanyakazi wa mashua* wakaogopa sana na kila mumoja wao akaanza kuitia mungu wake ili amusaidie. Na wakaanza kutupa katika bahari mizigo yenye ilikuwa ndani ya mashua ili kupunguza uzito wake.+ Lakini Yona alikuwa ameingia katika sehemu ya chini ya mashua, na kule alikuwa amelala na kusinzia kabisa. 6 Kapiteni wa mashua* akamukaribia na kumuambia: “Sababu gani unalala? Amuka, omba mungu wako! Pengine Mungu wa kweli atatufikiria, na hatutakufa.”+
7 Kisha wafanyakazi wa mashua* wakaambiana: “Mukuje, tupige kura+ ili tujue ni nani anatuletea taabu hii.” Basi wakapiga kura, na kura ikamuangukia Yona.+ 8 Wakamuambia: “Tafazali utuambie, ni nani anatuletea taabu hii yenye imetupata? Unafanya kazi gani, na unatoka wapi? Unatoka inchi gani, na unatoka kwa watu gani?”
9 Akajibu: “Niko Mwebrania, na ninamuogopa* Yehova Mungu wa mbinguni, Mwenye aliumba bahari na inchi kavu.”
10 Kwa hiyo watu hao wakaogopa hata zaidi, na wakamuuliza: “Umefanya nini?” (Watu hao wakajua kwamba alikuwa anamukimbia Yehova, kwa sababu Yona alikuwa amewaambia.) 11 Basi wakamuambia: “Tukufanye nini ili bahari itulie?” Kwa sababu upepo mukali ulikuwa unaendelea kuongezeka katika bahari. 12 Akajibu: “Muninyangule na kunitupa katika bahari, na bahari itatulia kwa ajili yenu; kwa sababu ninajua kwamba zoruba hii kali imewapiga kwa sababu yangu.” 13 Lakini, watu hao wakajaribu kupiga makasia* kwa nguvu* ili kurudisha mashua* kwenye inchi kavu, hata hivyo hawakuweza kwa sababu upepo mukali uliendelea kuongezeka katika bahari pande zote.
14 Kisha wakamulilia Yehova na kusema: “Tafazali, Ee Yehova, tusikufe kwa sababu ya mutu huyu!* Usiweke juu yetu damu yenye haina kosa, kwa sababu umefanya kama vile ulipenda, Ee Yehova!” 15 Basi wakamunyangula Yona na kumutupa katika bahari; na bahari ikatulia. 16 Kisha watu hao wakamuogopa sana Yehova,+ na wakamutolea Yehova zabihu na kufanya naziri.
17 Sasa Yehova akatuma samaki mukubwa amumeze Yona, na Yona akakaa ndani ya tumbo la ule samaki siku tatu (3) muchana na usiku.+
2 Halafu Yona akasali kwa Yehova Mungu wake wakati alikuwa ndani ya tumbo la samaki,+ 2 na kusema:
“Katika taabu yangu nilimuita Yehova, naye akanijibu.+
Katika sehemu za chini kabisa za* Kaburi* nilililia musaada.+
Ulisikia sauti yangu.
3 Wakati ulinitupa katika sehemu za chini kabisa, katika moyo wa bahari kubwa,
Halafu maji mengi yalinifunika.+
Matuta ya maji na mawimbi yako yote yalipita juu yangu.+
4 Na nilisema, ‘Nimefukuzwa mbali na macho yako!
Nitaweza namna gani kuona tena hekalu lako takatifu?’
Majani ya chini ya maji yalizunguka kichwa changu.
6 Nilizama mupaka sehemu za chini kabisa za milima.
Mapingo* ya dunia yalifungwa juu yangu milele.
Lakini ulitoa uzima wangu katika shimo, Ee Yehova Mungu wangu.+
7 Wakati uzima wangu ulikuwa unakaribia* mwisho, Yehova Ndiye nilikumbuka.+
Halafu sala yangu ilikufikia, ndani ya hekalu lako takatifu.+
8 Wale wenye kujitoa kwa sanamu zenye hazina mafaa yoyote wanaacha chanzo chao cha upendo mushikamanifu.*
9 Lakini mimi, nitakutolea zabihu kwa sauti ya shukrani.
Naziri yenye nimefanya, nitaitimiza.+
Wokovu unatoka kwa Yehova.”+
10 Mwishowe Yehova akaamuru samaki huyo, na akamutapika Yona kwenye inchi kavu.
3 Kisha neno la Yehova likakuja kwa Yona mara ya pili, na kusema:+ 2 “Simama, uende Ninawi+ ule muji mukubwa, na utangaze juu yake ujumbe wenye ninakuambia.”
3 Basi Yona akasimama na kuenda Ninawi+ kwa kutii neno la Yehova.+ Sasa Ninawi ulikuwa muji mukubwa sana*—mwendo wa kutembea kwa siku tatu (3). 4 Kisha Yona akaingia katika muji, na kutembea mwendo wa siku moja, alikuwa anatangaza hivi: “Kisha siku makumi ine (40) tu, Ninawi itaharibiwa.”
5 Na watu wa Ninawi wakaanza kumuamini Mungu,+ na wakatangaza kwamba watu wafunge na kuvaa nguo za magunia, kuanzia mukubwa zaidi mupaka mudogo zaidi kati yao. 6 Wakati ujumbe huo ulifikia mufalme wa Ninawi, akasimama kutoka kwenye kiti chake cha ufalme, akavua nguo yake ya kifalme, akavaa nguo za magunia, na kukaa katika majivu. 7 Zaidi ya hayo, akaamuru tangazo litolewe katika muji wote wa Ninawi,
“Mufalme na watu wake wenye vyeo wanatoa amri hii: Hakuna mutu wala munyama, mifugo wala kundi, wenye wanaruhusiwa kula kitu chochote. Hawapaswe kula chakula, wala kunywa maji. 8 Wote wavae nguo za magunia, watu na wanyama; na wamuombe Mungu kwa bidii na kuacha uovu wao na matendo yao ya jeuri. 9 Ni nani anajua kama Mungu wa kweli hatabadilisha nia yake* na kuacha kasirani yake yenye kuwaka, ili tusiangamie?”
10 Wakati Mungu wa kweli aliona mambo yenye walifanya, namna waliacha uovu wao,+ akabadilisha nia yake* kuhusu musiba wenye alisema ataleta juu yao, na hakuuleta.+
4 Lakini jambo hilo halikumufurahisha Yona hata kidogo, na akakasirika sana. 2 Kwa hiyo akasali hivi kwa Yehova: “Aa, sasa, Yehova, je, haiko vile nilikuwa ninafikiri wakati nilikuwa katika inchi yangu mwenyewe? Ndiyo sababu nilijaribu kwanza kukimbilia Tarshishi;+ kwa sababu nilijua kama wewe ni Mungu mwenye huruma* na rehema, mwenye hakasirike haraka na mwenye upendo mwingi mushikamanifu,+ mwenye kusikitika juu ya musiba. 3 Sasa, Ee Yehova, tafazali ondoa uzima wangu,* kwa sababu afazali nikufe kuliko kuishi.”+
4 Yehova akamuuliza: “Je, uko na sababu ya kukasirika vile?”
5 Kisha Yona akatoka katika muji na kuenda kukaa upande wa mashariki wa muji. Akajijengea kibanda kule na kukaa chini ya kivuli chake ili aone jambo lenye litapata muji.+ 6 Kisha Yehova Mungu akaotesha mumea wa mutango* juu ya Yona ili apate kivuli kwa ajili ya kichwa chake na ili taabu yake ipunguke. Basi Yona akafurahia sana mumea huo wa mutango.
7 Lakini siku yenye ilifuata, wakati kulipambazuka,* Mungu wa kweli akatuma kidudu na kikashambulia mumea huo wa mutango, na ukakauka. 8 Wakati jua lilianza kuwaka, Mungu akatuma pia upepo wa mashariki wenye joto kali, na jua likamuchoma Yona kwenye kichwa, na alikuwa karibu kuzimia. Akaendelea kuomba akufe,* na alikuwa anasema, “Afazali nikufe kuliko kuishi.”+
9 Mungu akamuuliza Yona: “Je, uko na sababu ya kukasirika vile kwa sababu ya mumea huo wa mutango?”+
Na Yona akasema: “Niko na sababu ya kukasirika, kukasirika sana na ninatamani hata nikufe.” 10 Lakini Yehova akasema: “Ulisikilia huruma mumea wa mutango wenye wewe haukuufanyia kazi, wala kuukomalisha; uliota usiku mumoja na kukauka usiku mumoja. 11 Je, singepaswa pia kusikilia huruma Ninawi muji mukubwa,+ wenye kuwa na watu zaidi ya elfu mia moja makumi mbili (120 000) wenye hawajue hata kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa,* na pia wanyama wao wengi?”+
Maana yake “Njiwa.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “ninamuabudu.”
Kasia ni chombo chenye kufanana na mwiko chenye kinatumiwa kuendesha mashua.
Ao “wakajaribu kupasua njia.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “kwa sababu ya nafsi ya mutu huyu!”
Tnn., “Katika tumbo la.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Maji yalinizunguka mupaka kwenye nafsi.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Ao “nafsi yangu ilikuwa inakaribia.”
Ao pengine, “ushikamanifu wao.”
Tnn., “muji mukubwa kwa Mungu.”
Ao “hatasikitika.”
Ao “akasikitika.”
Ao “neema.”
Ao “nafsi yangu.”
Ao pengine, “mbarika; mbono.”
Ni kusema, wakati mwangaza wa asubui ulianza kutokea.
Ao “nafsi yake ikufe.”
Ao “tofauti kati ya mukono wao wa kuume na wa kushoto.”