NAHUMU
1 Tangazo juu ya Ninawi:+ Kitabu cha maono ya Nahumu* Mwelkoshi:
2 Yehova ni Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu+ na ni mwenye kulipiza kisasi;
Yehova analipiza kisasi na iko* tayari kuonyesha kasirani yake.+
Yehova analipiza kisasi juu ya wapinzani wake,
Na anawekea maadui wake kasirani kali.
3 Yehova hakasirike haraka+ na ni mwenye nguvu nyingi,+
Lakini Yehova hatakosa hata kidogo kutoa azabu yenye kustahili.+
Njia yake iko katika upepo wenye kuharibu na katika zoruba,
Na mawingu ni vumbi ya miguu yake.+
Bashani na Karmeli zinakauka,+
Na maua ya Lebanoni yanakauka.
5 Milima inatetemeka kwa sababu yake,
Na vilima vinayeyuka.+
Dunia itainuka kwa sababu ya uso wake,
Pamoja na inchi na wale wote wenye kukaa ndani yake.+
6 Ni nani mwenye anaweza kusimama mbele ya kasirani yake kali?+
Ni nani mwenye anaweza kuvumilia joto la hasira yake?+
Atamwanga kasirani yake kama moto,
Na miamba itapasuka vipande-vipande kwa sababu yake.
7 Yehova ni mwema,+ naye ni ngome katika siku ya taabu.+
Hasahau* wenye wanatafuta kimbilio katika yeye.+
8 Kupitia mafuriko yenye kufagia ataharibu mahali pake kwa ukamili,*
Na giza litafuatilia maadui wake.
9 Mutafanya mupango gani mubaya juu ya Yehova?
Yeye ataleta uharibifu kamili.
Taabu haitatokea tena mara ya pili.+
10 Kwa sababu wamesukwa kama miiba,
Na wako kama watu wenye kulewa pombe;*
Lakini watateketea kwa moto kama nyasi yenye kukauka.
11 Katikati yenu atatokea mutu mwenye kupanga uovu juu ya Yehova,
Mwenye kutoa mashauri yenye hayana mafaa yoyote.
12 Yehova anasema hivi:
“Hata kama walikuwa na nguvu nyingi na walikuwa wengi,
Hata katika hali hiyo watakatwa na kupotea kabisa.*
Nimekutesa,* lakini sitaendelea kukutesa.
13 Na sasa nitavunja nira yake na kuiondoa juu yako,+
Na nitakata pingu zako vipande mbili.
14 Yehova ameamuru hivi juu yako:*
‘Jina lako halitaendelezwa tena.
Nitaharibu sanamu za kuchongwa na sanamu za metali* zenye kuwa katika nyumba ya* miungu yako.
Nitakuchimbia kaburi, kwa sababu wewe ni mwenye kuchukiza sana.’
Ufanye sikukuu zako,+ Ee Yuda, utimize naziri zako,
Kwa sababu mutu mwenye hana mafaa yoyote hatapita katikati yenu tena hata siku moja.
Ataharibiwa kabisa.”
2 Mutu mwenye kutawanya amekushambulia.*+
Ulinde ngome.
Ulinde njia.
Ujitayarishe* na ukusanye nguvu yako yote.
2 Kwa sababu Yehova atarudisha kiburi cha Yakobo,
Na kiburi cha Israeli,
Kwa sababu watu wenye kuacha ukiwa wamewaacha ukiwa;+
Na wameharibu machipukizi yao.
3 Ngao za wanaume wake wenye nguvu zimepakwa rangi nyekundu,
Wapiganaji-vita wake wamevaa nguo nyekundu sana.
Vyuma vya magari yao ya vita vinawaka kama moto,
Muchana anajitayarisha kwa ajili ya vita,
Na mikuki ya muberoshi imeinuliwa.
4 Magari ya vita yanaenda kiwazimu katika barabara.
Yanakimbia-kimbia katika viwanja vya watu wengi.
Yanangaa kama mienge yenye kuwaka na kuangaza kama umeme wa radi.
5 Ataita maofisa wake.
Watajikwaa wakati wanatembea.
Wanakimbilia kwenye ukuta wa muji;
Na wanaweka kizuizi.
7 Amri imetolewa: Amefunuliwa,
Amebebwa, na wafanyakazi wake wanamuke wanaomboleza;
Wanalia kama njiwa na kujipiga vifua.*
“Musimame wima! Musimame wima!”
Lakini hakuna mwenye kugeuka.+
9 Munyanganye feza, munyanganye zahabu!
Hazina zake hazina mwisho.
Inajaa vitu mbalimbali vyenye samani.
10 Muji hauna kitu ndani yake, umeachwa ukiwa, umeharibiwa!+
Mioyo yao inayeyuka kwa woga, magoti yao yanajikunja, viuno vyao vinatetemeka;
Nyuso zao zote zimejaa wasiwasi.
11 Liko wapi shimo la simba,+ mahali wana-simba* wanakula,
Mahali kwenye simba anapeleka kitoto chake,
Bila mutu wa kuwaogopesha?
12 Simba alipasua mawindo ya kutosha kwa ajili ya vitoto vyake
Na aliua wanyama kwa ajili ya simba-dike wake.
Alijaza mawindo katika mashimo yake,
Na wanyama wenye kupasuliwa katika mashimo yake.
13 “Angalia! Nitapambana na wewe,” ni vile Yehova wa majeshi anasema,+
“Nitateketeza kwa moto magari yake ya vita,+
Na upanga utameza wana-simba wako.*
Nitaondoa mawindo yako katika dunia,
Na sauti ya wajumbe wako haitasikiwa tena.”+
3 Ole wake muji wenye kumwanga damu!
Umejaa sana udanganyifu na unyanganyi.
Hakuna siku unakuwa bila mawindo!
2 Kuko sauti ya fimbo na mulio wa magurudumu,*
Farasi mwenye kukimbia mbio na gari lenye kuruka-ruka.
3 Mupanda-farasi mwenye kuwa juu ya farasi, upanga wenye kumetameta, na mukuki wenye kungaa,
Watu wengi wenye waliuawa na marundo ya mizoga
—Maiti hazina hesabu.
Watu wanakwaa juu ya maiti.
4 Hiyo ni kwa sababu ya matendo mengi ya ukahaba ya ule kahaba,
Mwenye kupendeza na mwenye kuvutia, mwanamuke mwenye kujua sana mambo ya uchawi,
Mwenye kunasa mataifa kupitia ukahaba wake na familia nyingi kupitia uchawi wake.
5 “Angalia! Nitapambana na wewe,”* ni vile Yehova wa majeshi anasema,+
“Nitapandisha sehemu za chini za nguo zako mupaka kwenye uso wako;
Nitaacha mataifa yaone uchi wako,
Na falme zione haya yako.
Ni nani atausikilia huruma?’
Nitapata wapi watu wa kukufariji?
8 Je, wewe ni mwema sana kuliko No-amoni,*+ mwenye alikaa pembeni ya mifereji ya Muto Nile?+
Maji yalimuzunguka;
Utajiri wake ulikuwa bahari na ukuta wake ulikuwa bahari.
9 Etiopia ilikuwa chanzo cha nguvu zake nyingi, na Misri pia.
Waputu+ na Walibya walikuwa wanakusaidia.+
10 Hata hivyo No-amoni pia alipelekwa katika uhamisho;
Alienda katika utekwa.+
Watoto wake pia walivunjwa vipande-vipande kwenye kila makutano ya barabara.*
Walipiga kura ili kuchukua waheshimiwa wake,
Na wakubwa wake wote wamefungwa kwa pingu.
11 Utalewa pia;+
Utaenda kujificha.
Utamukimbia adui na kujificha.
12 Ngome zako zote ni kama miti ya tini yenye kuwa na matunda ya kwanza yenye kukomaa;
Kama inatikiswa, matunda yake yataanguka katika kinywa cha watu wenye kumeza.
13 Angalia! Majeshi yako ni kama wanamuke katikati yako.
Milango mikubwa ya inchi yako itakuwa wazi kwa ajili ya maadui wako.
Moto utateketeza mapingo* ya milango yako mikubwa.
14 Ushote maji kwa sababu utazungukwa kwa ajili ya vita!+
Utie ngome zako nguvu.
Ingia katika matope na ukanyange udongo;
Shika sana chombo cha kutengenezea matofali.
15 Hata kule moto utakuteketeza.
Upanga utakuangamiza.+
Utakumeza kama vile nzige wadogo wanafanya.+
Ongezeka kama nzige wadogo!
Ndiyo, ongezeka kama nzige!
16 Umeongeza wafanyabiashara wako kuliko nyota za mbinguni.
Nzige mudogo anavua ngozi yake na anaruka mbali.
17 Walinzi wako ni kama nzige,
Na maofisa wako ni kama kundi la nzige.
Wanapiga kambi katika mazizi* ya majiwe siku ya baridi,
Lakini wakati jua linawaka, wanaruka mbali;
Na hakuna mwenye anajua kwenye wako.
18 Wachungaji wako wanasinzia, Ee mufalme wa Ashuru;
Watu wako wenye vyeo wanakaa katika makao yao.
Watu wako wametawanyika kwenye milima,
Na hakuna mutu wa kuwakusanya pamoja.+
19 Hakuna mwenye atakutuliza wakati utapatwa na musiba.
Kidonda chako hakiwezi kupona.
Wote wenye watasikia habari zako watapiga mikono;+
Kwa sababu ni nani mwenye haukutendea kwa ukali wenye hauna mwisho?”+
Maana yake “Mufariji.”
Ao “eko.”
Ao “Anawatunza.” Tnn., “Anawajua.”
Ni kusema, mahali pa Ninawi.
Ao “pombe ya ngano.”
Ao pengine, “na yeye atapita.”
Ni kusema, Yuda.
Ni kusema, Ashuru.
Ao “sanamu za kuyeyushwa.”
Ao “hekalu la.”
Ni kusema, Ninawi.
Tnn., “Tia nguvu viuno.”
Ao “itaporomoka.”
Tnn., “mioyo.”
Ao “wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Ao “wana-simba wako wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Ao “mipeto; pneus.”
Ni kusema, Ninawi.
Ni kusema, Tebesi.
Tnn., “kwenye kichwa cha barabara zote.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.