Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 3/14 uku. 8-9
  • Feza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Feza
  • Amuka!—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Feza ndizo zinaleta mambo yote mabaya?
  • Feza zinasaidia watu namna gani?
  • Namna gani unaweza kutumia feza kwa hekima?
  • Makuta Njo Chanzo ya Mambo Yote ya Mubaya?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Namna ya Kuwa na Mawazo ya Muzuri Juu ya Feza
    Amuka!—2015
  • Namna ya Kutumia Feza Vizuri
    Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
Amuka!—2014
g 3/14 uku. 8-9
Marundo ya feza katika chumba chenye kufunguliwa

MAONI YA BIBLIA

Feza

Feza ndizo zinaleta mambo yote mabaya?

“Kupenda [feza] ni chanzo cha mambo mabaya ya namna zote.”​—1 Timotheo 6:10.

MAMBO WATU FULANI WANASEMA:

Feza ndizo zinaleta mambo yote mabaya.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

Ni “kupenda [feza]” ndiko kunaleta “mambo mabaya,” wala si feza zenyewe. Katika Biblia, Mufalme Sulemani aliyekuwa tajiri sana, alionyesha mambo tatu mabaya yanayopata watu wanaopenda feza. Jambo la 1, woga: ‘Wingi alio nao tajiri haumuruhusu kulala.’ (Mhubiri 5:12) Jambo la 2, kukosa kutosheka: ‘Anayependa feza hatatosheka na feza, wala anayependa mali hatatosheka na mapato.’ (Mhubiri 5:10) Jambo la 3, kishawishi cha kuvunja sheria: “Yeye anayefanya haraka kupata utajiri hatabaki pasipo hatia.”​—Methali 28:20.

Feza zinasaidia watu namna gani?

“[Feza] ni ulinzi.”​—Mhubiri 7:12.

MAMBO WATU FULANI WANASEMA:

Feza zinamufanya mutu kuwa salama na zinamuletea furaha.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

Wazo la kwamba feza zinanunua furaha na usalama ni sehemu ya “nguvu za udanganyifu za utajiri.” (Marko 4:19) Hata hivyo, ‘[feza] zinatokeza jibu katika mambo yote.’ (Mhubiri 10:19) Kwa mufano, feza zinaweza kununua vitu ambavyo mutu anahitaji ili aendelee kuishi, vitu kama vile chakula na dawa.—​2 Wathesalonike 3:12.

Feza zinamusaidia pia mutu kutunza familia yake. Kwa kweli, Biblia inasema hivi: ‘Ikiwa yeyote hawaandalie mahitaji wale walio wake mwenyewe, na hasa wale walio washiriki wa nyumba yake, ameikana imani.’​—1 Timotheo 5:8.

Namna gani unaweza kutumia feza kwa hekima?

‘Uketi kwanza na uhesabu garama.’​—Luka 14:28.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

Utumie feza kwa njia ambayo Mungu anakubali. (Luka 16:9) Ni jambo la hekima kutumia feza vizuri na kwa njia ya haki. (Waebrania 13:18) Ili kuepuka muzigo wa kutumia feza nyingi zaidi ya zile unazopata, ufanye ‘namna yako ya maisha iwe bila upendo wa [feza].’​—Waebrania 13:5.

Hata ikiwa Biblia haikataze kuomba deni, inaonya hivi: ‘Mukopaji ni mutumishi wa mutu anayemukopesha.’ (Methali 22:7) Epuka kununua vitu bila mupango, kwa sababu ‘kila mutu anayetenda haraka-haraka bila shaka anaelekea uhitaji.’ (Methali 21:5) Lakini, ‘weka kando kitu fulani katika akiba kulingana na unavyofanikiwa,’ na uweke feza juu ya mambo yaliyo ya maana kwako.​—1 Wakorintho 16:2.

Biblia inatutia moyo ‘tuwe na mazoea ya kuwapa watu.’ (Luka 6:38) Watu wanaotaka kumupendeza Mungu wana sababu nzuri ya kuwa wakarimu, kwa kuwa ‘Mungu anamupenda mutoaji muchangamufu.’ (2 Wakorintho 9:7) Kwa hiyo, ‘musisahau kutenda mema na kushiriki vitu pamoja na wengine, kwa maana Mungu anapendezwa vema na zabihu za namna hiyo.’​—Waebrania 13:16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine