Ndoa
Nani njo alianzishaka ndoa?
Nani njo Mukristo anapaswa kuchagua kuwa bibi ao bwana yake?
Juu ya nini Wakristo wa kweli hawapaswe kuruhusu mutoto wao afunge ndoa na mutu mwenye haiko mutumishi wa Yehova mwenye kujitoa na kubatizwa?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mwa 24:1-4, 7—Abrahamu mwenye alishazeeka anaamua kutafutia mutoto wake Isaka bibi kati ya watumishi wa Yehova, hapana kati ya Wakanaani, wenye wanaabudu miungu ingine
Mwa 28:1-4—Isaka anaambia mutoto wake Yakobo atafute bibi kati ya waamini wenzake, hapana kati ya Wakanaani
Yehova anajisikiaka namna gani wakati Mukristo anaoana na mutu mwenye haiko mwamini?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
1Fa 11:1-6, 9-11—Yehova anamukasirikia Mufalme Sulemani juu anazarau amri ya Mungu na anaoa bibi wengi na kuwaruhusu wapotoshe moyo wake
Ne 13:23-27—Sawa Yehova, Gavana Nehemia anakasirika na anapatia azabu Waisraeli wenye wanaoa wanamuke wenye hawamutumikie Yehova
Juu ya nini ni jambo ya hekima kuoana na mutu mwenye iko namutumikia Yehova kwa uaminifu na mwenye iko na sifa za muzuri?
Ona pia Efe 5:28-31, 33
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
1Sa 25:2, 3, 14-17—Nabali ni mwanaume tajiri, lakini iko mukali na hatendee wengine muzuri; ile inafanya Abigaili amuone kuwa maskini
Mez 21:9—Kama tunachagua mubaya mutu mwenye tutaoana naye, ile inaweza kufanya tukose furaha na amani
Ro 7:2—Mutume Paulo anaonyesha kama wakati mwanamuke anaolewa, anakuwa chini ya mamlaka ya bwana yake mwenye hakamilike; njo maana ni jambo ya lazima mwanamuke akuwe muangalifu wakati anachagua mutu mwenye ataolewa naye
Kujitayarisha kwa ajili ya ndoa
Juu ya nini mwanaume anapaswa kuwa tayari kutegemeza familia mbele ya kufikiria kuoa?
Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:
Mez 24:27—Mbele mwanaume aoe na pengine afikie kuwa na watoto, anapaswa kutumika sana juu aweze kutegemeza familia
Juu ya nini watu wenye kuchumbiana wanapaswa kuhangaikia sana kutafuta mashauri ya hekima na kujuana muzuri kuliko kuhangaikia zaidi sura?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Rut 2:4-7, 10-12—Boazi anajikaza kumujua Rutu kwa kuchunguza namna iko najitoa mu kazi na pia kwa kufikiria ripoti ya muzuri yenye anapata juu ya sifa zake, namna anatendea watu wa familia yake, na hali yake ya kiroho
Rut 2:8, 9, 20—Rutu anamujua Boazi kwa kuona namna iko mwenye fazili, mukarimu, na namna anamupenda Yehova
Juu ya nini Yehova anapenda watu wenye kuchumbiana waendelee kuwa na mwenendo safi?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mez 5:18, 19—Matendo fulani ya kuonyeshana upendo ni ya watu wenye walishaoana tu
Wim 1:2; 2:6—Wakati wa uchumba, kijana muchungaji na mwanamuke Mushulami wanaonyeshana upendo mu njia ya muzuri
Wim 4:12; 8:8-10—Mwanamuke Mushulami anaendelea kuwa na mwenendo safi na anajizuia; iko sawa bustani yenye kufungwa
Juu ya nini bibi na bwana wanapaswa kuoana kulingana na sheria?
Daraka ya bwana
Bwana iko na madaraka gani mazito?
Bwana Wakristo wanapaswa kuiga mufano wa nani?
Juu ya nini ni jambo ya maana bwana ajikaze kuelewa bibi yake na kumutendea kwa upendo?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mwa 21:8-12—Yehova anamuomba Abrahamu amusikilize bibi yake, Sara, hata kama mawazo ya Sara haimufurahishe Abrahamu
Mez 31:10, 11, 16, 28—Bwana mwenye hekima wa mwanamuke mwenye uwezo, vile hii andiko inaonyesha, hachunguze-chunguze bibi yake wala kutafuta makosa, lakini anamutumainia na kumusifu
Efe 5:33—Maneno ya mutume Paulo yenye kuongozwa na roho inaonyesha kama mwanamuke anahangaikiaka zaidi kujisikia kuwa bwana yake anamupenda
Daraka ya bibi
Yehova alipatia bibi Wakristo daraka gani?
Daraka yenye Yehova amepatia bibi inamushushia heshima?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mez 1:8; 1Ko 7:4—Mu ndoa na mu familia, bibi na mama wako na mamlaka kwa kiasi fulani
1Ko 11:3—Mutume Paulo anafasiria kama mu mupango wa Mungu, viumbe wote wako chini ya ukichwa, isipokuwa tu Mungu mwenye ni Mweza-Yote
Ebr 13:7, 17—Mu kutaniko, ikuwe wanaume ao wanamuke, wote wanapaswa kujitiisha kwa wale wenye kuongoza
Namna gani bibi mwenye iko na bwana mwenye haiko Mukristo anaweza kumufurahisha Yehova?
Juu ya nini bibi Mukristo anapaswa kuendelea kuheshimia bwana yake?
Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:
Mwa 18:12; 1Pe 3:5, 6—Sara anamuheshimia kabisa bwana yake, anamuona kuwa “bwana” wake
Biblia inasifu bibi wa namna gani?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mwa 24:62-67—Rebeka anamusaidia bwana yake Isaka apate kitulizo kisha kifo ya mama yake
1Sa 25:14-24, 32-38—Abigaili analinda bwana yake mupumbavu na anaokoa nyumba yake kwa kujinyenyekeza mbele ya Daudi
Est 4:6-17; 5:1-8; 7:1-6; 8:3-6—Mara mbili, malkia Esta anatia uzima wake mu hatari kwa kuenda kumuona bwana yake, mufalme, bila kuitwa, juu ya kutetea watu wa Mungu