Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • scl uku. 72-76
  • Ndoa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ndoa
  • Maandiko ya Kutusaidia mu Maisha ya Kikristo
Maandiko ya Kutusaidia mu Maisha ya Kikristo
scl uku. 72-76

Ndoa

Nani njo alianzishaka ndoa?

Mwa 1:​27, 28; 2:​22-24; Mt 19:​4-6

Nani njo Mukristo anapaswa kuchagua kuwa bibi ao bwana yake?

Juu ya nini Wakristo wa kweli hawapaswe kuruhusu mutoto wao afunge ndoa na mutu mwenye haiko mutumishi wa Yehova mwenye kujitoa na kubatizwa?

1Ko 7:39; 2Ko 6:​14, 15

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 24:​1-4, 7—Abrahamu mwenye alishazeeka anaamua kutafutia mutoto wake Isaka bibi kati ya watumishi wa Yehova, hapana kati ya Wakanaani, wenye wanaabudu miungu ingine

    • Mwa 28:​1-4—Isaka anaambia mutoto wake Yakobo atafute bibi kati ya waamini wenzake, hapana kati ya Wakanaani

Yehova anajisikiaka namna gani wakati Mukristo anaoana na mutu mwenye haiko mwamini?

Kum 7:​3, 4

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Fa 11:​1-6, 9-11—Yehova anamukasirikia Mufalme Sulemani juu anazarau amri ya Mungu na anaoa bibi wengi na kuwaruhusu wapotoshe moyo wake

    • Ne 13:​23-27—Sawa Yehova, Gavana Nehemia anakasirika na anapatia azabu Waisraeli wenye wanaoa wanamuke wenye hawamutumikie Yehova

Juu ya nini ni jambo ya hekima kuoana na mutu mwenye iko namutumikia Yehova kwa uaminifu na mwenye iko na sifa za muzuri?

Mez 18:22; 31:​10, 28

Ona pia Efe 5:​28-31, 33

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 25:​2, 3, 14-17—Nabali ni mwanaume tajiri, lakini iko mukali na hatendee wengine muzuri; ile inafanya Abigaili amuone kuwa maskini

    • Mez 21:9—Kama tunachagua mubaya mutu mwenye tutaoana naye, ile inaweza kufanya tukose furaha na amani

    • Ro 7:2—Mutume Paulo anaonyesha kama wakati mwanamuke anaolewa, anakuwa chini ya mamlaka ya bwana yake mwenye hakamilike; njo maana ni jambo ya lazima mwanamuke akuwe muangalifu wakati anachagua mutu mwenye ataolewa naye

Kujitayarisha kwa ajili ya ndoa

Juu ya nini mwanaume anapaswa kuwa tayari kutegemeza familia mbele ya kufikiria kuoa?

1Ti 5:8

  • Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:

    • Mez 24:27—Mbele mwanaume aoe na pengine afikie kuwa na watoto, anapaswa kutumika sana juu aweze kutegemeza familia

Juu ya nini watu wenye kuchumbiana wanapaswa kuhangaikia sana kutafuta mashauri ya hekima na kujuana muzuri kuliko kuhangaikia zaidi sura?

Mez 13:10; 1Pe 3:​3-6

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Rut 2:​4-7, 10-12—Boazi anajikaza kumujua Rutu kwa kuchunguza namna iko najitoa mu kazi na pia kwa kufikiria ripoti ya muzuri yenye anapata juu ya sifa zake, namna anatendea watu wa familia yake, na hali yake ya kiroho

    • Rut 2:​8, 9, 20—Rutu anamujua Boazi kwa kuona namna iko mwenye fazili, mukarimu, na namna anamupenda Yehova

Juu ya nini Yehova anapenda watu wenye kuchumbiana waendelee kuwa na mwenendo safi?

Gal 5:19; Kol 3:5; 1Te 4:4

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mez 5:​18, 19—Matendo fulani ya kuonyeshana upendo ni ya watu wenye walishaoana tu

    • Wim 1:2; 2:6—Wakati wa uchumba, kijana muchungaji na mwanamuke Mushulami wanaonyeshana upendo mu njia ya muzuri

    • Wim 4:12; 8:​8-10—Mwanamuke Mushulami anaendelea kuwa na mwenendo safi na anajizuia; iko sawa bustani yenye kufungwa

Juu ya nini bibi na bwana wanapaswa kuoana kulingana na sheria?

Mt 22:21; Ro 13:1; Tit 3:1

Daraka ya bwana

Bwana iko na madaraka gani mazito?

Efe 5:​23, 25, 28-31, 33

Bwana Wakristo wanapaswa kuiga mufano wa nani?

1Ko 11:3; Efe 5:23

Juu ya nini ni jambo ya maana bwana ajikaze kuelewa bibi yake na kumutendea kwa upendo?

Kol 3:19; 1Pe 3:7

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 21:​8-12—Yehova anamuomba Abrahamu amusikilize bibi yake, Sara, hata kama mawazo ya Sara haimufurahishe Abrahamu

    • Mez 31:​10, 11, 16, 28—Bwana mwenye hekima wa mwanamuke mwenye uwezo, vile hii andiko inaonyesha, hachunguze-chunguze bibi yake wala kutafuta makosa, lakini anamutumainia na kumusifu

    • Efe 5:33—Maneno ya mutume Paulo yenye kuongozwa na roho inaonyesha kama mwanamuke anahangaikiaka zaidi kujisikia kuwa bwana yake anamupenda

Daraka ya bibi

Yehova alipatia bibi Wakristo daraka gani?

Mwa 2:18; Kol 3:18; Tit 2:​4, 5

Daraka yenye Yehova amepatia bibi inamushushia heshima?

Mwa 1:​26-28, 31; 2:18

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mez 1:8; 1Ko 7:4—Mu ndoa na mu familia, bibi na mama wako na mamlaka kwa kiasi fulani

    • 1Ko 11:3—Mutume Paulo anafasiria kama mu mupango wa Mungu, viumbe wote wako chini ya ukichwa, isipokuwa tu Mungu mwenye ni Mweza-Yote

    • Ebr 13:​7, 17—Mu kutaniko, ikuwe wanaume ao wanamuke, wote wanapaswa kujitiisha kwa wale wenye kuongoza

Namna gani bibi mwenye iko na bwana mwenye haiko Mukristo anaweza kumufurahisha Yehova?

1Ko 7:​13-16; 1Pe 3:​1, 2

Juu ya nini bibi Mukristo anapaswa kuendelea kuheshimia bwana yake?

Efe 5:33

  • Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:

    • Mwa 18:12; 1Pe 3:​5, 6—Sara anamuheshimia kabisa bwana yake, anamuona kuwa “bwana” wake

Biblia inasifu bibi wa namna gani?

Mez 19:14; 31:​10, 13-31

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 24:​62-67—Rebeka anamusaidia bwana yake Isaka apate kitulizo kisha kifo ya mama yake

    • 1Sa 25:​14-24, 32-38—Abigaili analinda bwana yake mupumbavu na anaokoa nyumba yake kwa kujinyenyekeza mbele ya Daudi

    • Est 4:​6-17; 5:​1-8; 7:​1-6; 8:​3-6—Mara mbili, malkia Esta anatia uzima wake mu hatari kwa kuenda kumuona bwana yake, mufalme, bila kuitwa, juu ya kutetea watu wa Mungu

Kumaliza matatizo

Ni kanuni gani za Biblia zinaweza kusaidia bibi na bwana wamalize matatizo mu ndoa?

1Ko 13:​4-8; Efe 5:33; Kol 3:​12-14

Ni kanuni gani za Biblia zinaweza kusaidia bibi na bwana wakuwe na mawazo yenye usawaziko juu ya makuta?

Lu 12:15; Flp 4:5; 1Ti 6:​9, 10; Ebr 13:5

Ona “Makuta”

Ni kanuni gani za Biblia zinaweza kusaidia bibi na bwana wamalize matatizo yenye inahusu watu wa familia na wakwe?

Zb 34:14; Mt 19:​5, 6; 1Ko 13:​4, 5

Ni kanuni gani za Biblia zinaweza kusaidia bibi na bwana kuhusu ngono?

Mez 5:​15-20; Mt 5:​27, 28; 1Ko 7:​3-5; 10:24; Flp 2:4; Ebr 13:4

Juu ya nini ni muzuri kuangalia zaidi sifa za muzuri za bibi ao bwana kuliko kuonaka tu makosa?

Zb 103:14; 130:​3, 4; Mez 17:9; 1Pe 4:8

Juu ya nini ni muzuri kumaliza matatizo kwa upendo na bila kukawia kuliko kubakia na mambo ku roho na kuacha kasirani iendelee?

Zb 37:8; Mez 14:29; Efe 4:​26, 27; Yak 1:​19, 20

Juu ya nini Mukristo hapaswe kukasirika kupita mipaka, kufoka, kusema mutu mubaya, na kumutendea mubaya?

Zb 11:5; Gal 5:​19-21; Efe 4:​31, 32; Tit 3:2

Wakati kunatokea hali ya kutoelewana, bibi na bwana wanapaswa kuwa na kusudi gani?

Zb 34:14; Mt 5:9; Ro 12:​17, 18, 21

Ndoa yenye inamutegemea Yehova inapataka baraka gani?

Muh 4:​9-12

Kanuni zenye zinahusu ndoa

Biblia inasema nini juu ya mambo ya ngono na ndoa?

Mez 6:32; Mt 5:​27, 28; 1Ko 6:​9, 10; Ebr 13:4

Mukristo anapaswa kuwa na mawazo gani kuhusu kuoa bibi wengi?

Mt 19:​8, 9; 1Ko 7:2; 1Ti 3:​2, 12

Tunajua namna gani kama ndoa inapaswa kuwa tu kati ya mwanaume na mwanamuke?

Mwa 2:​18, 22, 24; Mt 19:​4-6; Ro 1:​23-27

Juu ya nini watu wenye wameoana wanapaswa kuendelea kuwa pamoya?

Mk 10:​6-9; Ro 7:​2, 3; 1Ko 7:​10, 11

Ni sababu gani moya tu njo inaweza kufanya Wakristo wavunje ndoa?

Mt 5:32; 19:9

Yehova anajisikiaka namna gani wakati Wakristo wanavunja ndoa bila sababu ya kimaandiko?

Mal 2:​13-16

Wakati bibi ao bwana anakufa, ule mwenye anabakia anaweza kuoa ao kuolewa tena?

Ro 7:​2, 3; 1Ko 7:39

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine