Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 15/2 uku. 17-21
  • Tubaki Katika Bonde la Ulinzi la Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tubaki Katika Bonde la Ulinzi la Yehova
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘SIKU YA YEHOVA’ INAANZA
  • YEHOVA ANATOKEZA “BONDE KUBWA SANA”
  • WATU WANAANZA KUKIMBILIA KATIKA BONDE
  • ‘SIKU YA VITA’ INAANZA
  • ‘MAJI YA UZIMA YATATOKA’
  • Bakia “Katika Bonde la Milima”
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Taji na Magari ya Kukokotwa Vinawalinda
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 15/2 uku. 17-21
[Picha katika ukurasa wa 17]

Tubaki Katika Bonde la Ulinzi la Yehova

‘Yehova atapiga vita juu ya mataifa hayo kama katika siku yake ya vita, katika siku ya pigano.’​—ZEK. 14:3.

UNAWEZA KUELEZA?

  • Kupasuka kwa ‘mulima wa mizeituni’ kunafananisha nini?

  • “Bonde kubwa sana” linafananisha nini, na tunapaswa kufanya nini ili kubaki katika bonde hilo?

  • ‘Maji ya uzima’ yanafananisha nini, na ni nani watakaoyakunywa?

1, 2. Ni vita gani isiyo ya kuwazia itakayotokea hivi karibuni, na watumishi wa Mungu hawatafanya nini wakati wa vita hiyo?

MANGARIBI moja ya tarehe 30 Mwezi wa 10, 1938, mamilioni ya watu katika États-Unis walifuata kwenye radio programu moja iliyopendwa sana. Programu ya mangaribi hiyo ilitokana na kitabu kimoja cha hadisi ya kuwazia. Programu hiyo ilitangaza kwamba viumbe fulani wa planeti ya Marse wataishambulia Dunia yote na kuiharibu. Ijapokuwa ilitangazwa kwamba programu hiyo ilikuwa tu muchezo, wasikilizaji wengi walifikiri kama mambo hayo yalikuwa ya kweli na waliogopa sana. Wengine hata walichukua mipango fulani ili kujaribu kujilinda na viumbe hao.

2 Lakini, kuna vita isiyo ya kuwazia itakayotokea hivi karibuni. Hata hivyo, watu wengi hawahangaike hata kidogo kuhusu vita hiyo. Vita hiyo haizungumuziwe katika kitabu fulani cha hadisi za kuwazia, lakini katika Neno lililoongozwa na roho ya Mungu, Biblia. Vita hiyo ni Har-magedoni, ni kusema, vita ya Mungu ya kuondoa ulimwengu huu muovu. (Ufu. 16:14-16) Vita hiyo itakapoanza, watumishi wa Mungu hapa duniani hawatapigana na maadui fulani wa planeti ingine. Lakini, watajionea mambo ya ajabu na yenye kuogopesha ambayo Mungu atafanya.

3. Tutazungumuzia unabii gani, na sababu gani kufanya hivyo ni kwa faida yetu?

3 Unabii wa Biblia unaopatikana katika sura ya 14 ya kitabu cha Zekaria unazungumuzia sana vita hiyo ya Har-magedoni. Hata ikiwa uliandikwa miaka 2 500 hivi iliyopita, unabii huo ni wa maana kwetu leo. (Rom. 15:4) Unabii huo unazungumuzia mambo mengi ambayo yaliwapata watu wa Mungu kuanzia mwaka wa 1914, wakati Ufalme wa Masiya ulisimamishwa mbinguni, na unazungumuzia mambo yenye kufurahisha yatakayotokea hivi karibuni. Unabii huo unazungumuzia “bonde kubwa sana” na ‘maji ya uzima.’ (Zek. 14:4, 8) Bonde hilo lina kazi ya lazima sana ya kuwalinda waabudu wa Yehova. Na tutakapoelewa maana ya maji hayo ya uzima, tutatambua kwamba ni lazima kukunywa maji hayo na tutakuwa na hamu ya kuyakunywa. Kwa hiyo, ni kwa faida yetu ikiwa tunakazia unabii huo uangalifu.​—2 Pet. 1:19, 20.

‘SIKU YA YEHOVA’ INAANZA

4. (a) ‘Siku ya Yehova’ ilianza wakati gani? (b) Miaka mingi mbele ya mwaka wa 1914, watumishi wa Yehova walikuwa wanatangaza nini, na viongozi wa serikali na wa dini walitenda namna gani?

4 Sura ya 14 ya kitabu cha Zekaria inaanza kwa kuzungumuzia ‘siku ya Yehova.’ (Soma Zekaria 14:1, 2.) Siku hiyo ni nini? Ni “siku ya Bwana” iliyoanza wakati “ufalme wa ulimwengu” ulipoanza kuwa “ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake.” (Ufu. 1:10; 11:15) Siku hiyo ilianza katika mwaka wa 1914, wakati Ufalme wa Masiya ulianza kutawala mbinguni. Miaka mingi mbele ya 1914, watumishi wa Yehova walitangazia mataifa kwamba “nyakati zilizowekwa za mataifa” zingemalizika mwaka huo na kwamba ulimwengu ungeingia katika kipindi cha muvurugo ambao ulikuwa haujatokea mbele. (Lu. 21:24) Mataifa yalitenda namna gani? Kuliko kutii maonyo hayo yaliyotolewa kwa wakati unaofaa, viongozi wa serikali na wa dini walicheka wahubiri hao watiwa-mafuta na kuwatesa. Kwa kufanya hivyo, viongozi hao walimuzarau Mungu Mweza-yote, kwa kuwa wahubiri watiwa-mafuta, ambao ni mabalozi (ao ambasadere) wa Ufalme wanawakilisha “Yerusalemu la mbinguni” ao Ufalme wa Masiya.​—Ebr. 12:22, 28.

5, 6. (a) Kulingana na unabii, mataifa yangetendea “jiji” na ‘raia’ wake namna gani? (b) ‘Watu waliobaki’ walikuwa nani?

5 Zekaria alitabiri kwamba mataifa ‘yangekamata jiji [la Yerusalemu].’ “Jiji” hilo linamaanisha Ufalme wa Mungu unaoongozwa na Masiya. Ufalme huo unawakilishwa hapa duniani na ‘raia,’ wake ao mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta. (Flp. 3:20) Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, wasimamizi wa sehemu yenye kuonekana ya tengenezo la Yehova hapa duniani, ‘walikamatwa’ na kupelekwa katika gereza huko Atlanta, Géorgie, États-Unis. Wakati wasimamizi hao na watumishi wengine waaminifu walitendewa isivyo haki na kinyama, ‘nyumba ziliporwa,’ ao kuvunjwa. Washambuliaji walinyanganya ao kuiba mali ambayo mabaki walikuwa wanatumia, ni kusema, walikataza vichapo vyao na kazi ya kuhubiri.

6 Hata ikiwa watu wa Yehova walikuwa wachache, walisingiziwa, walipingwa, na kuteswa na maadui wao, maadui hao hawakuweza kumaliza ibada ya kweli. Kulikuwa ‘watu waliobaki,’ ao mabaki watiwa-mafuta ambao walikataa kwa uaminifu ‘kukatiliwa mbali kutoka katika jiji.’

7. Wakristo watiwa-mafuta wametuachia mufano gani?

7 Je, sehemu zote za unabii zilitimia mwishoni mwa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu? Hapana. Katika siku ambazo zingefuata mataifa yangeshambulia tena mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta na wenzao walio na tumaini la kuishi duniani. (Ufu. 12:17) Mambo yaliyotokea wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu yanashuhudia jambo hilo. Uaminifu ambao Wakristo watiwa​-mafuta walionyesha unawatia moyo watumishi wa Mungu leo wavumilie majaribu yoyote yanayoweza kuwapata, kama vile upinzani wa watu wa familia, wafanyakazi, ao wanafunzi wenzao wanaowacheka kwa sababu ya imani yao. (1 Pet. 1:6, 7) Mahali popote wanapoishi, waabudu wa kweli wameazimia sana ‘kusimama imara katika roho moja,’ na ‘kutowaogopa wapinzani wao.’ (Flp. 1:27, 28) Kwa hiyo, watu wa Yehova wanaweza kupata usalama wapi katika ulimwengu huu unaowachukia?—Yoh. 15:17-19.

YEHOVA ANATOKEZA “BONDE KUBWA SANA”

8. (a) Milima inaweza kufananisha nini katika Biblia? (b) ‘Mulima wa mizeituni’ unafananisha nini?

8 Kwa kuwa “jiji” la Yerusalemu ni la mufano, ‘mulima wa mizeituni, ulio mbele ya Yerusalemu’ ni wa mufano pia. Mulima huo unafananisha nini? Namna gani mulima huo “utapasuliwa katikati” na kuwa milima miwili? Sababu gani Yehova anaita milima hiyo “milima yangu”? (Soma Zekaria 14:3-5.) Katika Biblia, milima inaweza kufananisha falme, ao serikali. Biblia inazungumuzia pia namna watu watakavyobarikiwa na kulindwa katika mulima wa Mungu. (Zab. 72:3; Isa. 25:6, 7) Kwa hiyo, mulima wa mizeituni ambao Mungu anasimama juu yake, upande wa mashariki wa Yerusalemu unafananisha utawala wa Yehova juu ya ulimwengu wote mzima.

9. ‘Mulima wa Mizeituni’ unapasuliwa katika maana gani?

9 Kupasuliwa kwa mulima wa mizeituni kunamaanisha nini? Mulima, ulio upande wa mashariki wa Yerusalemu, unapasuka katika maana ya kwamba Yehova anasimamisha ufalme utakaotetea utawala wake juu ya ulimwengu wote. Yesu Kristo ndiye mufalme wa ufalme huo. Hiyo ndio sababu Yehova anaita milima hiyo miwili “milima yangu.” (Zek. 14:4) Milima hiyo miwili ni yake.

10. “Bonde kubwa sana” katikati ya milima miwili linafananisha nini?

10 Mulima huo unapopasuka, nusu ya mulima upande wa mashariki na nusu ingine upande wa kusini, miguu ya Yehova inaendelea kusimama juu ya milima hiyo miwili. Kisha kunakuwa “bonde kubwa” chini ya miguu ya Yehova. Bonde hilo la mufano linafananisha ulinzi na usalama ambao Yehova anatolea watumishi wake kupitia utawala wake juu ya ulimwengu wote muzima na kupitia ufalme wa Mwana wake. Yehova hataruhusu hata kidogo ibada safi imalizike. Mulima huo wa mizeituni ulipasuka wakati gani? Mulima huo ulipasuka wakati Ufalme wa Masiya ulianza kutawala mbinguni mwishoni mwa Nyakati za Mataifa katika mwaka wa 1914. Watu walianza kukimbilia katika bonde hilo la mufano wakati gani?

WATU WANAANZA KUKIMBILIA KATIKA BONDE

11, 12. (a) Watu walianza kukimbilia katika bonde la mufano wakati gani? (b) Ni nini inayoonyesha kama mukono wenye nguvu wa Yehova unaendelea kuwategemeza watu wake?

11 Yesu aliwaonya wafuasi wake hivi: ‘Mutachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.’ (Mt. 24:9) Katika siku za mwisho za ulimwengu huu, kuanzia mwaka wa 1914, chuki hiyo imeongezeka sana. Mabaki ya watiwa​-mafuta walishambuliwa na maadui wao wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, hata hivyo wote hawakuuawa. Walikombolewa kutoka katika utumwa wa Babiloni Mukubwa, ni kusema, dini zote za uongo, katika mwaka wa 1919. (Ufu. 11:11, 12)a Watu walianza kukimbilia katika bonde la mulima wa Yehova kuanzia wakati huo.

12 Kuanzia mwaka wa 1919 waabudu wa kweli wa Yehova duniani pote wanaendelea kulindwa katika bonde la Yehova. Kwa miaka mingi katika sehemu mbalimbali za dunia, maadui wetu wamekataza vichapo vyetu na kazi yetu ya kuhubiri. Hali hiyo inaendelea mupaka sasa katika inchi fulani. Lakini, hata mataifa yafanye nini, hayaweze hata kidogo kufuta ibada ya kweli duniani. Mukono wenye nguvu wa Yehova utaendelea kuwategemeza watu wake.​—Kum. 11:2.

13. Tunapaswa kufanya nini ili kubaki katika bonde la ulinzi la Yehova, na sababu gani ni jambo la maana kufanya hivyo leo?

13 Ikiwa tunaendelea kuwa waaminifu kwa Yehova na kubaki imara katika kweli, Yehova na Mwana wake Yesu Kristo, watatusaidia, na Mungu hataruhusu mutu yeyote ao kitu chochote ‘kitunyakue katika mukono Wake.’ (Yoh. 10:28, 29) Yehova iko tayari kututolea musaada wowote tunaohitaji ili tuweze kutii mamlaka yake na kuendelea kubaki waaminifu kwa Ufalme wa Masiya. Kwa kuwa tutahitaji zaidi kulindwa na Yehova wakati wa ziki kubwa inayokaribia sana, ni lazima tubaki katika bonde la ulinzi kuanzia leo.

‘SIKU YA VITA’ INAANZA

14, 15. Katika “siku ya vita [ya Mungu],” watu watakaokuwa inje ya bonde la ulinzi la Yehova watakuwa katika hali gani?

14 Kwa kuwa mwisho wa ulimwengu huu unakaribia sana, Shetani ataendelea kushambulia sana watumishi wa Yehova. Ndipo “siku yake [Mungu] ya vita” juu ya maadui wake itafika. Katika shambulio hilo la Shetani juu ya watu wa Mungu ambalo Zekaria anazungumuzia, Mutawala Mukubwa wa Ulimwengu Wote, atawapigania watu wake kuliko ‘siku nyingine ya pigano’ ambayo amekwisha kuwapigania.​—Zek. 14:3.

15 Katika siku ya vita ya Mungu, watu watakaokuwa inje ya “bonde kubwa” la ulinzi watakuwa katika hali gani? ‘Nuru yenye samani’ ya Mungu haitawaangazia. Katika siku hiyo ya pigano inayokuja, ‘farasi, nyumbu, ngamia, na punda-dume, na kila aina ya munyama wa kufugwa vitagandamana.’ Hilo linamaanisha kwamba silaha za vita za mataifa hazitatumika tena, zitakuwa kama vitu vinavyogandamana kwa sababu ya baridi. Yehova atatumia pia magonjwa makali ao “tauni.” Hatujue kama tauni hiyo itakuwa ya mufano ao hapana, lakini tunajua kwamba siku hiyo itanyamanzisha maadui wa Mungu. Siku hiyo, ‘macho ya mutu na ulimi wake vitaoza.’ Hilo linamaanisha kwamba maadui wa Mungu watashambulia wakiwa kama vipofu na vinywa vyao vitanyamazishwa kabisa. (Zek. 14:6, 7, 12, 15.) Uharibifu huo utakuwa kila mahali duniani. Majeshi ya Shetani yatakuwa mengi. (Ufu. 19:19-21) Kwa hiyo, ‘wale watakaouawa na Yehova siku hiyo hakika watakuwa kutoka mwisho mumoja wa dunia mupaka mwisho wa pili wa dunia.’​—Yer. 25:32, 33.

16. Kwa kuwa, siku ya vita ya Mungu inakaribia, ni maulizo gani ambayo tunapaswa kujiuliza, na itakuwa jambo la maana kufanya nini?

16 Kwa kawaida, vita inatokeza magumu, hata kwa wale wanaopata ushindi. Chakula kinaweza kukosekana. Mali zinaweza kupotea. Na hali ya maisha inaweza kuwa mbaya zaidi. Watu wanapoteza uhuru waliokuwa nao hapo mbele. Ikiwa tunajikuta katika hali hiyo, tutafanya nini? Je, tutaogopa sana? Je, tutaacha kumutumikia Yehova kwa sababu ya magumu hayo? Je, tutakata tamaa na kulemewa na huzuni? Wakati wa ziki kubwa, itakuwa jambo la maana kwetu kubaki katika bonde la ulinzi la Yehova kwa kuendelea kuwa waaminifu kwa Yehova na kutumaini nguvu zake zenye kuokoa.​—Soma Habakuki 3:17, 18.

‘MAJI YA UZIMA YATATOKA’

17, 18. (a) ‘Maji ya uzima’ yanamaanisha nini? (b) “Bahari ya mashariki” na “bahari ya mangaribi” zinafananisha nini? (c) Unapongojea wakati ujao, umeazimia kufanya nini?

17 Kisha Har-magedoni, ‘maji ya uzima’ yataendelea kububujika kutoka katika kiti cha Ufalme wa Masiya. Hayo ‘maji ya uzima’ yanafananisha mipango ya Yehova ya kuwasaidia wanadamu waishi milele. “Bahari ya mashariki” ndio Bahari ya Chumvi, na ‘bahari ya mangaribi’ ndio Bahari ya Mediterania. Bahari hizo mbili zinafananisha watu. Bahari ya Chumvi inafananisha wale wote walio katika kaburi. Kwa kuwa Bahari ya Mediterania inajaa viumbe vilivyo na uzima, bahari hiyo inafananisha kabisa ‘mukutano mukubwa’ wa watu watakaookoka Har-magedoni. (Soma Zekaria 14:8, 9; Ufu  7:9-15) Kwa hiyo, watu walio katika vikundi hivyo viwili watafaidika kwa kukombolewa kutoka katika zambi waliyoriti kwa Adamu kadiri wanavyoendelea kumaliza kiu chao kwa kunywa maji ya uzima ya mufano, yanayotoka katika ‘muto wa maji ya uzima.’​—Ufu. 22:1, 2.

[Picha katika ukurasa wa 21]

Azimia kubaki katika bonde la ulinzi la Yehova

18 Yehova atakapoharibu ulimwengu huu muovu, atatulinda na kutuingiza katika ulimwengu mupya wa haki. Hata ikiwa tunachukiwa na watu wa mataifa yote, acheni tuazimie kabisa kubaki raia waaminifu wa Ufalme wa Mungu, na tuendelee kubaki katika bonde la ulinzi la Yehova.

a Soma kitabu Ufunuo​—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! ukurasa 169-170.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine