Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 15/4 uku. 22-26
  • ‘Tuhakikishe Mambo Yaliyo ya Maana Zaidi’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Tuhakikishe Mambo Yaliyo ya Maana Zaidi’
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • SEHEMU ISIYOONEKANA YA TENGENEZO LA YEHOVA INASONGA MBELE
  • SEHEMU YENYE KUONEKANA YA TENGENEZO LA YEHOVA HAPA DUNIANI
  • TUKAZIE UANGALIFU “MAMBO YALIYO YA MAANA ZAIDI”
  • FUATA MUFANO WA TENGENEZO LA YEHOVA
  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • ‘Tusichoke Kabisa’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Yehova Iko Anaongoza Tengenezo Lake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Unaendelea Kusonga Mbele Pamoja na Tengenezo la Yehova?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 15/4 uku. 22-26
[Picha katika ukurasa wa 22]

‘Tuhakikishe Mambo Yaliyo ya Maana Zaidi’

‘Tuhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi.’—FLP. 1:10.

JIBU MAULIZO HAYA

  • Namna gani maono ambayo nabii Isaya, Ezekieli, na Danieli walipewa yanatusaidia tumutumaini Yehova zaidi?

  • Tunajifunza nini tunapofikiria kazi ambayo sehemu inayoonekana ya tengenezo la Yehova inakazia uangalifu zaidi?

  • Habari hii inatutia moyo tuazimie kufanya nini?

1, 2. Ni unabii gani kuhusu siku za mwisho ambao labda uliwashangaza wanafunzi wa Yesu, na sababu gani?

MWISHOWE Petro, Yakobo, Yohana na Andrea walikuwa pekee yao pamoja na Bwana wao. Akili zao zilihangaishwa kabisa na mambo ambayo Yesu alisema hapo mbele juu ya uharibifu wa hekalu. (Mk. 13:1-4) Kwa hiyo, walimuuliza hivi: ‘Tuambie, Mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mufumo wa mambo?’ (Mt. 24:1-3) Yesu alianza kuwaambia mambo, ao hali ambazo zingebadili kabisa maisha ya watu na ambazo zingekuwa alama za siku za mwisho za ulimwengu muovu wa Shetani. Kuna jambo moja la pekee ambalo labda liliwashangaza wanafunzi wa Yesu. Kisha kuzungumuzia mambo yenye kuhuzunisha kama vile vita, njaa, na kuongezeka kwa uasi wa sheria, Yesu alitabiri kwamba kuna jambo nzuri ambalo lingetokea katika siku za mwisho. Alisema hivi: “Na hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.”​—Mt. 24:7-14.

2 Wanafunzi wa Yesu walifurahia kuhubiri habari njema ya Ufalme pamoja na Kristo. (Lu. 8:1; 9:1, 2) Labda walikumbuka maneno haya ya Yesu: “Kwa kweli, mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Lu. 10:2) Lakini namna gani wangehubiri “katika dunia yote inayokaliwa” na kutoa “ushahidi kwa mataifa yote”? Wafanyakazi hao wangetoka wapi? Ikiwa wangekuwa na uwezo wa kuona jinsi mambo yanavyotendeka leo ni wazi kwamba wangeshangaa sana kuona namna maneno ya andiko la Mathayo 24:14 yanavyotimia leo.

3. Namna gani andiko la Luka 21:34 linatimia leo, na tunapaswa kujiuliza nini?

3 Unabii wa Yesu unatimia sasa. Mamilioni ya watu wameungana ili kueneza habari njema ya Ufalme katika dunia yote. (Isa. 60:22) Lakini, Yesu alionyesha kwamba ingekuwa vigumu kwa wengine kuendelea kutia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza katika siku hizi za mwisho. Wangekengeushwa na ‘kulemewa.’ (Soma Luka 21:34.) Maneno hayo yanatimia pia leo. Wakristo fulani wameanza kukengeushwa akili. Hilo linaweza kuonekana katika maamuzi wanayochukua kuhusu kazi, masomo ya juu, na kutafuta vitu vya kimwili, na vilevile wakati wanaotumia katika mambo ya michezo na kujifurahisha. Wengine wameanza kuchoka kwa sababu ya shida na mahangaiko ya maisha ya kila siku. Tunaweza kujiuliza: ‘Hali yangu iko namna gani? Je, maamuzi yangu yanaonyesha kwamba ninatia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza?’

4. (a) Mutume Paulo alisali kuhusu jambo gani kwa ajili ya Wakristo wa muji wa Filipi, na sababu gani? (b) Tutajifunza nini katika habari hii na ile inayofuata, na sababu gani?

4 Wakristo wa zamani walipaswa kujikaza ili kuendelea kutia kazi ya Mungu pa nafasi ya kwanza. Mutume Paulo aliona kwamba ni jambo la lazima sana kusali kwa ajili ya wale waliokuwa katika muji wa Filipi ili ‘wahakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi.’ (Soma Wafilipi 1:9-11.) Wakati huo, ndugu wengi kama vile mutume Paulo walikuwa ‘wanaonyesha uhodari hata zaidi kwa kulisema neno la Mungu bila woga.’ (Flp. 1:12-14) Vivyo hivyo, Wakristo wengi sana leo wanahubiri Neno la Mungu bila woga. Hata hivyo, yale yanayotimizwa sasa katika tengenezo la Yehova yanaweza kutusaidia tufikirie hata zaidi kutia pa nafasi ya kwanza kazi ya maana kuliko zote, ni kusema, kazi ya kuhubiri, sivyo? Ndiyo kabisa! Acheni tuzungumuzie katika habari hii mipango ambayo Yehova amechukua ili kutimiza maneno ya andiko la Mathayo 24:14. Ni jambo gani ambalo tengenezo la Yehova linatia pa nafasi ya kwanza ao kukazia uangalifu zaidi, na namna gani kujua jambo hilo kutatuchochea sisi na familia zetu? Katika habari inayofuata, tutajifunza jambo ambalo linaweza kutusaidia kuvumilia na kuendelea kutembea bega kwa bega na tengenezo la Yehova.

SEHEMU ISIYOONEKANA YA TENGENEZO LA YEHOVA INASONGA MBELE

5, 6. (a) Sababu gani Yehova aliwaonyesha manabii wake maono kuhusu sehemu isiyoonekana ya tengenezo lake? (b) Nabii Ezekieli aliona nini katika maono?

5 Kuna mambo mengi ambayo Yehova aliamua kutokuandikisha katika Neno lake Biblia. Kwa mufano, hakuandikisha habari kuhusu namna ubongo unavyofanya kazi ao namna ulimwengu unavyofanya kazi, hata ikiwa kujifunza habari hizo kungevutia sana! Badala yake, Yehova aliandikisha tu habari tunazohitaji ili tuelewe makusudi yake na ili tuishi kulingana na makusudi hayo. (2 Tim. 3:16, 17) Hata hivyo, ni jambo la kufurahisha kwamba Biblia inatuelezea kwa ufupi kuhusu sehemu isiyoonekana ya tengenezo la Yehova. Tunafurahia sana kusoma maelezo kuhusu sehemu ya mbinguni ya tengenezo la Yehova katika kitabu cha Isaya, Ezekieli, na Danieli na katika Ufunuo wa Yohana. (Isa. 6:1-4; Eze. 1:4-14, 22-24; Dan. 7:9-14; Ufu. 4:1-11) Ni kama vile Yehova anaondoa pazia ao mawingu ili tuone mambo yaliyo mbinguni. Sababu gani alitutolea habari hizo?

[Picha katika ukurasa wa 24]

6 Yehova alifanya hivyo ili tusisahau hata kidogo kama sisi ni sehemu ya tengenezo lake. Kuna mambo mengi yanayotendeka ili kutimiza makusudi ya Mungu ambayo sisi hatuone. Kwa mufano, Ezekieli aliona sehemu isiyoonekana ya tengenezo la Yehova inayofananishwa na gari kubwa la mbinguni. Gari hilo linaweza kutembea mbio sana na kugeukia haraka upande wowote. (Eze. 1:15-21) Magurudumu yake yalikuwa tayari kugeukia upande wowote, kwa hiyo gari hilo lingeenda mahali popote na lingeenda mbali bila kizuizi. Katika maono, Ezekieli aliweza pia kuona Mutembezaji wa gari hilo. Alisema hivi: ‘Nami nikaona kitu kama mungao wa muchanganyiko wa zahabu na feza, kinachoonekana kama moto kuzunguka pande zote. Kulikuwa ni kuonekana kwa mufano wa utukufu wa Yehova.’ (Eze. 1:25-28) Bila shaka, Ezekieli alishangaa sana kuona gari hilo! Alimuona Yehova akiongoza tengenezo lake lote kupitia roho yake takatifu. Gari hilo linafananisha kwa njia ya ajabu sehemu isiyoonekana ya tengenezo la Yehova huko mbinguni na namna linavyosonga mbele!

7. Namna gani maono ambayo Danieli alipewa yanatusaidia tumutumaini Yehova zaidi?

7 Nabii Danieli pia aliona mambo yanayotusaidia tumutumaini Yehova zaidi. Alipewa nafasi ya kumuona Yehova aliyefananishwa na ‘Muzee wa Siku’ akiwa ameketi juu ya kiti cha ufalme kilichokuwa na miale ya moto. Kiti hicho kilikuwa na magurudumu ao mipeto. (Dan. 7:9) Yehova alipenda kumuonyesha nabii Danieli namna tengenezo Lake linavyosonga mbele ili kutimiza kusudi Lake. Danieli aliona pia ‘mutu fulani kama mwana wa binadamu,’ ni kusema, Yesu, akipewa mamlaka juu ya sehemu yenye kuonekana ya tengenezo la Yehova hapa duniani. Utawala wa Yesu Kristo si wa muda muchache tu. Badala yake, ni ‘utawala unaodumu kwa wakati usio na kipimo ambao hautapitilia mbali, na ufalme wake ni ufalme ambao hautaharibiwa.’ (Dan. 7:13, 14) Maneno hayo yanatuchochea tumutumaini Yehova zaidi na kutambua mambo anayotimiza. Yehova alimutolea “utawala na heshima na ufalme” Mwana wake aliyeshinda majaribu, ni kusema, Yesu Kristo. Yehova anamutumainia Mwana wake. Kwa hiyo, sisi pia tunapaswa kutumainia utawala wake.

8. Maono ambayo Ezekieli na Isaya waliona yaliwachochea kufanya nini, na yanaweza kutuchochea kufanya nini?

8 Habari hizi kuhusu sehemu isiyoonekana ya tengenezo la Yehova zinapaswa kutuchochea namna gani? Kama Ezekieli, tunakuwa na unyenyekevu na woga tunapoona mambo ambayo Yehova anatimiza leo. (Eze. 1:28) Kutafakari kuhusu tengenezo la Yehova kunaweza kutuchochea tutende, kama vile nabii Isaya alivyochochewa kutenda. Mutu alipohitajiwa ili aende kuwaelezea wengine matendo ya Yehova, Isaya aliitikia bila kusita. (Soma Isaya 6:5, 8.) Isaya alikuwa hakika kwamba kwa musaada wa Mungu angeshinda vizuizi vyovyote. Vivyo hivyo, habari hizo kuhusu sehemu isiyoonekana ya tengenezo la Yehova zinapaswa kutuchochea tutende na kutufanya tumuogope Yehova. Ni jambo lenye kutia moyo kuona namna tengenezo la Mungu linavyosonga mbele na namna linavyoendelea kukaza uangalifu sana juu ya kutimizwa kwa makusudi ya Yehova!

SEHEMU YENYE KUONEKANA YA TENGENEZO LA YEHOVA HAPA DUNIANI

9, 10. Sababu gani sehemu yenye kuonekana ya tengenezo la Yehova ilihitajiwa?

9 Kupitia Mwana wake, Yehova amesimamisha hapa duniani sehemu yenye kuonekana ya tengenezo lake inayofanya kazi pamoja na sehemu isiyoonekana ya tengenezo lake. Sababu gani mupango huo unahitajiwa ili kutimiza maneno ya Mathayo 24:14? Acha tuzungumuzie sababu tatu.

10 Kwanza, Yesu alisema kwamba wanafunzi wake wangehubiri ‘mupaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.’ (Mdo. 1:8) Pili, mipango ilipaswa kufanywa ili kulisha kiroho na kuwatunza wale wanaofanya kazi ya kuhubiri. (Yoh. 21:15-17) Tatu, mipango ilipaswa kufanywa ili wahubiri hao wa habari njema wakusanyike pamoja ili kumuabudu Yehova na kufundishwa namna ya kuhubiri. (Ebr. 10:24, 25) Ili kutimiza mambo hayo, sehemu yenye kuonekana ya tengenezo la Yehova ilihitajiwa. Ili wanafunzi wa Yesu watimize kazi hiyo vizuri, kazi ilipaswa kupangwa.

11. Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunategemeza mipango inayochukuliwa na tengenezo la Yehova?

11 Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunategemeza mipango inayochukuliwa na tengenezo la Yehova? Njia moja ya lazima ni kutumainia kila siku wale ambao Yehova na Yesu wanatumia ili kutupa maagizo kuhusu kazi ya kuhubiri. Kuna shuguli ao mambo mengi katika ulimwengu leo yanayoweza kuwavutia wale wanaotuongoza. Hata hivyo, ni jambo gani ambalo sehemu inayoonekana ya tengenezo la Yehova inaendelea kutia pa nafasi ya kwanza ao kukazia uangalifu zaidi?

TUKAZIE UANGALIFU “MAMBO YALIYO YA MAANA ZAIDI”

12, 13. Namna gani wazee Wakristo wanatimiza daraka lao, na sababu gani jambo hilo linakutia moyo?

12 Duniani kote wazee wenye kukomaa kiroho wametiwa ili kusimamia na kufanya kazi ya kuhubiri Ufalme isonge mbele katika inchi wanamoishi. Ndugu hao wanapochukua maamuzi, wanachunguza Neno la Mungu, wakilifanya liwe ‘taa ya miguu yao na nuru kwa barabara yao, na wanasali kwa bidii ili Yehova awaongoze.​—Zab. 119:105; Mt. 7:7, 8.

13 Kama ilivyokuwa kwa wale waliosimamia kazi ya kuhubiri wakati wa mitume, wazee Wakristo wanaosimamia kazi ya kuhubiri leo wanajitoa sana “kwa huduma ya neno.” (Mdo. 6:4) Wanafurahia sana maendeleo yanayofanywa katika kazi ya kuhubiri mahali wanapoishi na ulimwenguni pote. (Mdo. 21:19, 20) Hawatuwekee sheria nyingi. Badala yake, wanafuata uongozi wa Neno la Mungu na wa roho takatifu yake wanapochukua mipango inayoweza kusaidia kazi ya kuhubiri isonge mbele. (Soma Matendo 15:28.) Kwa kufanya hivyo, ndugu hao wanawekea wote katika kutaniko mufano muzuri.​—Efe. 4:11, 12.

14, 15. (a) Ni mipango gani inayofanywa ili kutegemeza kazi ya kuhubiri duniani pote? (b) Unajisikia namna gani unapotegemeza kazi ya kuhubiri Ufalme?

14 Kutayarisha habari zinazopatikana katika vichapo vyetu, habari za kujifunza kwenye mikutano na mikusanyiko yetu ni kazi nyingi inayofanywa bila kuonwa na watu wengi. Maelfu ya wafanyakazi wenye kujitolea wanatumika kwa bidii ili kutafsiri chakula cha kiroho katika luga 600 hivi ili watu wengi zaidi wajifunze ‘mambo makubwa ya Mungu’ katika luga zao. (Mdo. 2:7-11) Ndugu na dada vijana wanatumia mashini za kuchapisha zinazotembea mbio sana ili kuchapa vichapo vyetu na mashini za kuunganisha vichapo hivyo. Kisha vichapo hivyo vinatumwa katika makutaniko hata yale yanayopatikana kwenye sehemu za mbali sana za dunia.

15 Mipango mingi imefanywa ili tuweze kukazia uangalifu wetu kwenye kazi ya kuhubiri habari njema katika kutaniko letu. Kwa mufano, wengi wanajitolea ili kusaidia kujenga Majumba ya Ufalme na Majumba ya Mikusanyiko, kusaidia wale waliopigwa na misiba ya asili ao wale wanaohitaji kutunzwa haraka, kutayarisha mikusanyiko, na kufundisha masomo mbalimbali yanayoongozwa na tengenezo la Mungu, na mambo mengine yanayofanywa bila sisi kuona. Sababu gani mambo hayo yote yanafanywa? Mambo hayo yanafanywa ili kazi ya kuhubiri habari njema ifanywe bila magumu, ili hali ya kiroho ya wahubiri iwe nzuri na ili kuendeleza ibada ya kweli. Kwa hiyo, je, tunaweza kusema kwamba sehemu yenye kuonekana ya tengenezo la Yehova hapa duniani imeendelea kutia mambo ya maana pa nafasi ya kwanza? Bila shaka, ndiyo!

FUATA MUFANO WA TENGENEZO LA YEHOVA

16. Unaweza kuamua kujifunza nini wakati wa funzo lako la pekee ao wakati wa ibada ya familia?

16 Je, tunachukua wakati fulani ili kutafakari juu ya kazi mbalimbali ambazo zimetimizwa na tengenezo la Yehova? Wakristo fulani wameamua kutafuta habari zaidi na kutafakari juu ya mambo hayo wakati wa ibada ya familia ao funzo la pekee. Inafurahisha sana kujifunza maono ambayo Isaya, Ezekieli, Danieli na Yohana walipewa. Kitabu Mashahidi wa Yehova—Wapiga-mbiu wa Ufalme wa Mungu na vitabu vingine ao DVD zinazopatikana katika luga yako zinatoa habari nyingi zenye kuvutia zinazotusaidia kuelewa tengenezo la Yehova.

17, 18. (a) Habari hii imekusaidia namna gani? (b) Tutazungumuzia nini katika habari inayofuata?

17 Ni jambo la maana kwetu kutafakari ao kufikiri sana juu ya mambo ambayo Yehova ametimiza kupitia tengenezo lake. Tunapotembea na tengenezo hilo nzuri, acheni tuazimie kuendelea kutia mambo ya maana pa nafasi ya kwanza. Kufanya hivyo kutatusaidia tuazimie kama Paulo, aliyeandika hivi: “Kwa kuwa sisi tuna huduma hii kulingana na rehema tuliyoonyeshwa, hatufi moyo.” (2 Kor. 4:1) Pia aliwatia moyo wafanyakazi wenzake hivi: ‘Tusife moyo katika kufanya yaliyo mema, kwa maana katika majira yanayofaa tutavuna ikiwa hatuchoke kabisa.’​—Gal. 6:9.

18 Je, kuna mabadiliko ambayo tunapaswa kufanya sisi ao familia yetu ili tuhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi katika maisha yetu ya kila siku? Je, tunaweza kurahisisha maisha yetu ao kupunguza mambo yanayochukua wakati wetu mwingi ili tufanye mengi zaidi katika kazi ya kuhubiri? Katika habari inayofuata, tutazungumuzia mambo matano yatakayotusaidia kutembea bega kwa bega na tengenezo la Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine