Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/8 uku. 16
  • Maulizo Juu Ya Habari Za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu Ya Habari Za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Kumukaribia Mungu Karibu Katika Sala
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Unaweza Kufanya Nini ili Umukaribie Mungu?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/8 uku. 16
[Picha katika ukurasa wa 16]

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Mungu anasikiliza sala zote?

Mungu anasikiliza watu wa mataifa yote. (Zaburi 145:18, 19) Neno lake, Biblia, linatutia moyo tuzungumuze naye juu ya jambo lolote linalotuhangaisha. (Wafilipi 4:6, 7) Hata hivyo, sala fulani hazimupendeze Mungu. Kwa mufano, sala za kurudilia-rudilia zilizowekwa katika akili hazimupendeze.​—Soma Mathayo 6:7.

Pia, Yehova anachukia sala za watu ambao wanavunja sheria zake kimakusudi. (Methali 28:9) Kwa mufano, nyakati za zamani, Mungu alikataa kuwasikiliza Waisraeli waliokuwa na hatia ya uuaji. Ni wazi kwamba tunapaswa kutimiza mambo fulani ili Mungu asikilize sala zetu.​—Soma Isaya 1:15.

Tunapaswa kufanya nini ili Mungu asikilize sala zetu?

Hatuwezi kumukaribia Mungu katika sala bila imani. (Yakobo 1:5, 6) Tunapaswa kuwa na uhakika kwamba Mungu yuko na kwamba anatuhangaikia. Tunaweza kufanya imani yetu iwe yenye nguvu kwa kujifunza Biblia kwa sababu imani ya kweli inategemea mambo ya kweli na usadikisho unaopatikana katika Neno la Mungu.​—Soma Waebrania 11:1, 6.

Tunapaswa kusali kwa moyo wote na kwa unyenyekevu. Hata Yesu, Mwana wa Mungu, alikuwa munyenyekevu aliposali. (Luka 22:41, 42) Kwa hiyo, kuliko kumuambia Mungu jambo la kufanya, tunapaswa kujikaza kuelewa mambo ambayo anatuomba tufanye kwa kusoma Biblia. Kwa kufanya hivyo tunaweza kusali kupatana na mapenzi ya Mungu.​—Soma 1 Yohana 5:14.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 17 ya kitabu hiki: Biblia Inafundisha Kabisa Nini?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kuchukua kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine