Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/6 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Wazazi, Musaidie Watoto Wenu Wamupende Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Unaweza Kufanya Nini Juu Familia Yako Ikuwe na Furaha?​—Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Namna ya Kumufundisha Mutoto Wako
    Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/6 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Mutu anaweza kufanya nini ili akuwe muzazi muzuri?

Baba na mutoto wake wanaangalia kerengende

Unafundisha mutoto wako kupenda Mungu?

Familia yenye kuwa na wazazi wenye kupendana na kuheshimiana ni mahali pazuri sana pa kukomalishia watoto. (Wakolosai 3:14, 19) Wazazi wazuri wanapenda watoto wao na wanawapongeza, kama vile Yehova alipongeza Mwana wake.—Soma Mathayo 3:17.

Baba yetu wa mbinguni anasikiliza watumishi wake, na anahangaikia namna wanajisikia moyoni. Ni muzuri wazazi wafuate mufano wake na wasikilize watoto wao. (Yakobo 1:19) Hawapaswe kuzarau mawazo ya watoto wao, hata wakati wanasema mubaya.—Soma Hesabu 11:11, 15.

Unaweza kufanya nini ili watoto wako wakuwe wenye kutumainika?

Wewe muzazi, uko na mamlaka ya kuwekea watoto wako sheria. (Waefeso 6:1) Ufuate mufano wa Mungu. Anapenda watoto wake kwa sababu anawaonyesha wazi sheria zake na matokeo yenye wanaweza kupata ikiwa hawatii sheria hizo. (Mwanzo 3:3) Halazimishe watu watii sheria zake, lakini anawaonyesha ni faida gani watapata ikiwa wanafanya mambo ya muzuri.—Soma Isaya 48:18, 19.

Ufanye mupango wa kusaidia watoto wako wamupende Mungu. Hilo litawasaidia watende kwa hekima hata kama hauko pamoja nao. Kama vile Yehova anafundisha kupitia mufano wake, wewe pia ufundishe watoto wako kupitia mufano wako.—Soma Kumbukumbu la Torati 6:5-7; Waefeso 4:32; 5:1.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 14 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza pia kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine