Wenye Kustahili Na Kuvalia Vifaa Ili Kufundisha Wengine
1 Yehova alimweka rasmi Musa ili kumwakilisha, lakini Musa hakujiona kuwa mwenye uwezo wa kutangaza maneno ya Mungu kwa Farao. (Kut. 4:10; 6:12) Kwa kumwambia Mungu kwamba alikuwa asiyejua kusema, Yeremia alionyesha kwamba hakuwa na uwezo wa kuwa nabii wa Yehova. (Yer. 1:6) Hakika, mwanzoni, walikuwa wenye kukosa uhakika ndani yao wenyewe, lakini manabii hao wawili walijionyesha kuwa mashahidi hodari kwa ajili ya Yehova. Mungu aliwatolea mazoezi kwa matokeo.
2 Leo, Yehova anatutolea yote yaliyo ya lazima ili kuwa wenye uhakika katika huduma yetu. (2 Kor. 3:4, 5; 2 Tim. 3:17) Kwa mfano wa fundi wa motokaa mwenye kustahili na aliye na vifaa vyote vya kazi, tuna vifaa vifaavyo ili kuitimiza kwa ustadi. Mnamo Februari, tunatolea kitabu chochote cha kurasa 192 kilichotangazwa kabla ya 1984 ambacho kutaniko linacho katika stoki. Hata ikiwa vifaa hivyo vya kiroho si vipya tena, vichwa vya habari za kibiblia ambazo vinazungumzia sikuzote ni vyenye kuvuma kwa sasa na vitawasaidia watu kuujua ukweli. Maagizo yafuatayo yanaweza kuambatanishwa kwa haidhuru kitabu gani ambacho tutatolea.
3 Tunaweza kutokeza kupendezwa kwa ajili ya Neno la Mungu kwa kusema juu ya elimu. Tungeweza kuanzisha mazungumzo kwa kusema:
◼ “Leo, watu wanaweka mkazo juu ya elimu ya hali ya juu. Kulingana nawe, ni aina gani ya elimu inafaa kutafuta ili kupata furaha na kufanikiwa? [Tusikilize jibu.] Wale wanaopata ujuzi wa Mungu wanaweza kufaidika nao milele. [Tusome Mezali 9:10, 11.] Kitabu hiki [tuonyeshe kichwa cha habari cha kitabu ambacho tunatolea] kina msingi juu ya Biblia. Kinavutia uangalifu juu ya chanzo pekee cha ujuzi uongozao kwenye uhai udumuo milele.” Tuonyesha mfano kamili unaotoka katika kitabu hicho. Ikiwa mtu anaonyesha kupendezwa kweli kweli, tumwaachie kitabu kwa bei ya sasa na tuagane naye kwa ajili ya ziara ya kurudia.
4 Kwa kurudi kumuona mtu tuliyezungumza naye umuhimu wa elimu ya kibiblia, tunaweza kusema:
◼ “Mara ya mwisho, tuliona kwamba Biblia ni chanzo cha elimu ambayo inaweza kututolea wakati ujao wa milele. Bila shaka, inaomba kufanya bidii ili kujifunza katika Maandiko yale tunayohitaji kujua. [Tusome Mezali 2:1-5.] Watu wengi wanaona kwamba maandiko fulani ya Biblia ni magumu kueleweka. Ningependa kukuonyesha kwa kifupi ufundi ambao tunatumia mara nyingi ili kuwasaidia watu kujua mengi zaidi juu ya mafundisho ya msingi ya Biblia.” Tufungue kitabu tulichoacha kwenye ukurasa unaofaa na tufanya onyesho ndogo la funzo la Biblia. Ikiwa msikilizaji wetu anatamani kujifunza kwa ukawaida, tumfasirie kwamba tutarudi tena kumuona pamoja na kitabu chetu cha funzo Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.
5 Watu wengi ni wenye wasiwasi kwa ajili ya mamilioni ya watoto wanaoteseka ulimwenguni. Labda tunaweza kumsaidia msikilizaji wetu kuelewa jinsi Mungu anavyoona hali yao ya mateso kwa kusema:
◼ “Bila shaka uliona kwenye televisheni picha za watoto ulimwenguni ambao ni wenye njaa, wagonjwa na walioachwa. Kwa nini mashirika yanayohusika hayafikii kutengeneza hali? [Tusikilize jibu.] Mungu anawatakia wanadamu yaliyo mema. Tazama yale anayoahidi katika Biblia kwa ajili ya watoto na watu wazima. [Tusome Ufunuo 21:4.] Kitabu hiki [tuonyeshe kichwa cha habari] kinatoa maelezo mengi juu ya ulimwengu unaosimamishwa na Mungu ambamo mateso yatatoeka.” Ikiwezekana, tuonyeshe picha ya Paradiso na tuseme juu yayo. Tutolee kitabu na tuchukue mipango ili kurudi tena.
6 Ikiwa, mara ya kwanza, tulizungumza juu ya mateso ya watoto, tunaweza kuendeleza mazungumzo namna ifuatayo wakati wa ziara ijayo ya kurudia:
◼ “Mara ya mwisho nilipokuja, ulionyesha wasiwasi yako kuhusu hali yenye kuhuzunisha ya watoto wanaoishi katika familia zenye kugawanyika, au wanaopatwa na njaa, magonjwa na jeuri. Ni jambo lenye kuburudisha kuona kwamba Biblia inasema juu ya ulimwengu ambamo magonjwa, maumivu na kifo havitawatesa tena wala watoto wala watu wazima. Maisha bora duniani yanaonyeshwa katika unabii wa kitabu cha Isaya.” Tusome Isaya 65:20-25 na tuieleze. Tuzungumzie uwezekano wa kujifunza Biblia kwa msaada wa kitabu Ujuzi.
7 Kwa kuwa sala ni zoea la watu wote wenye kuamini, tungeweza kuanzisha mazungumzo juu ya habari hiyo kwa kusema:
◼ “Wakati fulani wa maisha yetu, wengi wetu wanapambana na matatizo yanayotusukuma kusali kwa Mungu ili kupokea msaada wake. Lakini wengi wanahisi kwamba sala zao hazikubaliwi. Inaonekana hata kwamba sala zinazotolewa hadharani na wakuu wa kidini kwa ajili ya amani hazisikiwi. Tunasema hilo kwa kuwa vita vinaendelea kutesa wanadamu. Je! kweli Mungu anasikia sala? Ikiwa ndivyo, kwa nini sala nyingi zinaonekana kuwa hazijibiwi? [Tusikilize jibu.] Zaburi 145:18 inafasiria yale tunapaswa kufanya ili sala zetu zisikilizwe. [Tusome andiko hilo.] Kwanza kabisa, sala zinazotolewa kwa Mungu zinapaswa kuwa nyofu na zenye kupatana na ukweli unaopatikana katika Neno lake, Biblia.” Tuonyeshe kitabu ambacho tunatumia na tuvutie uangalifu juu ya kile kinachosema kuhusu thamani ya sala.
8 Ili kuendeleza mazungumzo yaliyohusu sala, tunaweza kujaribu kusema:
◼ “Nilithamini kuzungumza juu ya sala pamoja nawe. Utakubali bila shaka kwamba Yesu alitutolea msaada wenye kutenda kazi kwa kutoa mawazo yake juu ya kile kinachoweza kuombwa katika sala.” Tusome Mathayo 6:9, 10 na tukazie vichwa vya habari vya lazima ambavyo Yesu alikazia katika sala ya Baba Yetu. Tufungue kitabu Ujuzi kwenye sura 16, yenye kichwa “Jinsi Unavyoweza Kumkaribia Mungu,” na tuulize ikiwa tunaweza kuonyesha jinsi ya kujifunza.
9 Tunaposema juu ya kutangazia wengine ujuzi wa Mungu, labda tunauliza: “Na ni nani ambaye ana sifa za ustahili wa kutosha kwa ajili ya mambo haya?” Maandiko hujibu: “Ni sisi.”—2 Kor. 2:16, 17, TUM.