Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/97 uku. 1
  • Tushiriki Katika Kazi Ambayo Haitafanywa Kamwe Tena

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tushiriki Katika Kazi Ambayo Haitafanywa Kamwe Tena
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Hukumu za Mungu—Sikuzote Anaonya Watu Wakati wa Kutosha?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 3/97 uku. 1

Tushiriki Katika Kazi Ambayo Haitafanywa Kamwe Tena

1 Katika vipindi tofauti vya historia, Yehova aliweza kutekeleza hukumu yake juu ya maadui wake. Hata hivyo, katika rehema yake, alitengeneza njia ya wokovu kwa watu wenye mioyo minyofu. (Zab. 103:13) Kuitikia kwao kulikuwa kwa maana kwa ajili ya wakati wao ujao.

2 Kwa mfano, kabla ya gharika, mnamo mwaka wa 2370 kabla ya wakati wetu, Noa alikuwa “mhubiri wa uadilifu.” Wale waliopuuza onyo la kimungu walikufa. (2 Pt. 2:5; Ebr. 11:7, TUM) Kabla ya uharibifu wa Yerusalemu, mnamo mwaka wa 70 wa wakati wetu, Yesu alionyesha waziwazi yale mtu angeweza kufanya ili kuokoka uharibifu ambao ungeangukia mji. Wale wote waliotupilia mbali ujumbe wake wa onyo walipatwa na matokeo mabaya sana. (Lk. 21:​20-24) Katika historia kumekuwako na maonyo kama hayo na hukumu za kimungu.

3 Kazi ya Kuonya Katika Kipindi Chetu: Tangu zamani za kale, Yehova alisema kwamba hasira yake ingewaka dhidi ya mfumo huu mwovu na kwamba wanyenyekevu wangeweza peke yao kuokolewa. (Sef. 2:​2, 3; 3:8) Wakati unaobaki ili kutangaza onyo hilo unapita haraka sana! “Dhiki kubwa” inakaribia sana, na kuwakusanya wanyenyekevu kunasonga mbele. Kwa kweli, “mashamba . . . ni meupe kwa ajili ya kuvunwa.” Kwa hiyo, hakuna kazi yoyote iliyo ya maana na yenye uharaka kama hii.—Mt. 24:14, 21, 22 ; Yn. 4:​35, TUM.

4 Leo, tunapaswa kutangaza onyo hilo kwa majirani zetu, “kama watasikia ao kama watakataa.” Inahusu daraka tunalokabidhiwa na Yehova ambalo hatupaswi kutupilia mbali. (Ezek. 2:​4, 5; 3:17, 18) Kwa kushiriki kikamilifu katika kazi hiyo, tunaonyesha kwa namna yenye kusadikisha upendo wetu wa kina kirefu kwa Yehova, kupendezwa kwa kweli ambako tunaonyesha kwa jirani yetu na imani yetu isiyoyumba-yumba katika Mwokozi wetu, Yesu Kristo.

5 Huu Sasa Ndio Wakati wa Kutenda: Wakati wa nyuma, baada ya hukumu za Yehova kutekelezwa, uovu ulitokea tena, kwani Shetani na mashetani wake walikuwa wangali tu sikuzote wenye kutenda. Hata hivyo, mara hii, itakuwa tofauti. Uvutano wa Shetani utaondoshwa. Hakutakuwa tena kamwe lazima ya kutoa onyo la ulimwenguni pote kuhusu kukaribia sana kwa “dhiki kubwa.” (Ufu. 7:14; Rum. 16:20) Tunalo pendeleo la pekee la kushiriki katika kazi ambayo haitarudiliwa kamwe tena. Huu ndio wakati wa kufanya mengi katika kazi hii.

6 Akiwa na uhakika mwingi, mtume Paulo alisema yafuatayo kuhusu utendaji wake wa mahubiri: “Mimi ni safi kutokana na damu ya watu wote.” (Mdo. 20:​26, TUM) Kwa kuwa hakupuuza kutangaza onyo, hakujihisi kuwa mwenye hatia ya damu yoyote. Kwa nini? Kwa kuwa aliweza kusema kuhusu huduma yake: “Kwa madhumuni haya kwa kweli ninafanya kazi kwa bidii, nikijikakamua.” (Kol. 1:​29, TUM) Tushiriki pia kikamilifu katika kazi hii ambayo haitafanywa tena kamwe, na tutaridhika vilevile kama Paulo!—2 Tim. 2:15.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine