Waangalizi Wanaoongoza—Mwangalizi Wa Utumishi
1 Mwangalizi wa utumishi huhangaikia maendeleo ya kazi ya kueneza evangeli katika eneo la kutaniko. Hivyo, yeye ana fungu la maana katika kutusaidia tutimize daraka letu la kuhubiri habari njema. Mweneza-evangeli huyo mwenye bidii hupanga utendaji wote mbalimbali wenye kuhusu mahubiri. Akiwa mwalimu mwenye ustadi, yeye husaidia wahubiri wawe wenye matokeo zaidi katika huduma.—Efe. 4:11, 12.
2 Mzee huyo ndiye huangalia kazi ya watumishi wa huduma waliogawiwa kazi ya kushugulika na vichapo, magazeti, na maeneo. Yeye anapaswa kuhakikisha kwamba, kila mwezi, tuna kiasi cha kutosha cha vichapo, magazeti, na vifaa vingine kwa ajili ya mahubiri. Mara moja kwa mwaka, yeye huchunguza katika faili ya maeneo mahali ambapo imeshauriwa kutokwenda, naye anaomba ndugu wenye ustadi waende huko.[2]
3 Mwangalizi wa utumishi anapaswa kupanga aina mbalimbali za mahubiri, zaidi sana mahubiri katika maeneo ya biashara, mahubiri ya barabarani na mahubiri kupitia simu. Yeye anahakikisha kwamba amepanga, katika juma na katika siku za likizo, mikutano ya utumishi wa shambani yenye kufaa. Yeye ni mwenye kupendezwa sana na mafunzo ya Biblia. Yeye hujitahidi kutoa msaada wa kiroho kwa wale wanaokuwa wahubiri wasio wa kawaida au wasiotenda katika huduma. Yeye hushughulika na utumishi wa mapainia, na husimamia programu “Mapainia Husaidia Wengine.”
4 Akiwa mshiriki wa Halmashauri ya Utumishi wa Kutaniko, mwangalizi wa utumishi hupendekeza marekebisho ya lazima katika muundo wa mafunzo ya kitabu. Wakati anapotembelea funzo letu la kitabu, tusikose kuwako na kuhubiri pamoja naye.
5 Washiriki wote wa kutaniko wangepaswa kushiriki kwa hiari katika mipango inayofanywa na mwangalizi wa utumishi. Hilo litafanya iwezekane kwetu kuwa wenye matokeo zaidi katika kazi ya kufanya wanafunzi, na kupata furaha kubwa zaidi katika huduma.
[DO NOT SET] References
1. om 42, 95.
2. km 6/94 2.
3. om 45.