Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/98 uku. 4
  • Mapainia Husaidia Wengine

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mapainia Husaidia Wengine
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kupanua Utumishi Wako
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Baraka Zinazotokana na
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Kumbusho kwa Mwandishi na Mwangalizi wa Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Urekebishaji wa Idadi ya Saa Zinazoombwa kwa Mapainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 10/98 uku. 4

Mapainia Husaidia Wengine

1 Yesu alisema: “Kwa kweli, mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana-mkubwa wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.” Kwa kuwa wavunaji walikuwa wachache katika karne ya kwanza na eneo lao lilikuwa kubwa, Yesu angaliweza kuwatuma mmoja mmoja wapeleke habari njema ili kufikia watu wengi iwezekanavyo. Walakini, yeye ‘aliwatuma wawili-wawili.’ (Lk. 10:​1, 2) Kwa nini wawili-wawili?

2 Wanafunzi hao walikuwa wapya na wasio na uzoefu. Kwa kuhubiri pamoja, wangeweza kuzoezana na kutiana moyo. Kama Solomoni alivyosema, “wawili ni vizuri kuliko mmoja.” (Muh. 4:​9, 10) Hata baada ya kumwagwa kwa roho takatifu kwenye Pentekoste 33 W.K., Paulo, Barnaba, na wengine walikwenda pamoja na waamini katika huduma. (Mdo. 15:35) Lilikuwa pendeleo kama nini kwa wale waliofundishwa binafsi na wanaume hao wenye uwezo!

3 Programu Nzuri ya Mazoezi: Kama vile kifano chake cha karne ya kwanza, kutaniko la Kikristo leo limepangwa kitengenezo ili kuhubiri. Linatuandalia vilevile mazoezi. Kila mmoja wetu angepaswa kuwa na tamaa ya kutoa habari njema kwa matokeo zaidi iwezekanavyo. Ili wahubiri wengi zaidi wafanye matokeo hayo yawe bora, msaada wapendekezwa.

4 Kwenye Shule ya Huduma ya Ufalme iliyofanywa juzijuzi, Sosaiti ilitangaza kuanzishwa kwa programu ya msaada ambao mapainia watawatolea wengine katika huduma. Je! kuna uhitaji katika upande huo? Ndiyo. Zaidi ya wahubiri milioni moja walibatizwa katika hii miaka mitatu iliyopita, na wengi wao wanahitaji kuzoezwa ili wawe wenye matokeo zaidi katika mahubiri. Ni nani ambao mtu aweza kukimbilia ili watimize uhitaji huo?

5 Mapainia waweza kusaidia. Tengenezo la Yehova huwapa mashauri mengi na mazoezi. Muda wa yale majuma mawili ambayo Shule ya Mapainia huchukua, wao hupokea maagizo yenye kulingana na mahitaji yao. Wanafaidika vilevile na mikutano pamoja na mwangalizi wa mzunguko na wa wilaya, na pia mashauri wanayopewa na wazee. Bila shaka si mapainia wote walio na uzoefu kama ule waliokuwa nao Paulo na Barnaba, lakini wanapata mafundisho mazuri ajabu, na watafurahi kuyashiriki na wengine.

6 Ni Nani Watakaofaidika na Programu Hiyo? Je! ni wahubiri wapya au wale waliobatizwa juzijuzi tu ndio wanaohusika? Hata kidogo! Wakristo vijana na pia wengine wenye umri mkubwa zaidi ambao walijua kweli miaka mingi iliyopita wangethamini kusaidiwa katika pande fulani za huduma. Wengine hugawa vichapo vingi, jambo ambalo ni zuri, lakini wana ugumu wa kufanya ziara za kurudia au kuanzisha mafunzo ya Biblia. Wengine huanzisha mafunzo ya Biblia kwa urahisi, lakini wanatambua kwamba watu wale wanaojifunza nao hawafanyi maendeleo. Ni kitu gani kinachowazuia? Mapainia wenye uzoefu wataombwa watoe msaada katika pande hizo. Mapainia wengine hufaulu kuchochea kupendezwa, kuanzisha mafunzo ya Biblia na kuongoza wanafunzi kwenye tengenezo kwa urahisi. Uzoefu wao utakuwa wenye mafaa katika programu hiyo mpya.

7 Je! unaona kwamba programu yako ya kazi haikuruhusu utegemeze mikutano ya utumishi wa shambani ya kutaniko kwa kadiri ambavyo ungetaka? Painia mmoja ataweza labda kutumika na wewe wakati ambapo wahubiri wengine hawapatikani.

8 Ushirikiano Mwema Wahitajiwa: Mara mbili kwa mwaka, wazee watafanya mipango ili wahubiri wanaotamani kupata msaada wa binafsi waupate kupitia programu “Mapainia Husaidia Wengine.” Ikiwa unakubali kufaidika na msaada huo, zungumza na painia aliyegawiwa kukushughulikia, fanya programu ya utumishi yenye kufaa na uiheshimu. Heshimu mapatano yote ya kukutana. Wakati mnapohubiri pamoja, ona njia zenye matokeo za kutoa habari njema. Fikiria sababu zinazofanya njia fulani za kukaribia watu ziwe na matokeo. Usipuuze madokezo anayokutolea painia ili kufanya labda utoaji wako mbalimbali uwe bora. Ikiwa unatumikisha mambo unayojifunza, maendeleo yako katika huduma yatakuwa wazi kwako na kwa wengine. (Ona 1 Timotheo 4:​15.) Mhubiri pamoja mara nyingi iwezekanavyo, mshiriki katika pande zote za huduma, kutia ndani ushahidi wa vivi hivi, lakini mkikaza fikira kwenye hali ya pekee ambayo inataka upate msaada.

9 Mwangalizi wa utumishi atashughulikia maendeleo yatakayofanywa. Pindi kwa pindi, yeye atamwuliza kiongozi wa funzo la kitabu lenu faida ambazo unapata kutokana na programu. Mwangalizi wa mzunguko atakusaidia vilevile anapozuru kutaniko lenu.

10 Yehova ataka kwamba watu wake wazoezwe na ‘waandaliwe vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.’ (2 Tim. 3:​17) Tuone programu “Mapainia Husaidia Wengine” kuwa mpango bora uliokusudiwa kusaidia wale wanaotamani kufanya uwezo wao wa kuhubiri neno uwe bora. Ikiwa tunalo pendeleo la kushiriki katika programu hiyo, acheni tufanye hivyo kwa shukrani, unyenyekevu, na shangwe.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine