Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/98 uku. 1
  • Inafaa Wote ‘Wakubali Neno Kwa Ukunjufu Wa Moyo’!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Inafaa Wote ‘Wakubali Neno Kwa Ukunjufu Wa Moyo’!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi Ya Kufanya Wanafunzi Kwa Msaada Wa Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Saidia Mwanafunzi Wako wa Biblia Afikie Kubatizwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Pili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 11/98 uku. 1

Inafaa Wote ‘Wakubali Neno Kwa Ukunjufu Wa Moyo’!

1 Mamilioni ya watu ni wenye kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Ili wajifanye wenye kustahili uhai udumuo milele, inafaa ‘wakubali neno kwa ukunjufu wa moyo,’ kama walivyofanya wale 3 000 waliotubu na kubatizwa kwenye Pentekoste 33 W.K. (Mdo. 2:​41) Jambo hilo linatutwika daraka gani leo?

2 Tunapaswa kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wasitawishe ujitoaji kwa Yehova. (1 Tim. 4:​7-​10) Kwa kusudi hilo, nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996, fungu 20, yadokeza: “Muda wote wa funzo, tafuta nafasi za kujenga shukrani [kwa] Yehova kwa [sababu] ya sifa zake. Onyesha hisia-moyo za kina kirefu unazohisi kuelekea Mungu. Saidia mwanafunzi kufikiri kwa namna ambayo anaweza kukomaza uhusiano wa kibinafsi na wenye shauku pamoja na Yehova.”

3 Tatizo Tunalokabili: Kwa sababu ya nguvu za dini ya uwongo, watu walio wengi hutosheka na aina ya ibada inayoomba kutumia wakati na jitihada kidogo iwezekanavyo, isiyoomba badiliko lolote la kweli katika namna yao ya maisha. (2 Tim. 3:5) Tatizo linalotukabili ni lile la kusaidia wanafunzi wetu waone kwamba ibada ya kweli inatia ndani mengi zaidi ya kuwa tu wasikilizaji wa neno la Mungu. Inafaa watumie katika maisha yao mambo wanayojifunza. (Yak. 1:​22-​25) Ikiwa jambo fulani kuhusu mwenendo wao binafsi halikubaliwi na Mungu, wanapaswa kutambua wajibu wao wa ‘kugeuka kabisa’ na kufanya yale yaliyo sawa ili kumpendeza yeye. (Mdo. 3:​19) Ili kupata uhai udumuo milele, inafaa ‘wajikakamue wenyewe kisulubu’ na kuchukua msimamo thabiti kwa ajili ya kweli.​—Lk. 13:24, 25.

4 Tunapozungumzia pande mbalimbali za adili, tumwulize mwanafunzi wetu wa Biblia namna anavyoona kwa kweli mambo hayo na yale ambayo angefanya ikiwa anaona uhitaji wa kufanya mabadiliko katika maisha yake. Tuongoze uangalifu wake kwenye tengenezo ambalo kupitia hilo yeye ni mwenye kujifunza kweli, na tumtie moyo ahudhurie mikutano ya kutaniko kwa kawaida.​—Ebr. 10:25.

5 Acheni tujiwekee mradi wa kufanya mafundisho yetu yaguse moyo wa wanafunzi. Tutakuwa wenye furaha tunapochochea wapya wakubali neno la Mungu kwa ukunjufu wa moyo na kubatizwa!​—1 Thes. 2:​13.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine