Mikutano ya utumishi ya agosti
Juma toka Agosti 2
Wimbo 39
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Toa maelezo juu ya ripoti ya utumishi wa shambani ya Aprili katika nchi na katika kutaniko lenu. Tia moyo wahubiri wote washiriki katika huduma ya shambani mnamo Agosti.
Dak. 17: “Thamini Sana Jina Zuri la Yehova.” Fanya maelezo ya utangulizi yasifikie dakika moja, na uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu. Tia mkazo juu ya maandiko yaliyotajwa.—Ona kitabu Kuishi Milele, kurasa 184-5.
Dak. 18: “Elimu ya Kimwili na Miradi Yako ya Kiroho.” Baba mmoja anazungumzia makala pamoja na mwana au binti wake. Wanarudilia pia habari yenye kupatana na hiyo kutoka Amkeni! ya Desemba 22, 1995, kurasa 7-11.
Wimbo 148 na sala ya mwisho.
Juma toka Agosti 9
Wimbo 138
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti.
Dak. 12: Mapainia Husaidia Wengine—Ni Maendeleo Gani Yaliyofanywa? Hotuba na mahojiano vinavyoongozwa na mwangalizi wa utumishi. Rudilia mwongozo uliotolewa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1998, ukurasa 4. Eleza jinsi hilo lilivyopangwa mahali penu, na utoe ripoti ya kisasa kuhusu maendeleo yaliyofanywa na wale waliosaidiwa. Hoji painia mmoja au wawili na baadhi ya wahubiri waliofaidika na msaada wao. Tia moyo wale watakaosaidiwa karibuni wafaidike kikamili na uandalizi huo.
Dak. 25: “Je, Mlango Uongozao Kwenye Upainia Umefunguka Sasa kwa Ajili Yako?” Maulizo na majibu yanayoongozwa na mzee. Kwa namna yenye kufaa, onyesha uwezekano uliopo kwa wahubiri wengi zaidi kupainia. Hoji mapainia ambao wanaweza kueleza kutokana na mambo waliyojionea wenyewe jinsi walivyokuwa na uwezo wa kushinda vizuizi vya kawaida na jinsi walivyofanikiwa. Changanua “Programu za Kielelezo za Painia wa Kawaida,” ukitia mkazo juu ya jinsi kupanga mambo vizuri kunavyoweza kufanya iwezekane kufikia kiwango cha saa. Tangaza kwamba yeyote anayetaka kupata ombi la kuwa painia anaweza kulipata baada ya mkutano.
Wimbo 202 na sala ya mwisho.
Juma toka Agosti 16
Wimbo 131
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kunabaki tu miisho-juma miwili katika mwezi wa Agosti; kwa hiyo, tia moyo kila mmoja ashiriki katika huduma kabla ya mwezi kuisha. Rudilia “Programu Mpya ya Mkusanyiko wa Pekee wa Siku Moja.”
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 20: Je, Unashiriki Katika Kufanya Wanafunzi? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Kwa kuwa kuna kiasi kikubwa cha vichapo tunavyoachia watu, mradi wetu ungepaswa kuwa wa kuanzisha mafunzo ya Biblia ili kusaidia watu wafaidike na vichapo wanavyopokea. Omba wahubiri watoe maelezo juu ya matatizo yanayowazuia kuongoza mafunzo ya Biblia mengi: (1) Katika maeneo fulani, ni vigumu kukuta watu wanaotaka kujifunza. (2) Watu fulani wanaoonyesha kupendezwa husema kwamba wao ni wenye kazi nyingi hivi kwamba hawawezi kujifunza. (3) Baada ya funzo kuanzishwa, ni vigumu kukuta mtu nyumbani ili kufanya funzo liwe la kawaida. Pia vuta uangalifu juu ya mawazo ambayo huenda wahubiri fulani wakawa nayo kuhusu kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia: (1) ‘Sijisikii kuwa mwalimu mwenye kufaa.’ (2) ‘Sina wakati wa kuongoza funzo la Biblia la kila juma.’ (3) ‘Ninasita kujifunga wajibu na mtu mwingine.’ (4) ‘Ninatosheka na kushiriki katika pande nyinginezo za huduma.’ Toa madokezo yenye kufaa juu ya jinsi ya kushinda vizuizi hivyo ili kushiriki kibinafsi katika kazi ya kufanya wanafunzi. Omba wahubiri wenye matokeo waeleze furaha ambayo wamepata katika kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia.—Ona nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 1998, mafungu 3-8, 15.
Wimbo 100 na sala ya mwisho.
Juma toka Agosti 23
Wimbo 94
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Saidieni Wale Waliopendezwa Juzijuzi Wathamini Utakatifu wa Ndoa. Mzee mmoja anaongoza mazungumzo yenye msingi juu ya kitabu Kutoa Sababu, kurasa 241-2. Tunakuta waume na wake wenye kuoana ambao huitikia ujumbe wa Ufalme lakini ambao hawafanyi maendeleo ya haraka kwa sababu wanaishi pamoja bila kuhalalisha ndoa. Zungumzia jinsi ya kuwasaidia waelewe kwa nini Wakristo wanapaswa kushikamana na ndoa yenye kuheshimika. (Ona Amkeni! ya Kifaransa ya Januari 8, 1992, kurasa 26-7.) Toa madokezo kuhusu yale tunayoweza kusema kwa busara ili kusaidia waume na wake kama hao waone kwa nini hawawezi kuwa sehemu ya kutaniko hadi ndoa yao itakapoandikishwa kihalali.
Dak. 20: Moja ya makala ya Julai au Agosti ambayo hamkujifunza kwa sababu ya mkusanyiko wa wilaya, au “Utasema Nini kwa Mbuddha?” Maulizo na majibu. Mara nyingi sisi tunajiuliza jambo la kusema tunapokuta katika eneo watu ambao huamini dini isiyo ya Kikristo ambayo ni yenye msingi juu ya mawazo, mazoea, na desturi tusizozijua. Makala hii inaanza mfululizo wenye sehemu tano juu ya habari hiyo. Fanyeni onyesho la utoaji uliotayarishwa vizuri. Ili kupata habari zaidi juu ya Dini ya Buddha, ona nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1998; kitabu Kutoa Sababu, ukurasa 21; na Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, sura 6.
Wimbo 133 na sala ya mwisho.
Juma toka Agosti 30
Wimbo 99
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote watoe ripoti za utumishi wa shambani za Agosti. Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wangepaswa kuhakikisha kwamba kila mmoja katika kikundi chao ametoa ripoti yake kusudi zote zisafirishwe kufikia Septemba 6.
Dak. 17: Sisi Tunapenda Ndugu Zetu. Hotuba inayofanywa na mzee, ikitia ndani mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakiwa na msingi juu ya Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1, 1995, kurasa 15-17, mafungu 7-11. Tia mkazo juu ya faida tunazopata kwa kujua ndugu zetu vizuri, kushiriki kitia-moyo, na kusaidiana kuvumilia majaribu. Eleza jinsi jambo hilo linavyoweza kufanywa kwa kiwango kikubwa zaidi. Alika wasikilizaji waeleze mambo yaliyoonwa yanayoonyesha jinsi kitia-moyo chenye upendo kutoka kwa wengine kilivyowaburudisha na kuwatia nguvu.
Dak. 18: Toa Sababu ya Tumaini Lako. Mzee anahoji kijana tineja mmoja au wawili wenye mfano wa kuigwa walio katika shule. Kwa kuendelea, wao hupambana na hali ambazo katika hizo vijana wenzao wa ulimwengu hutaka kujua kwa nini vijana wetu huchagua kutojiunga nao katika utendaji wao mbalimbali. Huku wakifaidika na nafasi hizo ili kufasiria imani zao zenye msingi juu ya Biblia, vijana wetu wanahitaji kubaki imara katika kushindana kwao. Kikundi hicho kinazungumzia jinsi wanavyoweza kujibu ikiwa wanatolewa sigara au dawa za kulevya. Rudilia namna ya kufikiri inayotolewa katika kitabu Vijana Huuliza, kurasa 277-81. Fasiria jinsi kutetea azimio lao la kufanya lililo sawa kunavyotumika kuwa ulinzi na jinsi kunavyotoa ushahidi mzuri.
Wimbo 129 na sala ya mwisho.