Mikutano ya utumishi ya Septemba
Juma toka Septemba 6
Wimbo 190
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Toa maelezo juu ya ripoti ya utumishi wa shambani ya Mei katika nchi na katika kutaniko lenu.
Dak. 17: “Je! Wewe Unatumika Ukiwa na Kusudi?” Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, na uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu. Tia ndani maelezo juu ya kitabu Huduma Yetu, kurasa 88-9. Tia moyo wote watimize huduma yao bila ugeugeu na kikamili.
Dak. 18: “Wazazi—Toeni Mfano Mzuri kwa Watoto Wenu.” Utangulizi mfupi unatolewa na mzee, ukifuatwa na mazungumzo ya makala yakifanywa na ndugu wawili walio wazazi. Wanaonyesha hangaiko kuhusu kulinda watoto wao wasipatwe na mazoea na mtazamo mbaya kutokana na shule, televisheni, na washiriki wa familia wasio Mashahidi na wengine. Ndugu hao wanafikiria mitazamo isiyo na heshima, usemi na mavazi vya kilimwengu, na kiburudisho kisichofaa. Baada ya kufikiri juu ya uhitaji wa kutoa mfano mzuri, wanazungumzia njia za kusitawisha shauku kubwa zaidi kuelekea funzo la familia, mikutano ya kutaniko, na utumishi wa shambani.—Ona Amkeni! ya Septemba 22, 1991, kurasa 8-9.
Wimbo 101 na sala ya kumalizia.
Juma toka Septemba 13
Wimbo 171
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti.
Dak. 15: Tulifanya Nini Mwaka Uliopita? Hotuba inayotolewa na mwangalizi wa utumishi. Rudilia mambo makuu kutokana na ripoti ya kutaniko ya mwaka wa utumishi 1999. Toa pongezi kwa mambo mazuri yaliyotimizwa. Onyesha mahali ambapo maendeleo yanaweza kuhitajiwa. Tia mkazo juu ya kile ambacho kutaniko lilifanya kuhusiana na hudhurio kwenye mikutano na kuongoza mafunzo ya Biblia. Toa miradi yenye kufaa kwa ajili ya mwaka ujao.
Dak. 20: “Utasema Nini kwa Mhindu?” Maulizo na majibu. Kazia faida ya kusitawisha uwanja wa makubaliano na mtu, na uonyeshe pande ambazo katika hizo tunaweza kukubaliana na Mhindu. Onyesha jinsi utoaji uliopendekezwa unavyoweza kurekebishwa ili kutoa ushahidi kwa watu wa malezi yoyote ya kidini. Fanyeni onyesho lililotayarishwa vizuri kuhusu kutoa ushahidi kwa Mhindu. Ili kupata habari zaidi juu ya Uhindu, ona nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1998; kitabu Kutoa Sababu, kurasa 21-2; na Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, sura 15.
Wimbo 140 na sala ya kumalizia.
Juma toka Septemba 20
Wimbo 193
Dak. 12: Matangazo ya kwenu na mambo yaliyoonwa katika utumishi wa shambani.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 18: Fanyeni Matumizi Mazuri ya Kitabu Muumba. Hotuba na maonyesho. Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1999 ilifasiria kwamba kitabu Muumba kinaweza kupendekezwa wakati wowote tunapokuta watu ambao (1) hawaamini Mungu au (2) wanaamini Mungu lakini hawana wazo halisi kuhusu yeye ni nani au kuhusu sifa zake na makusudi yake. Yale maulizo na maelezo yenye kuchochea kufikiri kwenye jalada ya mwisho vinaweza kutumiwa ili kuamsha kupendezwa katika kusoma kitabu hicho. Au ukurasa 152 unaweza kutumiwa kwa matokeo. Mhubiri anaweza kuuliza: “Ni wapi ambapo tunaweza kupata shauri bora kabisa kuhusu jinsi ya kutatua matatizo yetu yenye kutatanisha zaidi?” Anaweza kuonyesha mtu jinsi watu wenye mamlaka ambao wanajulikana walivyosifia Mahubiri ya Yesu ya Mlimani, anaweza kumwomba achague moja ya zile nukta saba zinazoonyeshwa ambayo inampendeza zaidi, na kisha asome maandiko fulani yenye kutajwa. Fanyeni maonyesho ya madokezo hayo yote mawili kwa ajili ya kutolea watu kitabu Muumba, mkisema juu ya mpango wa kutoa mchango katika kila utoaji. Tia moyo wote wachukue kitabu hicho katika utumishi wa shambani, wakiwa tayari kukitolea watu kila wakati nafasi inapojitokeza.
Wimbo 175 na sala ya kumalizia.
Juma toka Septemba 27
Wimbo 141
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Septemba. Tia moyo wote wachukue mipango kwa ajili ya kushiriki kikamili katika ugawaji wa magazeti mnamo Oktoba. Rudilia madokezo fulani yaliyotokea katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1996, ukurasa 8, kuhusu jinsi ya kutayarisha utoaji. Kwa kutumia magazeti ya kisasa, taja mambo fulani mazuri yenye kupendeza na mfanye onyesho moja au mawili ya utoaji mfupi. Onyesha jinsi ya kusema na mwenye-nyumba kuhusu mpango wa kutoa mchango.
Dak. 15: Majibu ya Maulizo Yenu. Hotuba inayotolewa na mzee. Tia ndani maelezo yenye kupatana na habari hiyo kutokana na Huduma Yetu ya Ufalme ya Desemba 1995, ukurasa 5, na kisanduku “Wakati Wako Una Thamani Kadiri Gani?” katika Amkeni! ya Julai 22, 1997, ukurasa 13.
Dak. 15: “Ibada ya Kweli Ni Yenye Kupanuka Katika Ulaya ya Mashariki.” Mzee anaongoza kipindi hiki kwa maulizo na majibu. Taja mambo yaliyoonwa au ushuhuda unaoonyesha ongezeko katika nchi zinazowakilishwa, kama inavyoripotiwa katika Vitabu-Mwaka vya juzi-juzi.
Wimbo 87 na sala ya kumalizia.