Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea watu mnamo Septemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Oktoba: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo kupendezwa kunaonekana wakati wa ziara ya kurudia, uandikishaji unaweza kupendekezwa. Novemba: Mungu Anataka Nini Kwetu? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Desemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele pamoja na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.
◼ Mwangalizi msimamizi au mtu mwingine atakayechaguliwa naye angepaswa kufanya uchunguzi wa akaunti za kutaniko mnamo Septemba 1 au mapema zaidi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Jambo hilo litakapokuwa limefanywa, fanyeni tangazo kwa kutaniko baada ya kusoma ripoti ya akaunti ya kawaida.
◼ Wazee wanakumbushwa kufuata maagizo yaliyotolewa kwenye kurasa 21-3 za Mnara wa Mlinzi wa Aprili 15, 1991, kuhusu mtu yeyote aliyetengwa au aliyejitenga mwenyewe ambaye anaweza kuwa na mwelekeo wa kutaka kurudishwa.
◼ Ni jambo la lazima kwamba vikundi vya watu 15 au zaidi wanaopanga kutembelea makao ya Sosaiti wajulishe kwanza ofisi ya Betheli kupitia barua. Tafadhali, tumeni habari kuhusu hesabu ya wale watakaokuja na pia tarehe na saa ya ziara hiyo. Kabla ya ziara yenu, tafadhali rudilieni Majibu ya Maulizo Yenu katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 1998.
◼ Wale wanaoshirikiana na kutaniko wangepaswa kutuma uandikishaji mpya na uandikishaji wenye kufanywa upya wote kwa Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, kutia ndani uandikishaji wao wenyewe, kupitia kutaniko.
◼ Sosaiti haitoi vichapo vinavyoombwa kwenye maombi ya vichapo ya wahubiri binafsi. Mwangalizi msimamizi angepaswa kufanya mipango ili tangazo lifanywe kila mwezi kabla ya ombi la kila mwezi la vichapo la kutaniko kutumwa kwa Sosaiti, kusudi wale wote wanaopendezwa na kupata vichapo vya binafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulika na vichapo. Tafadhali kumbukeni ni nini vilivyo vichapo vyenye kufanyiwa ombi la pekee.
◼ Makusanyiko ya wilaya au ya kimataifa 1998 “Njia ya Mungu ya Maisha” yalikuwa baraka kwelikweli kwa wahudhuriaji wote. Kati yao, kulikuwa wamishonari na watumishi wa kimataifa 2,764 walioweza kurudi katika nchi zao walikotoka, kupitia zawadi za ukarimu zilizotolewa na makutaniko. Utegemezo uliotolewa kwa mpango huo unathaminiwa sana. Kwa kuwa makusanyiko hayo yamemalizika, fedha za ziada zinatumiwa ili kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote ya kuhubiri.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Sikiliza Unabii wa Danieli! —Kiingereza, Kifaransa, Lingala