Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/99 uku. 2
  • Mikutano ya utumishi ya Novemba

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mikutano ya utumishi ya Novemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Vichwa Vidogo
  • Juma toka Novemba 1
  • Juma toka Novemba 8
  • Juma toka Novemba 15
  • Juma toka Novemba 22
  • Juma toka Novemba 29
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 11/99 uku. 2

Mikutano ya utumishi ya Novemba

Juma toka Novemba 1

Wimbo 156

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Rudilia “Ona Nguvu ya Biblia!”

Dak. 15: “Mahubiri Hututofautisha Sisi.” Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, na uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu. Kwa kutumia kitabu Ujuzi, ukurasa 173, fungu 8, eleza kwa kifupi yale tunayoweza kusema ili kutia moyo mwanafunzi wa Biblia ajitahidi kufikia kushiriki katika huduma.

Dak. 20: “Ni Nani Awezaye Kukubali Funzo la Biblia?” Hotuba na maonyesho. Kwa kupatana na fungu 4, dokeza njia mbalimbali za kuchochea watu wapendezwe na kujifunza yale yaliyo katika vitabu vyetu. Fanyeni maonyesho mawili mafupi yanayoonyesha jinsi jambo hilo linavyoweza kufanywa. Alika wasikilizaji waseme jinsi walivyopata matokeo katika kuanzisha mafunzo.

Wimbo 198 na sala ya kumalizia.

Juma toka Novemba 8

Wimbo 204

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti. Kumbusha akina ndugu wajitayarishe kwa ajili ya mazungumzo ya juma lijalo ya mafungu 18 ya kwanza ya nyongeza ya Novemba.

Dak. 15: Majibu ya Maulizo Yenu. Hotuba. Onyesha mipango ya kwenu ili kudumisha Jumba la Ufalme likiwa safi na lenye hali nzuri.

Dak. 20: “Utasema Nini kwa Mwislamu?” Maulizo na majibu. Kazia uhitaji wa kuonyesha utambuzi wakati wa kuzungumza na watu wa tamaduni nyingine. Fanyeni onyesho la utoaji uliotayarishwa vizuri. Ili kupata habari zaidi kuhusu Uislamu, ona nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1998; kitabu Kutoa Sababu, kurasa 23-4; na Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, sura 12.

Wimbo 208 na sala ya kumalizia.

Juma toka Novemba 15

Wimbo 211

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Kumbusha mipango iliyochukuliwa kwa ajili ya mahubiri. Toa maelezo kuhusu ripoti ya utumishi wa shambani ya Julai katika nchi na katika kutaniko lenu.

Dak. 25: Mahitaji ya kutaniko au “Matumizi ya Internet​—Fanyeni Angalisho kwa Hatari!” Mazungumzo ya maulizo na majibu ya mafungu 1-18. Someni mafungu 4-7, 12, 16, 17. Tia moyo wote wajitayarishe kwa ajili ya mazungumzo ya juma lijalo ya mafungu 19-36.

Dak. 12: Wazazi​—Je! Nyinyi Huongoza Funzo la Familia la Kawaida? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Fasiria kwa nini familia zinahitaji kujifunza pamoja. (Ona Kiongozi cha Shule, kurasa 37-8.) Zungumzia mambo yafuatayo ambayo hu­zuia funzo la familia: (1) kufikiri kwamba watoto ni wachanga mno hivi kwamba hawawezi kufaidika, (2) kufikiri kwamba kuhudhuria mikutano ya kutaniko kunatosha, (3) kuchoka kwa sababu ya programu zenye shughuli nyingi, na (4) kukengeushwa na kutazama televisheni. (Ona Mnara wa Mlinzi wa Mei 15, 1994, kurasa 11-12.) Alika vichwa vya familia waeleze jinsi wanavyoshinda mambo yanayowazuia kudumisha programu nzuri ya funzo la familia. Kazia kwamba hilo linaomba jitihada, nia thabiti, na ushirikiano.

Wimbo 217 na sala ya kumalizia.

Juma toka Novemba 22

Wimbo 158

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na mambo yaliyoonwa katika utumishi wa shambani.

Dak. 10: Ni Nini Mtazamo Wako Kuelekea Migawo? Hotuba inayofanywa na mzee. Kuna orodha ndefu ya mambo ya lazima yanayoombwa ili kufanya kutaniko liendelee kufanya kazi: kutayarisha migawo ya programu; kuchukua wengine kwa ajili ya mikutano au kuwapeleka katika utumishi; kusaidia wazee-wazee; na kusafisha, kutengeneza, na kushughulika na Jumba la Ufalme, kutia ndani majani yenye kupandwa uwanjani. Wewe huitikiaje wakati unapoombwa kusaidia? Wengine wanaweza kukataa, kukubali kwa moyo usiotaka, au kushindwa kuendeleza kazi hadi kuimaliza. Zungumzia kwa nini kukubali na kutimiza migawo ni pendeleo lenye furaha. Tia moyo wote katika kutaniko waonyeshe roho tayari ya kujitakia.​​—Zab. 110:3; Isa. 6:8.

Dak. 25: Mahitaji ya kutaniko au “Matumizi ya Internet​—Fanyeni Angalisho kwa Hatari!” Mazungumzo ya maulizo na majibu ya mafungu 19-36. Someni mafungu 23-5 na 34-6.

Wimbo 223 na sala ya kumalizia.

Juma toka Novemba 29

Wimbo 215

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Novemba.

Dak. 15: Tieni Moyo Wapya Wahudhurie Mikutano. Mazungumzo kati ya mzee na mtumishi wa huduma mmoja au wawili, yenye msingi juu ya broshua​—Wanafanya Mapenzi ya Mungu, kurasa 14-15. Rudilia kwa nini ni jambo la lazima kwamba wapya wahudhurie mikutano. Huko kwenye mikutano watapokea sehemu kubwa ya elimu yao, kitia-moyo, na msaada. Rudilia ile mikutano mitano ya kila juma, ukifasiria faida za kila mmoja. Sema jinsi mikutano inavyositawisha mwenendo wa kimungu, kujenga hali ya kiroho, kutuvuta kwenye tengenezo, kutusaidia kusitawisha vifungo vya karibu pamoja na wengine, na kutusaidia kuelewa kusudi la huduma yetu. Tia moyo wasikilizaji watumie broshua hiyo ili kuchochea wapya waje kwenye mikutano.

Dak. 20: Chaguo Letu​—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Hotuba na maonyesho. Kati ya matengenezo ya kidini, tengenezo letu ni la pekee kwa sababu tunatangaza, tunatumia, na tunagawa tafsiri ya Biblia iliyofanywa na waabudu watiwa-mafuta wa Yehova. Si kwamba tunataka kufaidika kibiashara au kueneza imani za farakano. Badala yake, tunachochewa na tamaa ya kuheshimu jina la Mungu na kusaidia wengine wapate kumjua vizuri zaidi. Mara nyingi, tafsiri nyinginezo hutafsiri Neno la Mungu kwa namna isiyosikika; kwa hiyo rudilia faida zilizo wazi za Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. (Ona kitabu “Kila Andiko,” kurasa 327-31. Ona maelezo katika fungu 3, onyesha mifano ya tafsiri zilizofanywa kuwa bora katika fungu 6, na utie mkazo juu ya faida zinazozungumziwa katika mafungu 22-3.) Fanyeni maonyesho mawili mafupi yanayodokeza jinsi tunavyoweza kujibu wakati wengine wanaposema, “Ninyi mna Biblia yenu wenyewe.”​—Ona kitabu Kutoa Sababu, kurasa 251-2.

Wimbo 205 na sala ya kumalizia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine