Unapofanya ziara za kurudia kwa wale ulioachia magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, unaweza kusema hivi:
“Mara ya mwisho nilipokutembelea, nilifurahi kukuachia nakala ya gazeti Mnara wa Mlinzi. Labda ulitambua kwamba kichwa kamili cha gazeti hilo ni Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova. Leo, ninataka kukueleza Ufalme huo ni nini na kile ambacho unaweza kumaanisha kwako na kwa familia yako.” Kisha, fungua broshua Anataka kwenye somo la 6, na usome na kuzungumzia habari nyingi zaidi kulingana na wakati msikilizaji alio nao.
◆
“Nilikutembelea juzijuzi, nami nilikuachia nakala za magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Magazeti hayo yanaongeza uthamini wa watu kuelekea Biblia na uongozi wake wa kiadili. Kwa kuwa ninafikiri kuwa jambo la maana sana kwa kila mmoja kuelewa Neno la Mungu, nimerudi ili kukuonyesha kitu fulani kitakachokusaidia kufanya hivyo.” Toa broshua Anataka au kitabu Ujuzi, na upendekeze funzo la Biblia.
Unapotolea watu chochote cha vitabu vya zamani vyenye kurasa 192, unaweza kujaribu utoaji huu:
“Mkazo mwingi umetiwa juu ya uhitaji wa kuwa na elimu nzuri. Kwa maoni yako, ni elimu gani ambayo mtu anapaswa kufuatia ili kupata furaha kubwa zaidi na mafanikio maishani? [Acha mtu ajibu. Kisha, soma Mezali 9:10, 11.] Kitabu hiki [soma kichwa cha kitabu unachopendekeza] kinategemea Biblia. Kinavuta uangalifu juu ya chanzo pekee cha ujuzi unaoweza kuongoza kwenye uhai wa milele.” Onyesha mfano fulani hasa katika kitabu, na umtie mtu moyo akisome.
Ikiwa umepata utoaji wenye matokeo katika kukomaza kupendezwa, kwa vyovyote endelea kuutumia! Uurekebishe tu ili kuupatanisha na toleo la vichapo la mwezi wa sasa.
[Picture on page 6]
Vichapo Vingine
Utoaji mbalimbali uliopendekezwa kuhusu vitabu na broshua zingine unaweza kupatikana katika Index des publications de la Société Watch Tower chini ya:
Présentations
Liste par publications
[Picture on page 6]
Utoaji wa Moja kwa Moja
Ili kuanzisha funzo la Biblia, jaribu kutumia mmoja wa utoaji huu mbalimbali wa moja kwa moja:
“Je, unajua kwamba kwa dakika chache tu unaweza kupata jibu kwa ulizo la maana la Biblia? Kwa mfano, . . . ” Kisha, uliza ulizo linaloonekana mwanzoni mwa moja ya yale masomo yaliyo katika broshua Anataka na ambalo unafikiri litamvutia mtu unayezungumza naye.
“Ninakutembelea ili kukuonyesha programu yetu ya funzo la Biblia bila malipo. Inaomba dakika tano hivi ili kukuonyesha jinsi linavyofanywa. Je, unazo dakika tano?” Ikiwa jibu ni ndiyo, tumia somo la 1 katika broshua Anataka ili kuonyesha jinsi funzo linavyofanywa, ukisoma tu andiko moja au mawili uliyochagua. Baadaye, uliza: “Ni wakati gani utakapokuwa na dakika 15 ili tuzungumzie somo lenye kufuata?”
“Watu wengi wanayo Biblia, lakini hawatambui kwamba ina majibu ya maulizo ya maana tuliyo nayo sote kuhusu wakati wetu ujao. Kwa kutumia msaada huu kwa ajili ya funzo [broshua Anataka au kitabu Ujuzi] kwa saa moja au zaidi kwa juma, unaweza kupata uelewevu wa msingi wa Biblia kwa kipindi cha miezi michache tu. Nitakuwa mwenye furaha kukuonyesha jinsi programu hiyo inavyofanya kazi.”
“Ninakutembelea ili kukutolea funzo la Biblia la nyumbani bila malipo. Ningetaka kutumia tu dakika chache ili kuonyesha jinsi watu katika nchi 200 hivi wanavyozungumzia Biblia nyumbani wakiwa vikundi vya familia. Tunaweza kutumia chochote cha vichwa hivi vya habari kuwa msingi wa mazungumzo. [Onyesha yaliyomo katika kitabu Ujuzi.] Ni habari gani inayokupendeza kipekee?” Ngoja mtu achague. Fungua sura inayochaguliwa, na uanze funzo katika fungu la kwanza.
“Ninatoa mafunzo ya Biblia bila malipo na nina wakati katika programu yangu kwa ajili ya wanafunzi zaidi. Kitabu hiki chenye kusaidia kujifunza Biblia ndicho tunachotumia. [Onyesha kitabu Ujuzi.] Funzo huchukua miezi michache tu, nalo hutoa majibu kwa maulizo kama vile: Sababu gani Mungu huruhusu kuteseka? Kwa nini tunazeeka na kufa? Ni nini kinachowapata wapendwa wetu waliokufa? Na tunawezaje kumkaribia Mungu? Je, ninaweza kuonyesha jinsi ya kujifunza somo moja?”