Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kabla ya 1987 kilicho katika stoki ya kutaniko. Makutaniko yaliyo na Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu yanaweza kukitolea watu. Februari: Kitabu chochote cha zamani chenye kurasa 192 kilicho katika stoki ya kutaniko. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Aprili: Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Toleeni watu broshua Anataka, mkiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani.
◼ Wahubiri wote wenye kubatizwa watakaokuwako kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Februari 4 wanaweza kupokea kadi Instructions médicales na Document d’identité médical kwa ajili ya watoto wao.
◼ Kuanzia Februari, wala si baada ya Machi 3, hotuba mpya ya watu wote itakayotolewa na waangalizi wa mzunguko itakuwa “Kupata Usalama Katika Ulimwengu Wenye Hatari.”
◼ Makutaniko yanapaswa kuchukua mipango yenye kufaa ili kuadhimisha Ukumbusho mwaka huu, Siku ya Nne, Machi 28, baada ya jua kutua. Ingawa hotuba inaweza kuanza mapema, kupitishwa kwa mifano hakupaswi kuanza mpaka jua linapokuwa limetua. Chunguzeni kutoka vyanzo vya kwenu ili mjue wakati ambapo jua litatua katika eneo lenu. Ingawa ni vizuri kila kutaniko lifanye mwadhimisho walo lenyewe wa Ukumbusho, huenda hilo lisiwezekane sikuzote. Mahali ambapo makutaniko fulani hutumia kwa kawaida Jumba la Ufalme lilelile, labda kutaniko moja au zaidi yanaweza kupata kibali cha kutumia jengo lingine jioni hiyo. Mahali ambapo inawezekana, tungependekeza afadhali kuwe na dakika 40 katikati ya programu mbalimbali kusudi wote wafaidike kikamili na tukio hilo; jambo hilo litafanya iwezekane kukutana na wageni na kutia moyo wale waliopendezwa karibuni. Ufikirio unapaswa pia kutolewa kuhusiana na hali za usafiri na uegeshaji wa magari, kutia ndani kuacha na kutwaa wasafiri. Baraza la wazee linapaswa kuamua ni mipango gani inayoweza kuwa bora zaidi mahali pao.
◼ Amkeni! katika Cibemba itabadilishwa toka toleo la mara moja kwa mwezi kuwa toleo la baada ya kila miezi mitatu.
◼ Matoleo ya Amkeni! ya Januari 8 na Januari 22, 2002, yatazungumzia habari zenye kupendeza watu ulimwenguni pote: kuanguka kwa ile minara miwili yenye kufanana ya World Trade Center huko New York, tatizo la wakimbizi ulimwenguni, na mateso ya Mashahidi wa Yehova huko Georgia. Kwa kuwa habari hizo ni zenye kupendeza kipekee, maombi ya makutaniko yataongezwa kwa asilimia 20 kuhusu matoleo hayo.
◼ Amkeni! ya Februari 8, 2002, itazungumzia habari ‘Siku ya Arusi Yenye Shangwe.’ Bila shaka, habari hiyo itaamsha kupendezwa kwa wengi katika eneo letu. Kwa hiyo, ombi la kawaida la kila kutaniko litaongezwa kwa asilimia 15 kuhusu toleo hilo.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Kiingereza: Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? (T-26); Kuyachunguza Maandiko Kila Siku 2002; Index 1986-2000.
Kifaransa: Annuaire 1999; Index 1986-95; buku la Mnara wa Mlinzi 1996; buku la Amkeni! 1995, 1996, 1997; Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? (T-26); Unabii wa Isaya I, miandiko mikubwa.
Kiswahili: Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? (T-26); Unabii wa Isaya I, miandiko mikubwa.