Mashirika Mapya Yaliyoundwa
Toleo la Mnara wa Mlinzi la Januari 15, 2001, liliripoti namna ya kitengenezo ambayo kwa hiyo Mashahidi wa Yehova wanaendelea kusonga mbele na kazi ya Ufalme katika dunia yote. Lilieleza pia jinsi mashirika mbalimbali ya kisheria yanavyotumiwa kuwa vyombo vya kufanya iwe vyepesi kueneza habari njema. Mashirika hayo ni ya lazima ili kujipatanisha na sheria za taifa, kama vile Neno la Mungu linavyoomba. (Rom. 13:1) Kwa sababu ya ukubwa na sehemu mbalimbali za kazi yetu, Baraza Linaloongoza limekubali kuundwa kwa mashirika ya zaidi ili kushughulikia mahitaji fulani ya Mashahidi wa Yehova huko Amerika. Mashirika mapya ni haya:
Christian Congregation
of Jehovah’s Witnesses
Religious Order
of Jehovah’s Witnesses
Kingdom Support
Services, Inc.
Mashirika hayo yatafanya kazi pamoja na Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc. Ushirikiano na marekebisho hayo yaliyofanywa na Baraza Linaloongoza katika kutimiza mgawo wayo wa kutunza mali yote ya Bwana-Mkubwa utathaminiwa sana.—Mt. 24:45-47.