Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/02 uku. 3-6
  • Programu Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2003

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2003
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Vichwa Vidogo
  • Maagizo
  • PROGRAMU
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 10/02 uku. 3-6

Programu Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2003

Maagizo

Mnamo 2003, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi itaendeshwa kulingana na mipango ifuatayo.

VICHAPO VITAKAVYOTUMIWA: Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo [bi7], Biblia [La Sainte Bible en swahili du Zaïre], Mnara wa Mlinzi [w], Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi [be], “Kila Andiko Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa” (Chapa ya 1992) [si], na Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko (Chapa ya 1989) [rs-SW].

Shule inapaswa kuanza PA WAKATI, kwa wimbo, sala, na maneno ya ukaribishaji, kisha utaratibu ufuatao unapaswa kufuatwa:

SIFA YA USEMI: Dakika 5. Mwangalizi wa shule, mshauri msaidizi, au mzee mwingine anayestahili atazungumzia sifa moja ya usemi akitumia habari kutoka katika kitabu cha Shule ya Huduma. (Katika makutaniko yenye wazee wachache, mtumishi wa huduma anayestahili anaweza kutoa hotuba hiyo.) Isipokuwa maagizo tofauti yanatolewa, visanduku vilivyo kwenye kurasa zilizotolewa kuwa mgawo vinapaswa kutiwa ndani ya mazungumzo. Mazoezi yanayotiwa ndani ya kila somo hayapaswi kushughulikiwa. Hayo yamekusudiwa kutumiwa na kila mwanafunzi kibinafsi na kwa ajili ya kutoa shauri la siri.

MGAWO NA. 1: Dakika 10. Hotuba hii inapaswa kutolewa na mzee au mtumishi wa huduma, na habari zitategemea Mnara wa Mlinzi, Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, au “Kila Andiko Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa.” Hii ni hotuba ya maagizo ya dakika kumi bila maulizo ya kujikumbusha. Lengo la hotuba halipaswi kuwa kuzungumzia tu habari lakini kukaza uangalifu juu ya jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa maishani, na vilevile kukazia habari ambazo zitasaidia hasa kutaniko. Kichwa cha habari kinachoonyeshwa kwenye programu kinapaswa kutumiwa. Ndugu wanaogawiwa hotuba hiyo wanatarajiwa kumaliza pa wakati. Shauri linaweza kutolewa kwa siri inapohitajika.

MAMBO MAKUU KUTOKA USOMAJI WA BIBLIA: Dakika 10. Mzee au mtumishi wa huduma anayestahili anapaswa kutumia dakika sita za kwanza ili kuonyesha jinsi habari hiyo inavyohusu kutaniko lenu. Anaweza kutoa maelezo kuhusu sehemu yoyote ya usomaji wa Biblia wa juma hilo, kwa kuwa ndugu anayetoa mgawo Na. 2 hatatoa maelezo juu ya mistari anayosoma. Maelezo hayo hayapaswi kuwa tu muhtasari wa usomaji wa Biblia. Lengo kuu ni kusaidia wasikilizaji waelewe kwa nini habari hiyo ni yenye faida na jinsi inavyotufaidi. Kisha, muda wa dakika nne, msemaji ataomba wasikilizaji washiriki kwa kutoa maelezo mafupi (yasiyozidi sekunde 30) juu ya maulizo haya mawili: “Uliona nini katika usomaji wa Biblia wa juma hili kitakachokusaidia katika huduma yako au maishani mwako?” na “Ni nini kilichoimarisha imani yako na kuzidisha uthamini wako kwa Yehova?” Kisha mwangalizi wa shule ataruhusu wanafunzi walio na migawo katika shule ya pili na ya tatu kuondoka.

MGAWO NA. 2: Dakika 4. Huu ni usomaji unaopaswa kutolewa kwa ndugu. Kwa kawaida sehemu fulani ya Biblia itasomwa. Mara moja kwa mwezi sehemu fulani katika Mnara wa Mlinzi itasomwa. Mwanafunzi anapaswa kusoma habari aliyogawiwa bila kutoa utangulizi wala maneno ya kumalizia. Sehemu zilizopangwa kusomwa hazitakuwa na urefu uleule kila juma, lakini sehemu zote zinapaswa kusomwa kwa dakika nne au chini ya dakika nne. Mwangalizi wa shule anapaswa kuchunguza habari kabla ya kuigawia msomaji, ili kuhakikisha kwamba habari inafaa umri na uwezo wa wanafunzi. Mwangalizi wa shule atapenda hasa kusaidia wanafunzi kusoma kwa njia ya kueleweka, kwa ufasaha, kukazia maana kwa njia inayofaa, kuwa na ubadilifu wa sauti, kutua kwa njia inayofaa, na kusoma jinsi ambavyo watu huongea kwa kawaida.

MGAWO NA. 3: Dakika 5. Dada atagawiwa mgawo huu. Wanafunzi wanaogawiwa mgawo huu watachagua kikao au wataonyeshwa kikao cha kutumiwa katika orodha kwenye ukurasa wa 82 katika kitabu cha Shule ya Huduma. Mwanafunzi anapaswa kutumia kichwa kinachoonyeshwa katika programu na kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa katika utumishi wa shambani katika eneo la kutaniko lao. Ikiwa vichapo vya kutumiwa ili kupata habari havionyeshwi, itambidi mwanafunzi kufanya utafiti wa habari hiyo katika vichapo vilivyotolewa na mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Wanafunzi wapya wanapaswa kupewa migawo ambayo kwa ajili ya hiyo vichapo vya kutumia vinaonyeshwa. Mwangalizi wa shule atapenda hasa kuona jinsi mwanafunzi anavyofafanua habari hiyo na jinsi anavyosaidia mwenye nyumba kuelewa maana ya Maandiko na kuelewa mambo makuu. Wanafunzi wanaopewa migawo hiyo wanapaswa kujua kusoma. Mwangalizi wa shule atachagua msaidizi mmoja.

MGAWO NA. 4: Dakika 5. Mwanafunzi anapaswa kutumia kichwa kinachoonyeshwa katika programu. Ikiwa vichapo vya kutumiwa havionyeshwi, itambidi mwanafunzi kufanya utafiti kuhusu habari hii katika vichapo vilivyotolewa na mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Ndugu anapopewa mgawo huo, anaweza kuutayarisha ili ufae wasikilizaji kwenye Jumba la Ufalme. Dada anapopewa mgawo huo, unapaswa kutolewa siku zote jinsi Mgawo Na. 3 unavyotolewa. Tafadhali ona kwamba habari zenye kufuatwa na nyota zinapaswa kugawiwa ndugu pekee na kutolewa kama hotuba.

WAKATI: Hotuba na maelezo ya mshauri hayapaswi kamwe kupitisha wakati uliowekwa. Wanafunzi wanaotoa migawo Na. 2 hadi 4 wanapaswa kukatizwa kwa upole wakati wao unapokwisha. Ndugu wanaotoa hotuba juu ya sifa ya usemi, Hotuba Na. 1, au mambo makuu kutoka usomaji wa Biblia, wanapaswa kushauriwa kwa siri wanapopitisha wakati uliowekwa. Wote wanapaswa kuwa waangalifu ili kuheshimu wakati vizuri. Programu nzima: Dakika 45, bila kutia ndani wimbo na sala.

SHAURI: Dakika 1. Mwangalizi wa shule atatumia muda usiozidi dakika moja baada ya hotuba ya kila mwanafunzi ili kutoa maelezo yanayojenga kuhusu sehemu ya hotuba inayostahili kusifiwa. Lengo lake si la kumpongeza tu, lakini kuonyesha ni kwa nini jambo fulani katika hotuba lilikuwa zuri. Kulingana na uhitaji wa kila mwanafunzi, shauri linaweza kutolewa baada ya mkutano au wakati mwingine ili kumsaidia kufanya maendeleo.

MSHAURI MSAIDIZI: Zaidi ya mwangalizi wa shule, baraza la wazee linaweza kuchagua mzee mwingine mwenye uwezo, ikiwa anapatikana, ili kumweka kuwa mshauri msaidizi. Daraka lake litakuwa kuwashauri akina ndugu wanaoshughulikia Mgawo Na. 1 na mambo makuu kutoka usomaji wa Biblia, wanapohitaji kushauriwa. Si lazima awashauri wazee wenzake au watumishi wa huduma kila mara wanapotoa hotuba hizo. Utaratibu huo utafuatwa katika mwaka wa 2003 na huenda ukarekebishwa baada ya hapo.

FOMU YA MASHAURI: (Katika kitabu cha shule)

KUJIKUMBUSHA KWA MANENO TU: Dakika 30. Baada ya kila miezi miwili, mwangalizi wa shule ataongoza kujikumbusha kwa maneno tu. Sehemu hiyo itafanywa baada ya hotuba juu ya sifa ya usemi na mambo makuu kutoka usomaji wa Biblia, kama inavyoonyeshwa hapo juu. Kujikumbusha kwa maneno tu kutategemea habari zilizozungumziwa katika shule mnamo miezi miwili iliyotangulia, kutia ndani juma la kujikumbusha.

PROGRAMU

Jan. 6 Usomaji wa Biblia: Mathayo 1-6 Wimbo 91

Sifa ya Usemi: Karibu Kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (be uku. 5 fu.1–uku. 8 fu. 1)

Na. 1: Furahia Neno la Mungu (be uku. 9 fu. 1-5)

Na. 2: Mathayo 4:1-22

Na. 3: Ishara za Siku za Mwisho Zina Uvutano Gani Juu ya Wakristo wa Kweli? (rs-SW uku. 301 fu. 1-2)

Na. 4: Yesu Anafanya Nini Wakati Huu?

Jan. 13 Usomaji wa Biblia: Mathayo 7-11 Wimbo 40

Sifa ya Usemi: Soma Biblia Kila Siku (be uku. 10 fu. 1−uku. 12 fu. 3)

Na. 1: ‘Kimbieni kwa Njia Hiyo’ (w01-SW 1/1 uku. 28-31)

Na. 2: Mathayo 9:9-31

Na. 3: Kwa Nini Tunahubiria Wengine?

Na. 4: Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Husema Kwamba Siku za Mwisho Zilianza Mwaka wa 1914? (rs-SW uku. 302 fu. 1-4)

Jan. 20 Usomaji wa Biblia: Mathayo 12-15 Wimbo 133

Sifa ya Usemi: Kusoma kwa Usahihi (be uku. 83 fu. 1-5)

Na. 1: Unaweza Kukabiliana na Kivunja-Moyo! (w01-SW 2/1 uku. 20-23)

Na. 2: Mathayo 13:1-23

Na. 3: Je! Yeyote Atapata Kuishi Duniani Baada ya Mwisho wa Ulimwengu Uliopo? (rs-SW uku. 303 fu. 1-4)

Na. 4: Je, Mungu Hubadilika?

Jan. 27 Usomaji wa Biblia: Mathayo 16-21 Wimbo 129

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kusoma kwa Usahihi (be uku. 84 fu. 1–uku. 85 fu 3)

Na. 1: Wakati Unapita Haraka Sana (si-SW uku. 278 fu. 1–uku. 279 fu. 6)

Na. 2: w01-SW 1/15 uku. 20 fu. 20–uku. 21 fu. 24

Na. 3: Ni Nini Kitakacholeta Umoja Ulimwenguni?

Na. 4: Kwa Nini Mungu Anaruhusu Wakati Mwingi Sana Upite Kabla ya Kuharibu Waovu? (rs-SW uku. 303 fu. 5–uku. 304 fu. 2)

Feb. 3 Usomaji wa Biblia: Mathayo 22-25 Wimbo 139

Sifa ya Usemi: Kusema kwa Njia Inayoeleweka Wazi (be uku. 86 fu. 1-6)

Na. 1: ‘Kazia Uangalifu Jinsi Unavyosikiliza’ (be uku. 13 fu. 1–uku. 14 fu. 5)

Na. 2: Mathayo 22:15-40

Na. 3: Jinsi Tunavyojua Kwamba Ishara Hutimizwa Katika Wakati Huu Wetu (rs-SW uku. 304 fu. 4–uku. 305 fu. 1)

Na. 4: Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara Ni Nani?

Feb. 10 Usomaji wa Biblia: Mathayo 26-28 Wimbo 27

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kusema kwa Njia Inayoeleweka Wazi (be uku. 87 fu. 1–uku. 88 fu. 3)

Na. 1: Jinsi ya Kupata Furaha ya Kweli (w01-SW 3/1 uku. 4-7)

Na. 2: Mathayo 26:6-30

Na. 3: Kile Kinachofanya Nisitumie Dawa za Kulevya

Na. 4: Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai wa Kibinadamu? (rs-SW uku. 341 fu. 4–uku. 342 fu. 4)

Feb. 17 Usomaji wa Biblia: Marko 1-4 Wimbo 137

Sifa ya Usemi: Matamshi Mazuri—Mambo ya Kufikiria (be uku. 89 fu. 1–uku. 90 fu. 2)

Na. 1: Viishara vya Wakati Vilivyotumiwa Nyakati za Biblia (si-SW uku. 279 fu. 7–uku. 280 fu. 13)

Na. 2: w01-SW 2/15 uku. 25 fu. 10–uku. 26 fu. 14

Na. 3: Je, Wanadamu Waliumbwa Waishi kwa Muda Mfupi Kisha Wafe? (rs-SW uku. 343 fu. 1-3)

Na. 4: Kwa Nini Kucheza Kamari Ni Makosa?

Feb. 24 Usomaji wa Biblia: Marko 5-8 Wimbo 72

Sifa ya Usemi: Njia za Kuboresha Matamshi (be uku. 90 fu. 3–uku. 92)

Kujikumbusha kwa Maneno Tu

Machi 3 Usomaji wa Biblia: Marko 9-12 Wimbo 195

Sifa ya Usemi: Ufasaha (be uku. 93 fu. 1–uku. 94 fu. 3)

Na. 1: Kuwa Msikivu Unaposikiliza Hotuba, Wakati wa Mazungumzo, na Kusanyikoni (be uku. 15 fu. 1–uku. 16 fu. 5)

Na. 2: Marko 10:1-22

Na. 3: Jinsi Tunavyoweza Kupata Nguvu Kutoka kwa Mungu

Na. 4: Tumaini Letu la Kuishi Milele Linategemea Nini? (rs-SW uku. 344 fu. 5-7)

Machi 10 Usomaji wa Biblia: Marko 13-16 Wimbo 187

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuboresha Ufasaha (be uku. 94 fu. 4–uku. 96 fu. 3, bila kutia ndani kisanduku kwenye uku. 95)

Na. 1: Paradiso ya Kiroho Ni Nini? (w01-SW 3/1 uku. 8-11)

Na. 2: Marko 13:1-23

Na. 3: Matazamio kwa Ajili ya Uhai wa Wakati Ujao Yatatimizwaje? (rs-SW uku. 344 fu. 8–uku. 345 fu. 3)

Na. 4: Je, Mungu Anaunga Mkono Upande Fulani Katika Vita ya Wanadamu?

Machi 17 Usomaji wa Biblia: Luka 1-3 Wimbo 13

Sifa ya Usemi: Kukabiliana na Kigugumizi (be uku. 95, kisanduku)

Na. 1: “Heri Mtu Yule Aonaye Hekima” (w01-SW 3/15 uku. 25-28)

Na. 2: Luka 3:1-22

Na. 3: Je, Inafaa Kumwabudu Yesu?

Na. 4: aJe, Ni Jambo la Maana Kufunga Ndoa Kupatana na Matakwa ya Kisheria? (rs-SW uku. 241 fu. 2–uku. 242 fu. 2)

Machi 24 Usomaji wa Biblia: Luka 4-6 Wimbo 156

Sifa ya Usemi: Kutua kwa Kufuata Alama za Vituo na ili Kubadili Mawazo (be uku. 97 fu. 1–uku. 98 fu. 5)

Na. 1: Je, Unahisi Umeeleweka Vibaya? (w01-SW 4/1 uku. 20-23)

Na. 2: Luka 6:1-23

Na. 3: Maana ya Ukumbusho Ni Nini? (rs-SW uku. 353 fu. 1-3)

Na. 4: Je, Wakristo Wanaweza Kutazamia Ulinzi Kutoka kwa Mungu?

Machi 31 Usomaji wa Biblia: Luka 7-9 Wimbo 47

Sifa ya Usemi: Kutua ili Kutia Mkazo, Kutua ili Kusikiliza

(be uku. 99 fu. 1–uku. 100 fu. 4)

Na. 1: “Hofu Mungu wa Kweli na Uzishike Amri Zake” (be uku. 272 fu. 1–uku. 275 fu. 3)

Na. 2: w01-SW 3/15 uku. 18 fu. 17–uku. 19 fu. 20

Na. 3: Jinsi Tunavyojua Kwamba Biblia ni Neno la Mungu

Na. 4: Mkate na Divai Inayotumiwa Kwenye Ukumbusho Ni Mifano ya Nini? (rs-SW uku. 353 fu. 4–uku. 354 fu. 1)

Apr. 7 Usomaji wa Biblia: Luka 10-12 Wimbo 68

Sifa ya Usemi: Kukazia Maana kwa Njia Inayofaa (be uku. 101 fu. 1–uku. 102 fu. 3)

Na. 1: ‘Kutoa Ushahidi Kumhusu Yesu’ (be uku. 275 fu. 4–uku. 278 fu. 4)

Na. 2: Luka 10:1-22

Na. 3: Ni Nani Wanaopaswa Kushiriki Katika Chakula cha Jioni cha Bwana? (rs-SW uku. 354 fu. 3-4)

Na. 4: Watu Wawili wa Kwanza Waliunganishwa Katika Ndoa Jinsi Gani? (rs-SW uku. 242 fu. 3-4)

Apr. 14 Usomaji wa Biblia: Luka 13-17 Wimbo 208

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kukazia Maana Vizuri Zaidi (be uku. 102 fu. 4–uku. 104 fu. 4)

Na. 1: “Habari Njema Hii ya Ufalme” (be uku. 279 fu. 1–uku. 281 fu. 4)

Na. 2: Luka 15:11-32

Na. 3: Jinsi Tunavyoweza Kujilinda Tusipatwe na Uvutano wa Mashetani

Na. 4: Ukumbusho Unapaswa Kuadhimishwa Mara Ngapi, na Wakati Gani? (rs-SW uku. 355 fu. 3–uku. 356 fu. 1)

Apr. 21 Usomaji wa Biblia: Luka 18-21 Wimbo 23

Sifa ya Usemi: Kukazia Mawazo Makuu (be uku. 105 fu. 1–uku. 106 fu. 1)

Na. 1: Majira Ambayo Yehova Amepanga kwa Hekima na Upendo (si-SW uku. 280 fu. 14-17)

Na. 2: w01-SW 4/15 uku. 6 fu. 19–uku. 7 fu. 22

Na. 3: Jinsi Tumaini la Ufufuo Linavyotusaidia Maishani

Na. 4: bJe, Biblia Inakubali Ndoa ya Wake Wengi? (rs-SW uku. 243 fu. 1–uku. 244 fu. 1)

Apr. 28 Usomaji wa Biblia: Luka 22-24 Wimbo 218

Sifa ya Usemi: Kiasi cha Sauti Kinachowafaa Wasikilizaji (be uku. 107 fu. 1–uku. 108 fu. 5)

Kujikumbusha kwa Maneno Tu

Mei 5 Usomaji wa Biblia: Yohana 1-4 Wimbo 31

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuboresha Kiasi cha Sauti (be uku. 108 fu. 6–uku. 110 fu. 2)

Na. 1: Unaweza Kuboresha Kumbukumbu Yako (be uku. 17 fu. 1–uku. 19 fu. 1)

Na. 2: Yohana 2:1-25

Na. 3: Je, Mungu Anakataza Matumizi ya Kileo?

Na. 4: cMaoni ya Mungu Ni Nini Kuhusu Kutengana? (rs-SW uku. 244 fu. 2)

Mei 12 Usomaji wa Biblia: Yohana 5-7 Wimbo 150

Sifa ya Usemi: Ubadilifu wa Sauti—Rekebisha Kiasi cha Sauti (be uku. 111 fu. 1–uku. 112 fu. 2)

Na. 1: Unaweza Kufanikiwa Ijapokuwa Malezi Yako (w01-SW 4/15 uku. 25-28)

Na. 2: Yohana 5:1-24

Na. 3: Kwa Nini Si Jambo la Akili Kuamini Kwamba Mungu Ameamua Kimbele Wale Watakaookoka?

Na. 4: dBiblia Inasema Nini Kuhusu Talaka na Kuoa au Kuolewa Tena? (rs-SW uku. 244 fu. 3–uku. 245 fu. 3)

Mei 19 Usomaji wa Biblia: Yohana 8-11 Wimbo 102

Sifa ya Usemi: Ubadilifu wa Sauti—Badili Mwendo wa Kuzungumza (be uku. 112 fu. 3-6)

Na. 1: ‘Kwa hekima Siku Zetu Zitazidishwa’ (w01-SW 5/15 uku. 28-31)

Na. 2: Yohana 10:16-42

Na. 3: Kwa Nini Mungu Aliruhusu Ndoa Kati ya Ndugu na Dada Hapo Zamani? (rs-SW uku. 245 fu. 4-5)

Na. 4: Jinsi ya Kukabiliana na Mikazo ya Maisha

Mei 26 Usomaji wa Biblia: Yohana 12-16 Wimbo 24

Sifa ya Usemi: Ubadilifu wa Sauti—Kuinua na Kupunguza Sauti (be uku. 113 fu. 1–uku. 114 fu. 2)

Na. 1: Maana ya Mwaka Katika Maandiko Matakatifu (si-SW uku. 280 fu. 18–uku. 282 fu. 23)

Na. 2: w01-SW 5/1 uku. 14 fu. 4–uku. 15 fu. 7

Na. 3: ‘Kutokuwa Sehemu ya Ulimwengu’ Kunamaanisha Nini?

Na. 4: Ni Nini Kinachoweza Kuiboresha Ndoa? (rs-SW uku. 246 fu. 1-4)

Juni 2 Usomaji wa Biblia: Yohana 17-21 Wimbo 198

Sifa ya Usemi: Zungumza kwa Hisia (be uku. 115 fu. 1–uku. 116 fu. 4)

Na. 1: Jinsi Roho ya Mungu Inavyoweza Kutusaidia Kukumbuka (be uku. 19 fu. 2–uku. 20 fu. 3)

Na. 2: Yohana 20:1-23

Na. 3: Ni Nini Kinachoweza Kuiboresha Ndoa? (rs-SW uku. 246 fu. 5-8)

Na. 4: Je, Dini Yenye Kupangwa Kitengenezo Ni ya Lazima?

Juni 9 Usomaji wa Biblia: Matendo 1-4 Wimbo 92

Sifa ya Usemi: Shauku Inayofaa Habari (be uku. 116 fu. 5–uku. 117 fu. 4)

Na. 1: Imarisha Tumaini Lako Katika Yehova (w01-SW 6/1 uku. 7-10)

Na. 2: Matendo 4:1-22

Na. 3: Biblia Inatuambia Nini Kumhusu Mariamu? (rs-SW uku. 172 fu. 1-6)

Na. 4: Je, Mungu Anapendezwa na Jinsi Tunavyoabudu?

Juni 16 Usomaji wa Biblia: Matendo 5-7 Wimbo 2

Sifa ya Usemi: Kuongea kwa Huruma (be uku. 118 fu. 1–uku. 119 fu. 5)

Na. 1: Ungamo Linaloleta Ponyo la Kiroho (w01-SW 6/1 uku. 28-31)

Na. 2: Matendo 7:1-22

Na. 3: Kile Kinachowafanya Mashahidi wa Yehova Wawe Tofauti na Dini Nyingine

Na. 4: Je, Kweli Mariamu Alikuwa Bikira Alipomzaa Yesu? (rs-SW uku. 172 fu. 7–uku. 173 fu. 1)

Juni 23 Usomaji wa Biblia: Matendo 8-10 Wimbo 116

Sifa ya Usemi: Kuongea kwa Hisia (be uku. 119 fu. 6–uku. 120 fu. 4)

Na. 1: Watazame Mayatima na Wajane katika Dhiki Yao (w01-SW 6/15 uku. 9-12)

Na. 2: w01-SW 6/1 uku. 12 fu. 1–uku. 13 fu. 5

Na. 3: Je, Mariamu Alikuwa Bikira Sikuzote? (rs-SW uku. 173 fu. 2–uku. 174 fu. 1)

Na. 4: eKwa Nini Kuhudhuria Mikutano Ni kwa Lazima Ili Kufanya Maendeleo ya Kiroho

Juni 30 Usomaji wa Biblia: Matendo 11-14 Wimbo 167

Sifa ya Usemi: Ishara za Mwili na za Uso Ni Muhimu (be uku. 121 fu. 1-4)

Kujikumbusha kwa Meneno Tu

Julai 7 Usomaji wa Biblia: Matendo 15-17 Wimbo 38

Sifa ya Usemi: Kutumia Ishara za Mwili na za Uso (be uku. 122 fu. 1–uku. 123 fu. 2)

Na. 1: Jitahidi Uwe Msomaji Mzuri (be uku. 21 fu. 1–uku. 23 fu. 3)

Na. 2: Matendo 15:1-21

Na. 3: Jinsi Tunavyounga Mkono Enzi Kuu ya Yehova

Na. 4: Je, Mariamu Alikuwa Mama ya Mungu? (rs-SW uku. 174 fu. 2-4)

Julai 14 Usomaji wa Biblia: Matendo 18-21 Wimbo 32

Sifa ya Usemi: Kuwatazama Wasikilizaji Katika Huduma (be uku. 124 fu. 1–uku. 125 fu. 4)

Na. 1: Usiruhusu Imani Yako Iharibiwe na Shaka (w01-SW 7/1 uku. 18-21)

Na. 2: Matendo 19:1-22

Na. 3: fJe, Mariamu Alikingiwa Dhambi ya Asili Mama Yake Alipopata Mimba? (rs-SW uku. 175 fu. 1-2)

Na. 4: ‘Kuendelea Kutafuta Ufalme Kwanza’ Kunamaanisha Nini?

Julai 21 Usomaji wa Biblia: Matendo 22-25 Wimbo 222

Sifa ya Usemi: Kuwatazama Wasikilizaji Unapotoa Hotuba

(be uku. 125 fu. 5–uku. 127 fu. 1)

Na. 1: Je, Wewe Ni Mvumilivu Kweli? (w01-SW 7/15 uku. 21-23)

Na. 2: Matendo 24:1-23

Na. 3: Je, Ibilisi Ni Kiumbe Halisi?

Na. 4: gJe, Mariamu Alipaa Mbinguni Akiwa na Mwili wa Binadamu? (rs-SW uku. 175 fu. 3–uku. 176 fu. 1)

Julai 28 Usomaji wa Biblia: Matendo 26-28 Wimbo 14

Sifa ya Usemi: Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida Katika Huduma ya Shambani (be uku. 128 fu. 1–uku. 129 fu. 1)

Na. 1: Hakuna Mwaka Sifuri (si-SW uku. 282 fu. 24-26)

Na. 2: w01-SW 7/1 uku. 14 fu. 5-8

Na. 3: Je, Inafaa Kusali kwa Mariamu Akiwa Mwombezi? (rs-SW uku. 176 fu. 2-4)

Na. 4: Jinsi Tunavyoonyesha Kwamba Tunaheshimu Zawadi ya Uhai

Ago. 4 Usomaji wa Biblia: Waroma 1-4 Wimbo 106

Sifa ya Usemi: Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida Jukwaani (be uku. 129 fu. 2-5)

Na. 1: Jinsi ya Kujizoeza Kuwa Msomaji Mzuri (be uku. 23 fu. 4–uku. 26 fu. 5)

Na. 2: Waroma 2:1-24

Na. 3: Je, Umepata Kuishi Ukiwa na Umbo Jingine?

Na. 4: Je, Mariamu Aliheshimiwa kwa Njia ya Pekee Katika Kutaniko la Kikristo la Karne ya Kwanza? (rs-SW uku. 177 fu. 2–uku. 178 fu. 1)

Ago. 11 Usomaji wa Biblia: Waroma 5-8 Wimbo 179

Sifa ya Usemi: Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida Mbele ya Watu (be uku. 130 fu. 1-3)

Na. 1: ‘Baraka kwa Waadilifu’ (w01-SW 7/15 uku. 24-27)

Na. 2: Waroma 5:6-21

Na. 3: hJe, Ninyi Mnamwamini Bikira Mariamu? (rs-SW uku. 178 fu. 2-4)

Na. 4: Je, Unaamini Kwamba Watu Huzaliwa Upya Katika Umbo Jingine?

Ago. 18 Usomaji wa Biblia: Waroma 9-12 Wimbo 206

Sifa ya Usemi: Sura Safi Hufanya Ujumbe Uvutie Zaidi (be uku. 131 fu. 1-3)

Na. 1: Acha Mazoea Yakunufaishe (w01-SW 8/1 uku. 19-22)

Na. 2: w01-SW 8/15 uku. 21 fu. 10–uku. 22 fu. 13

Na. 3: Je, Wanadamu Wameibadili Biblia?

Na. 4: Je, Mkate na Divai Hubadilika Kuwa Mwili na Damu Halisi ya Kristo? (rs-SW uku. 201 fu. 1–uku. 202 fu. 3)

Ago. 25 Usomaji wa Biblia: Waroma 13-16 Wimbo 43

Sifa ya Usemi: Jinsi Kiasi na Utimamu wa Akili Zinavyotusaidia kwa Habari ya Mavazi na Mapambo (be uku. 131 fu. 4–uku. 132 fu. 3)

Kujikumbusha kwa Maneno Tu

Sept. 1 Usomaji wa Biblia: 1 Wakorintho 1-9 Wimbo 48

Sifa ya Usemi: Umuhimu wa Mavazi Yanayofaa (be uku. 132 fu. 4–uku. 133 fu. 1)

Na. 1: Jinsi ya Kujifunza (be uku. 27 fu. 1−uku. 31 fu. 2)

Na. 2: 1 Wakorintho 3:1-23

Na. 3: Ni Nini Maana ya Yohana 6:53-57? (rs-SW uku. 202 fu. 4–uku. 203 fu. 1)

Na. 4: Je, Umaskini Unampa Mtu Sababu ya Kuiba?

Sept. 8 Usomaji wa Biblia: 1 Wakorintho 10-16 Wimbo 123

Sifa ya Usemi: Tukiwa Nadhifu Hatutakwaza Mtu Yeyote (be uku. 133 fu. 2-4)

Na. 1: Shinda Vikwazo Vinavyokuzuia Usifanye Maendeleo! (w01-SW 8/1 uku. 28-30)

Na. 2: 1 Wakorintho 12:1-26

Na. 3: Kwa Nini Mungu Anaruhusu Mambo Mabaya Yatukie?

Na. 4: Je, Yesu Alianzisha Misa? (rs-SW uku. 203 fu. 2–uku. 205 fu. 2)

Sept. 15 Usomaji wa Biblia: 2 Wakorintho 1-7 Wimbo 16

Sifa ya Usemi: Jinsi Unavyosimama na Vifaa Nadhifu (be uku. 133 fu. 5–uku. 134 fu. 4)

Na. 1: Jinsi ya Kufanikisha Ujana Wako (w01-SW 8/15 uku. 4-7)

Na. 2: 2 Wakorintho 6:1–7:1

Na. 3: Maoni ya Mkristo Kuhusu Mamlaka ya Ulimwengu (rs-SW uku. 138 fu. 3–uku. 139 fu. 2)

Na. 4: Mungu Anaonaje Uchafuzi wa Mazingira?

Sept. 22 Usomaji wa Biblia: 2 Wakorintho 8-13 Wimbo 207

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kupunguza Wasiwasi Unapotoa Hotuba (be uku. 135 fu. 1–uku. 137 fu. 2)

Na. 1: Jinsi Unavyoweza Kufanya Maamuzi ya Hekima (w01-SW 9/1 uku. 27-30)

Na. 2: 2 Wakorintho 8:1-21

Na. 3: Nafsi Inakwenda Wapi Baada ya Kifo?

Na. 4: Maandiko Yanayohusisha Maoni ya Mkristo Juu ya Vita (rs-SW uku. 139 fu. 3–uku. 140 fu. 2)

Sept. 29 Usomaji wa Biblia: Wagalatia 1-6 Wimbo 163

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuwa Mtulivu (be uku. 137 fu. 3–uku. 138 fu. 5)

Na. 1: Kwa Nini Tarehe za Msingi Ni za Maana Sana? (si-SW uku. 282 fu. 27–uku. 283 fu. 30)

Na. 2: w01-SW 9/1 uku. 15 fu. 8–uku. 17 fu. 11

Na. 3: Kwa Nini Yehova Aliwaruhusu Waisraeli Kwenda Vitani? (rs-SW uku. 140 fu. 3-4)

Na. 4: Jinsi Tunavyojua Kwamba Ufalme wa Mungu Unatawala Sasa

Okt. 6 Usomaji wa Biblia: Waefeso 1-6 Wimbo 99

Sifa ya Usemi: Umuhimu wa Kikuza-Sauti (be uku. 139 fu. 1–uku. 140 fu. 1)

Na. 1: Funzo Lina Faida (be uku. 31 fu. 3–uku. 32 fu. 3)

Na. 2: Waefeso 2:1-22

Na. 3: Kumwamini Mungu Ni Jambo la Akili

Na. 4: Maoni ya Mkristo Kuhusu Kutojihusisha Katika Masuala ya Kisiasa Hutegemea Maandiko Gani? (rs-SW uku. 142 fu. 1-5)

Okt. 13 Usomaji wa Biblia: Wafilipi 1–Wakolosai 4 Wimbo 105

Sifa ya Usemi: Tumia Kikuza-Sauti kwa Njia Inayofaa (be uku. 140 fu. 2–uku. 142 fu. 1)

Na. 1: Tembea Katika ‘Njia ya Unyofu’ (w01-SW 9/15 uku. 24-28)

Na. 2: Wafilipi 2:1-24

Na. 3: Maoni ya Mkristo Kuhusu Sherehe za Kizalendo Hutegemea Maandiko Gani? (rs-SW uku. 143 fu. 1–uku. 144 fu. 2)

Na. 4: Kile Ambacho Yehova Anataka Tufanye Leo

Okt. 20 Usomaji wa Biblia: 1 Wathesalonike 1–2 Wathesalonike 3 Wimbo 145

Sifa ya Usemi: Kutumia Biblia Kujibu Maswali (be uku. 143 fu. 1-3)

Na. 1: Maoni ya Yehova Kuhusu Wakati (si-SW uku. 283 fu. 31–uku. 284 fu. 33)

Na. 2: w01-SW 10/15 uku. 23 fu. 6–uku. 24 fu. 9

Na. 3: Ni Nani Watakaokwenda Mbinguni?

Na. 4: Je, Wakristo Hukataa Kuunga Mkono Vita na Siasa kwa Sababu Hawajali Majirani Wao? (rs-SW uku. 144 fu. 3)

Okt. 27 Usomaji wa Biblia: 1 Timotheo 1–2 Timotheo 4 Wimbo 46

Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kutumia Biblia Vizuri Zaidi (be uku. 144 fu. 1-4)

Kujikumbusha kwa Maneno Tu

Nov. 3 Usomaji wa Biblia: Tito 1–Filemoni Wimbo 30

Sifa ya Usemi: Kuwatia Wasikilizaji Moyo Kutumia Biblia (be uku. 145-146)

Na. 1: Jinsi ya Kufanya Utafiti (be uku. 33 fu. 1–uku. 35 fu. 2)

Na. 2: Filemoni 1-25

Na. 3: Je, Maisha Katika Hali Kamilifu Yatakuwa ya Kuchosha?

Na. 4: Kwa Nini Jina la Yehova Limetumiwa Katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo Katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya? (rs-SW uku. 250 fu. 3–uku. 251 fu. 1)

Nov. 10 Usomaji wa Biblia: Waebrania 1-8 Wimbo 149

Sifa ya Usemi: Kutoa Utangulizi Mzuri wa Maandiko Ni Muhimu (be uku. 147 fu. 1–uku. 148 fu. 2)

Na. 1: Enoki Alitembea Pamoja na Mungu Katika Ulimwengu Wenye Dhambi (w01-SW 9/15 uku. 29-31)

Na. 2: Waebrania 2:1-18

Na. 3: iJinsi ya Kujibu Mtu Anayesema, ‘Ninyi Mna Biblia Yenu Wenyewe’ (rs-SW uku. 251 fu. 3–uku. 252 fu. 2)

Na. 4: Watakaofufuliwa Watahukumiwa Kufuatana na Matendo Gani?

Nov. 17 Usomaji wa Biblia: Waebrania 9-13 Wimbo 144

Sifa ya Usemi: Kuchagua Maelezo Yanayofaa Kutoa Utangulizi wa Maandiko (be uku. 148 fu. 3–uku. 149 fu. 3)

Na. 1: Inamaanisha Nini Kuwa Mwaminifu-Mshikamanifu? (w01-SW 10/1 uku. 20-23)

Na. 2: Waebrania 9:11-28

Na. 3: Je, Viumbe wa Mungu wa Mbinguni Wamepangwa Kitengenezo? (rs-SW uku. 311 fu. 3-4)

Na. 4: Mwenendo Unaomheshimu Mungu Una Faida Kubwa

Nov. 24 Usomaji wa Biblia: Yakobo 1-5 Wimbo 88

Sifa ya Usemi: Mkazo Unaofaa Unatia Ndani Kusoma kwa Hisia (be uku. 150 fu. 1-2)

Na. 1: Kupima Matukio Katika Mkondo wa Wakati (si-SW uku. 284 fu. 1-4)

Na. 2: w01-SW 11/1 uku. 12 fu 15–uku. 13 fu. 19

Na. 3: Sifa ya Kiasi Ni ya Maana Sana

Na. 4: Mungu Alitumia Njia Gani Ili Kuwapa Maagizo Watumishi Wake wa Kale Waliokuwa Duniani (rs-SW uku. 312 fu. 1-2)

Des. 1 Usomaji wa Biblia: 1 Petro 1–2 Petro 3 Wimbo 54

Sifa ya Usemi: Kazia Maneno Yanayofaa (be uku. 150 fu. 3–uku. 151 fu. 2)

Na. 1: Kujifunza Kutumia Vifaa Vingine vya Utafiti (be uku. 35 fu. 3–uku. 38 fu. 4)

Na. 2: 1 Petro 1:1-16

Na. 3: Je, Biblia Inaonyesha Kwamba Wakristo wa Kweli Wangepangwa Kitengenezo? (rs-SW uku. 313 fu. 1-4)

Na. 4: Dhabihu ya Ukombozi ya Kristo Inapaswa Kuwa na Matokeo Gani Maishani Mwetu?

Des. 8 Usomaji wa Biblia: 1 Yohana 1–Yuda Wimbo 22

Sifa ya Usemi: Njia za Kutia Mkazo (be uku. 151 fu. 3–uku. 152 fu. 5)

Na. 1: Linda Dhamiri Yako (w01-SW 11/1 uku. 4-7)

Na. 2: 1 Yohana 3:1-18

Na. 3: Biblia Haiungi Mkono Kuwatendea Wanawake Bila Heshima

Na. 4: Je, Watumishi Waaminifu wa Mungu Wametawanyika Katika Makanisa Mbalimbali Yanayodai Kuwa ya Kikristo (rs-SW uku. 314 fu. 1-3)

Des. 15 Usomaji wa Biblia: Ufunuo 1-6 Wimbo 219

Sifa ya Usemi: Kutumia Maandiko Vizuri (be uku. 153 fu. 1–uku. 154 fu. 3)

Na. 1: Noa Auhukumu Ulimwengu kwa Imani Yake (w01-SW 11/15 uku. 28-31)

Na. 2: Ufunuo 2:1-17

Na. 3: Sehemu Inayoonekana ya Tengenezo la Yehova Inaweza Kutambuliwa Jinsi Gani? (rs-SW uku. 314 fu. 4–uku. 315 fu. 2)

Na. 4: Kwa Nini Wakristo Hawasherehekei Krismasi?

Des. 22 Usomaji wa Biblia: Ufunuo 7-14 Wimbo 6

Sifa ya Usemi: Onyesha Vizuri Jinsi Andiko Linavyohusika

(be uku. 154 fu. 4–uku. 155 fu. 4)

Na. 1: Unaweza Kuepuka Ugonjwa wa Moyo wa Mfano (w01-SW 12/1 uku. 9-13)

Na. 2: w01-SW 12/15 uku. 17 fu. 10–uku. 18 fu. 13 (kutia ndani kielezi-chini)

Na. 3: Unaweza Kushinda Vishawishi vya Wenzako

Na. 4: Tunaweza Kuonyesha Heshima kwa Tengenezo la Yehova Jinsi Gani? (rs-SW uku. 315 fu. 3-7)

Des. 29 Usomaji wa Biblia: Ufunuo 15-22 Wimbo 60

Sifa ya Usemi: Tumia Maandiko Kutoa Sababu (be uku. 155 fu. 5–uku. 156 fu. 5)

Kujikumbusha kwa Maneno Tu

[Maelezo ya chini]

a Toa mgawo huu kwa akina ndugu tu.

b Toa mgawo huu kwa akina ndugu tu.

c Toa mgawo huu kwa akina ndugu tu.

d Toa mgawo huu kwa akina ndugu tu.

e Toa mgawo huu kwa akina ndugu tu.

f Ikiwa wakati unaruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.

g Ikiwa wakati unaruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.

h Ikiwa wakati unaruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.

i Ikiwa wakati unaruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine