Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Novemba 1-14: Kampeni ya pekee ya kugawa broshua Endeleeni Kukesha! Novemba 15-30: Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Ikiwa watu wanasema kwamba hawana watoto, watoleeni broshua Anataka. Mnapotumia broshua hiyo kazeni fikira juu ya kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu mwingine atakayechaguliwa naye anapaswa kufanya uchunguzi wa akaunti za kutaniko mnamo Desemba 1 au mapema zaidi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Ikiwa kuna hazina kwa ajili ya ujenzi au utunzaji wa Jumba la Ufalme, mipango itachukuliwa pia ili kufanya uchunguzi wa akaunti hiyo. Jambo hilo litakapokuwa limefanywa, toeni tangazo kwa kutaniko baada ya kusoma ripoti ya akaunti ya kawaida.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuomba mabuku ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ya 2004 kwenye maombi yayo ya vichapo yajayo. Orodha ya lugha ambazo katika hizo mabuku hayo yanapatikana itatokea katika “Tangazo kwa Makutaniko Yote,” linalotumwa katika barua kwa makutaniko yote kila mwezi. Mpaka mabuku hayo yatakapopatikana na usafirishaji kufanywa, hayo yatakuwa na maandishi “Noté pour plus tard” (au “Pending”) kwenye orodha za usafirishaji za kutaniko. Mabuku ni vitabu vinavyofanyiwa ombi la pekee.
◼ Kuanzia juma la Mei 23, 2005, tutajifunza broshua Endeleeni Kukesha! kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko.
◼ Ni jambo la lazima kwa Sosaiti kuendelea kuwa na maandishi ya kisasa kuhusu anwani na namba za simu za waangalizi wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kuna badiliko wakati wowote, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko inapaswa kujaza na kutuma fomu Changement d’adresse du surveillant-président/secrétaire (S-29-F) kwenye ofisi ya tawi bila kukawia. Hiyo inatia ndani mabadiliko yoyote kuhusu namba za simu na za miito (code).
◼ Siku ya Posho Novemba 27, 2004, familia ya Betheli itakuwa na shughuli za kipekee na Siku ya Posho Desemba 4, 2004, kutakuwa na usafishaji wa Betheli kwa ujumla. Kwa hiyo, tafadhali msipange kutembelea Ofisi la Tawi au washiriki wa Betheli siku hizo mbili.