Programu ya Mikutano ya Utumishi
Juma Toka Novemba 8
Wimbo 180
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Kampeni ya pekee ya kugawa broshua Endeleeni Kukesha! itamalizika Novemba 14. Baada ya tarehe hiyo mpaka mwisho wa mwezi wa Novemba, tutatolea watu kitabu Jifunze Kukoka kwa Mwalimu Mkuu. Rudilieni kwa kifupi utoaji mbalimbali uliopendekezwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 2004, ukurasa wa 3.
Dak. 15: Faidika Kikamili na Mkutano wa Utumishi. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 71-72. Ni katika sehemu gani tano ambazo Mkutano wa Utumishi unatusaidia kufanya maendeleo tukiwa wahudumu Wakristo? Taja mifano kutoka programu ya mwezi huu. Ni faida gani zinazotokana na kutayarisha kimbele? Kwa nini kuhudhuria kwa ukawaida? Mkutano huo una msingi gani wa Kimaandiko?
Dak. 20: “Kutambua Umaana wa Kutenda kwa Haraka!”* Tia ndani maelezo kutoka Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 2000, ukurasa wa 12-13.
Wimbo 19 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Novemba 15
Wimbo 170
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ikiwa mapendekezo kwenye ukurasa wa 4 ni yenye kufaa eneo la kutaniko lenu, yatumieni ili kuonyesha jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa Novemba 15 na Amkeni! ya Novemba 22. Utoaji mwingine mbalimbali wenye kufaa unaweza kutumiwa.
Dak. 15: Je, Unajua Furaha Inayotokana na Kutoa? Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1, 2004, ukurasa wa 19-23.
Dak. 20: Sitawisha Kupendezwa Unapotumia ile Broshua Mpya. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Itatolewa na mwangalizi wa utumishi. Tunapaswa kufanya ziara za kurudia ili kusitawisha kupendezwa kwa kila mtu aliyekubali nakala ya broshua Endeleeni Kukesha! Ukitumia yaliyomo kwenye ukurasa wa 2, toa kwa kifupi mwono wa jumla wa broshua, ukivuta uangalifu kwenye sehemu kuu fupi (sehemu hizo zinaorodheshwa katika maandishi ya kawaida chini ya vichwa vinavyochapwa kwa herufi nzito nyeusi). Habari hiyo inaweza kutumiwa kwa ajili ya mazungumzo mafupi na yenye kuelimisha yakitegemea habari iliyozungumziwa mbele. Kwa mfano, ikiwa ukurasa wa 3-4 ulikaziwa kwenye ziara ya kwanza, sehemu kubwa “Je, Kweli Mungu Anajali?” kwenye ukurasa wa 5 inaweza kutumiwa ili kufanya ziara ya kurudia. Eleza jinsi hilo linavyoweza kufanywa. Rudilia sehemu nyingine kubwa, kama vile zile zinazopatikana kwenye ukurasa wa 6-8 na 17-18 au sehemu nyingine zinazofaa eneo lenu. Fanyeni onyesho la ziara ya kurudia, mkitumia moja ya sehemu kubwa. Andiko moja au zaidi kati ya yale yanayotajwa yanapaswa kusomwa na kuzungumziwa. Mhubiri anamalizia kwa kuvuta uangalifu kwenye sehemu kubwa ingine inayoweza kuzungumziwa kwenye ziara ijayo.
Wimbo 66 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Novemba 22
Wimbo 199
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 20: Kuanza Mafunzo ya Biblia na Wale Waliokubali ile Broshua Mpya. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Itatolewa na mwangalizi wa utumishi. Rudilieni kwa kifupi ziara ya kurudia iliyoonyeshwa kwenye Mkutano wa Utumishi uliopita, mkitaja hasa sehemu kubwa iliyotajwa mwishoni mwa ziara hiyo. Omba wahubiri walewale (ikiwezekana) watumie habari ile ili kufanya onyesho la ziara ya kurudia lijalo. Kisha mhubiri anatumia jalada ya broshua hiyo ili kupendekeza funzo la Biblia, na mipango inafanywa ili kuchunguza somo la 1 la broshua Anataka kwenye ziara ijayo. Tia wote moyo kukaza uangalifu juu ya kuanzisha mafunzo ya Biblia pamoja na wale waliokubali nakala ya broshua Endeleeni Kukesha!
Wimbo 58 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Novemba 29
Wimbo 23
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote watoe ripoti za utumishi wa shambani za Novemba. Fanyeni maonyesho kuhusu jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1 na Amkeni! ya Desemba 8
Dak. 10: Kisanduku cha Maulizo. Hotuba itakayotolewa na mzee.
Dak. 25: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu 3.”* Tumia maulizo yaliyotolewa. Baada ya kuzungumzia fungu la 3, tieni ndani onyesho fupi la funzo la Biblia katika broshua Anataka, somo la 5, fungu la 1. Fungu limekwisha kusomwa na ulizo kujibiwa. Kiongozi na mwanafunzi wanasoma na kuzungumzia Isaya 45:18 na Mhubiri 1:4. Kiongozi anatumia maulizo rahisi ili kuchochea mwanafunzi kueleza jinsi kila andiko linavyohusiana na mambo mnayochunguza.
Wimbo 178 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Desemba 6
Wimbo 96
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Sema kuhusu toleo la vichapo la Desemba. Fanyeni onyesho moja au mawili kuhusu yale tunayoweza kufanya tunapotolea watu kitabu Mtu Mkuu Zaidi.
Dak. 20: “Je, Unaweza Kusaidia?”* Hoji mhubiri mmoja au wawili waliothamini msaada au kitia moyo kilichotolewa na wengine.
Dak. 15: Mambo yaliyoonwa ya kwenu. Omba wasikilizaji wasimulie mambo yaliyoonwa waliyofurahia waliporudilia wale ambao walikubali broshua Endeleeni Kukesha! Pangeni kimbele kucheza upya mambo yaliyoonwa yenye kutokeza. Pongeza wote kwa tegemezo lao kwa kampeni hii ya pekee.
Wimbo 101 na sala ya kumalizia.
* Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.