Programu ya Mikutano ya Utumishi
Juma Toka Mei 9
Wimbo 217
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa eneo lenu) ili kuonyesha jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa Mei 15 na Amkeni! ya Mei 22. Utoaji mwengine unaofaa kulingana na hali unaweza kutumiwa. Katika utoaji mmoja, onyesha jinsi ya kutoa magazeti kivivi hivi katika magari ya kusafirishia watu wote.
Dak. 15: Tumia Neno la Mungu Ili Kugusa Moyo. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi wa Februari 1, 2005, ukurasa wa 28-31. Zungumzia jinsi Yesu alivyotumia Maandiko ili kumsaidia Petro. Zungumzia jinsi tunavyoweza kufuata mfano wa Yesu wakati ambapo kuna uhitaji wa kurekebisha fikira na hisia za watoto wetu, wanafunzi wetu wa Biblia, na hata sisi wenyewe.
Dak. 20: “Fanyeni Programu ya Familia Yenye Kufaa.” Katika hotuba ya utangulizi isiyofikia dakika mbili, kazia thamani ya programu iliyoandikwa na zungumzia jinsi ya kujaza programu iliyo wazi kwenye ukurasa wa 6. Uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu ya makala “Programu ya Familia—Mikutano ya Kutaniko.” Omba wasikilizaji watoe maelezo juu ya jinsi wanavyozuia shughuli nyingine zisiingilie mikutano ya kutaniko. Sehemu nyingine za programu ya familia zitachunguzwa katika majuma yenye kufuata.
Wimbo 176 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Mei 16
Wimbo 201
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu.
Dak. 15: “Programu ya Familia—Utumishi wa Shambani Pamoja na Familia.”* Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu faida za kutumika pamoja kwa ukawaida katika huduma wakiwa familia.
Dak. 20: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu 9.”* Mnapozungumzia fungu la 2, kazia jambo moja au mawili kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Desemba 2004, ukurasa wa 8. Tia ndani onyesho fupi la funzo la Biblia. Baada ya kumaliza somo la 2 katika broshua Anataka, kiongozi wa funzo anauliza mwanafunzi: “Namna gani utamwelezea rafiki jina la Mungu ni nani?” Mwanafunzi anaeleza jinsi atakavyotumia Zaburi 83:18, baada ya hilo kiongozi wa funzo anampongeza.
Wimbo 134 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Mei 23
Wimbo 194
Dak. 12: Matangazo ya kutaniko lenu. Soma ripoti ya akaunti na ya shukrani kuhusu zawadi. Tumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (ikiwa yanafaa eneo lenu) ili kuonyesha jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa Juni 1 na Amkeni! ya Juni 8. Utoaji mwengine unaofaa kulingana na hali unaweza kutumiwa.
Dak. 18: “Siku ya Yehova Iko Karibu.”* Unapotayarisha sehemu hii, chunguza kitabu Unabii wa Danieli, ukurasa wa 59, fungu 28.
Dak. 15: “Programu ya Familia—Funzo la Familia.”* Fanya mipango kimbele ili mtu mmoja au wawili waeleze jinsi wanavyopanga programu ya funzo lao la familia na jitihada inayohitajiwa ili kufanya funzo kwa ukawaida.
Wimbo 152 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Mei 30
Wimbo 190
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Mei. Onyesha toleo la mwezi wa Juni. Fanyeni onyesho la jinsi ya kutolea watu vichapo, ukitumia utoaji moja au mbili uliopendekezwa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005 (ikiwa utoaji huo unafaa eneo lenu). Utoaji mwingine unaofaa unaweza kutumiwa.
Dak. 20: “Programu ya Familia—Andiko la Siku.”* Omba wasikilizaji waeleze jinsi familia yao inafaidika na uchunguzi wa andiko la siku pamoja, na waeleze programu wanayoona kuwa yenye kufaa kwa uchunguzi wa andiko la siku.
Dak. 15: Simulieni au chezeni upya mambo yaliyoonwa katika utumishi wa shambani mnamo Machi, Aprili, na Mei. Fanya mipango kimbele ili mtu mmoja au wawili watoe maelezo kuhusu jitihada waliyofanya ili kuongeza ushiriki wao katika huduma mnamo majira ya Ukumbusho na baraka walizopata kama matokeo.
Wimbo 115 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Juni 6
Wimbo 155
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu.
Dak. 15: Mwe Waangalifu na Desturi Zisizompendeza Mungu. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yatakayoongozwa na mzee na yanayotegemea Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 2005, ukurasa 27-30.
Dak. 20: “Sitawisha Kupendezwa kwa Watu Unaowaachia Magazeti kwa Ukawaida.”* Mnapozungumzia fungu la 3, vuta uangalifu kwenye kitabu Kutoa Sababu, ukurasa 327-332. Habari hiyo inaweza kutumiwa ili kutayarisha mfululizo wa mazungumzo yenye kukazia andiko moja juu ya yale ambayo Ufalme wa Mungu utatimiza. Tia ndani onyesho linalohusu jinsi mhubiri anavyoweza kuwa na mazungumzo pamoja na mtu anayeachia magazeti kwa ukawaida, mazungumzo yenye kukazia andiko moja. Mhubiri anapaswa kuzungumza kwa kifupi na kutoa mfano juu ya jinsi ya kufanya matumizi ya andiko ili kusaidia mwenye nyumba kulielewa kwa usahihi na kuona thamani yalo katika maisha yake.
Wimbo 107 na sala ya kumalizia.
* Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.