Programu ya Mikutano ya Utumishi
Juma Tokea Tarehe 11/06
Wimbo 153
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Mkitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au utoaji mwingine mbalimbali wenye kufaa eneo lenu, fanyeni onyesho la jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15/06 na Amkeni! ya mwezi wa 6.
Dak. 15: Tumetayarishwa Vizuri Kuwa Walimu wa Neno la Mungu. Hotuba yenye kuchukuliwa katika Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15 mwezi wa 2, 2002, ukurasa wa 24-28. Wakristo wengine wanasita kupendekeza kujifunza Biblia na watu wenye kuonyesha kupendezwa kwa kuwa wanajiona kuwa hawastahili kuongoza funzo. Lakini, kupitia Neno lake, roho yake takatifu, na tengenezo lake, Yehova anatutayarisha kuwa watumishi. Mradi wetu si kutolea tu watu vitabu. Tunapaswa kujikaza kufundisha watu. (Mt. 28:19, 20) Tia moyo wahubiri wakusudie kuanzisha mafunzo ya Biblia.
Dak. 20: Fanyeni Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yenye kuchukuliwa katika kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, sura ya 13.
Wimbo 144 na sala ya kumalizia.
Juma Tokea Tarehe 18/06
Wimbo 217
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 15: Je, Unakumbuka? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yenye kuchukuliwa katika Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15 mwezi wa 4, 2007, ukurasa wa 19.
Dak. 20: “Sisi Ni Wenye Furaha Kujitoa Katika Utumishi wa Yehova!”* Ikiwa kuna wakati, omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yanayotajwa.
Wimbo 82 na sala ya kumalizia.
Juma Tokea Tarehe 25/06
Wimbo 15
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Soma ripoti ya feza na shukrani kuhusu michango. Mkitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au utoaji mwingine mbalimbali wenye kufaa eneo lenu, fanyeni onyesho la jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/07 na Amkeni! ya mwezi wa 7.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko lenu.
Dak. 20: “Je, Unaweza Kuingia Katika ‘Mlango Mkubwa Unaoongoza Kwenye Utendaji’?”* Uliza painia wa kawaida mmoja au wawili maulizo machache. Ni mabadiliko gani waliyofanya ili wawe mapainia wa kawaida? Ni faida gani ambayo wamepata?
Wimbo 138 na sala ya kumalizia.
Juma Tokea Tarehe 2/07
Wimbo 208
Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za mahubiri za mwezi wa 6. Taja kitabu tutakachotolea watu katika mwezi wa 7, na fanyeni onyesho moja.
Dak. 15: Kuhubiria Watu Hata Ikiwa Hatukupanga Kufanya Hivyo, Ni Njia ya Maana ya Kutangaza Habari Njema. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yenye kuchukuliwa katika kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 101-102. Toa mapendekezo fulani yenye kufaa kuhusu jinsi ya kuhubiria watu hata ikiwa hatukupanga kufanya hivyo. Omba wasikilizaji wazungumzie mambo waliyoona yenye kutia moyo walipokuwa wakihubiria watu hata ikiwa hawakupanga kufanya hivyo.
Dak. 20: “Endeleeni ‘Kuzaa Matunda Mengi.’”* Mnapozungumzia fungu la 4, tia ndani maelezo ya kisanduku “Jinsi ya ‘Kuzaa Matunda kwa Uvumilivu,’” katika Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 2, 2003, ukurasa wa 21.
Wimbo 69 na sala ya kumalizia.
* Maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.