Matangazo
◼ Toleo la vitabu la mwezi wa 8: Mnaweza kutumia broshua yoyote ya kurasa 32, kama inavyoonyeshwa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 5, 2007. Mwezi wa 9: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mjikaze sana kuanzisha mafunzo ya Biblia mnapohubiria watu kwa mara ya kwanza. Ikiwa wasikilizaji wamekwisha kuwa na kitabu hicho, muwaonyeshe kwa kifupi jinsi funzo la Biblia linavyofanywa ili wafaidike nacho. Mwezi wa 10: Tutatolea watu magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo watu wanaonyesha kupendezwa, muwatolee na kuzungumzia trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? mkiwa na kusudi la kuanzisha funzo la Biblia. Mwezi wa 11: Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Ikiwa watu wanasema kwamba hawana watoto, muwatolee broshua Endeleeni Kukesha!
◼ Kwa kuwa mwezi wa 9 una Siku za Posho tano na Siku za Yenga, huo utakuwa mwezi mzuri sana ili kufanya kazi ya upainia msaidizi.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuomba Kalenda ya Mashahidi wa Yehova ya 2008, Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2008 na Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2008 katika ombi lao la vitabu watakalofanya karibuni. Luga zote ambamo vitabu hivyo vinapatikana zitaonyeshwa katika “Tangazo kwa Makutaniko Yote,” linalotumwa katika barua kwa makutaniko yote kila mwezi.
◼ Wazee wanakumbushwa kufuata maagizo yanayotolewa katika Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15/04/91, ukurasa wa 21-23 kuhusu wale wote waliotengwa na ushirika wa kutaniko au waliojitenga wenyewe, ambao labda wana nia ya kurudishwa.