Kujikumbusha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maulizo ya kujikumbusha yanayofuata yatatumiwa kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi mnamo juma tokea tarehe 27 mwezi wa 8, 2007. Kwa dakika 30, mwangalizi wa Shule ataongoza kujikumbusha kunakotegemea habari zilizozungumziwa katika migawo ya majuma ya tarehe 2 mwezi wa 7 mpaka tarehe 27 mwezi wa 8, 2007.
SIFA ZA USEMI
1. Namna gani tunaweza kuonyesha wengine heshima katika kazi yetu ya kuhubiri na katika kutaniko? [be uku. 192 fu. 2-4]
2. Ni mambo gani yaliyo ya lazima ili kuonyesha kwamba tunasadiki yale tunayosema? [be uku. 196 fu. 1-3]
3. Ni mapendekezo gani ambayo yatatusaidia kuhubiria wengine kwa kutumia akili nzuri? [be uku. 198 fu. 1-5]
4. Tunapohubiria wengine, jinsi gani kutumia akili nzuri kunatusaidia kujua wakati unaofaa wa kusema? (Met. 25:11) [be uku. 199 fu. 1-3]
5. Namna gani tunaweza kutoa hotuba zetu kwa njia yenye kutia moyo? [be uku. 203 fu.3–uku. 204 fu. 1]
MGAWO Na. 1
6. Tunaweza kusema nini kuhusu uandikaji wa Ezekieli na kuhusu kukubalika na ukweli wa kitabu cha Ezekieli? [si uku. 133 fu. 3]
7. Ni sifa gani iliyo ya maana ili mtu avumilie ukosefu wa haki? [w05 6/1 uku. 29 fu. 4]
8. Tunajifunza nini kutokana na jibu ambalo Yesu alitolea Masadukayo kuhusu ufufuo? (Luka 20:37, 38) [be uku. 66 fu. 4]
9. Mwanafunzi wa Biblia au mwamini mwenzako anapokuuliza jambo la kufanya katika hali fulani, utamjibu namna gani? [be uku. 69 fu. 4-5]
10. Ni nini kinachohusika katika “kufanywa upya katika nguvu zinazoendesha akili yenu”? (Efe. 4:23) [be uku. 74 fu. 4]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Katika Ezekieli 9:2-4, mwanamume anayevaa kitani anafananisha nani, na “alama kwenye mapaji ya uso” inafananisha nini? [w88 9/15 uku. 14 fu. 18]
12. Namna gani viongozi wa dini zinazojiwazia kuwa za Kikristo ni kama ‘manabii wajinga waliofuata roho yao wenyewe’ wanaozungumziwa kwenye Ezekieli 13:3? [w99 10/1 uku. 13]
13. Kwa kusema ‘neno la mfano’ lililoandikwa kwenye Ezekieli 18:2, Waisraeli walijaribu kufanya nini, na ni somo gani la maana linalokaziwa kuhusu daraka la mtu la kutoa hesabu juu ya vitendo vyake? [w88 9/15 uku. 18 fu. 10]
14. Wakati wa kuzingirwa (kuzungukwa) na kuharibiwa kwa Yerusalemu, Ezekieli alikuwa “bubu” katika njia gani? (Eze. 24:27; 33:22) [w03 12/1 uku. 29]
15. ‘Gogu wa inchi ya Magogu’ ni nani, na ni wakati gani ambapo atasimama ili kuharibu watu wa Mungu? (Eze. 38:2, 16) [w97 3/1 uku. 14 fu. 1–uku. 15 fu. 3]