Kujikumbusha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maulizo ya kujikumbusha yanayofuata yatatumiwa kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika juma tokea tarehe 31 mwezi wa 8, 2009. Kwa dakika 20, mwangalizi wa shule ataongoza kujikumbusha kunakotegemea habari zilizozungumziwa tokea tarehe 6 mwezi wa 7 mpaka tarehe 31 mwezi wa 8, 2009.
1. Kwa nini mutu yeyote ‘aliyewalaani’ wazazi wake alipaswa kuuawa? (Law. 20:9) [w04 5/15 uku. 24 fu. 6]
2. Kwa kuwa wanaume wote Waisraeli waliombwa kwenda kuhuzuria Sherehe ya Keki Zisizotiwa Chachu, ni nani aliyevuna matunda ya kwanza ya shayiri kwa ajili ya toleo? (Law. 23:5, 11) [w07 7/15 uku. 26 fu. 3]
3. Ni nini kinachofananishwa na mwaka wa Yubile? (Law. 25:10, 11) [w04 7/15 uku. 26-27]
4. Je, “alama” zinazotajwa kwenye Hesabu 2:2 zilikuwa na maana fulani ya kidini kwa Waisraeli? [w02 9/15 uku. 21 fu. 4]
5. Wahubiri wa Ufalme wa wakati wote wanaonyesha roho gani leo inayofanana na ile iliyoonyeshwa na Wanaziri katika Israeli la zamani? (Hes. 6:3, 5, 6) [w04 8/1 uku. 24-25]
6. Ni kanuni gani ya sheria inayohusu kuacha utumishi wa Kilawi inayoweza kutumiwa kuhusu watu wa Yehova leo? (Hes. 8:25, 26) [w04 8/1 uku. 25 fu. 1]
7. Namna gani Waisraeli walifikia kuonyesha “tamaa ya uchoyo” na hilo linawafundisha nini Wakristo leo? (Hes. 11:4) [w01 6/15 uku. 14-15; w95 3/1 uku. 16 fu. 10]
8. Kwa nini Miriamu peke yake ndiye aliyepigwa kwa ukoma na ni jambo gani la maana tunaloweza kujifunza kutokana na hilo? (Hes. 12:9-11) [w04 8/1 uku. 26 fu. 2; it-2-F uku. 295 fu. 1]
9. Yoshua na Kalebu walimaanisha nini waliposema kwamba wakaaji wa Kanaani ni “mkate”? (Hes. 14:9) [w06 10/1 uku. 17 fu. 5; it-2-F uku. 472 fu. 3]
10. Andiko la Hesabu 21:5 linatoa mfano gani wenye kuonya? [w99 8/15 uku. 26-27]