Programu ya Juma Tokea Tarehe 25 Mwezi wa 6
JUMA TOKEA TAREHE 25 MWEZI WA 6
Wimbo 63 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 22 fu. 15-21 (Dak. 25)
□ Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi:
Usomaji wa Biblia: Ezekieli 1-5 (Dak. 10)
Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi (Dak. 20)
□ Mukutano wa Utumishi:
Wimbo 59
Dak. 10: Matangazo. Kwa kutumia njia mbalimbali za kuanzisha mazungumuzo zinazoonyeshwa kwenye ukurasa wa 4, mufanye onyesho kuhusu jinsi funzo la Biblia linavyoweza kuanzishwa Siku ya Posho ya kwanza ya mwezi wa 7.
Dak. 15: Tumia Wakati Wako kwa Hekima Unapokuwa Katika Mahubiri. (Efe. 5:15, 16) Mazungumuzo yanayotegemea maulizo yafuatayo. (1) Namna gani tunaweza kutumia wakati kwa hekima: (a) tunapoongoza mukutano kwa ajili ya mahubiri? (b) mukutano kwa ajili ya mahubiri unapomalizika? (c) wakati muhubiri tuliyeenda naye katika motokari moja anakuwa na mazungumuzo marefu na mutu mwenye kupendezwa? (d) tunapowarudilia watu wenye kutawanyika katika eneo kubwa? (2) Namna gani tunakomboa wakati (a) ikiwa tunatumia chakula mbele ya kwenda kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri? (b) ikiwa kila mutu anafika kwa wakati kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri? (c) ikiwa tunasikiliza kwa uangalifu ndugu anayeongoza anapopanga watu na hivyo asilazimike kuwapanga watu upya kisha mukutano kwa ajili ya mahubiri? (d) ikiwa kila mutu anajua mahali ambapo ataanza kuhubiri mbele ya kwenda katika eneo?
Dak. 10: Broshua za Kutolea Watu Katika Mwezi wa 7. Mazungumuzo. Zungumuzia mambo makuu yaliyo katika moja kati ya broshua za kutolea watu katika mwezi wa 7, na mufanye onyesho moja ao maonyesho mawili.
Wimbo 29 na Sala