MAISHA YA MUKRISTO
Unaweza Kujaribu kwa Mwaka Moja?
Kujaribu nini? Kazi ya upainia wa kawaida! Utapata baraka nyingi sana! —Met 10:22.
KAMA UNAFANYA KAZI YA UPAINIA, UNAWEZA . . .
kuwa mweneza-injili mwenye ufundi na kufurahia zaidi kazi ya kuhubiri
kukomalisha urafiki wako pamoja na Yehova. Kwa sababu unazungumuza mara nyingi na wengine juu ya Yehova, utakumbushwa sifa zake zenye kupendeza sana
kujionea mwenyewe furaha yenye inatokana na kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza na furaha yenye inatokana na kujitoa kwa ajili ya wengine. —Mt 6:33; Mdo 20:35
kuhuzuria mukutano wenye mwangalizi wa muzunguko anafanya pamoja na mapainia wakati anatembelea kutaniko, mukutano wa pekee wakati wa mukusanyiko wa muzunguko, na Masomo ya Mapainia
kuwa na nafasi nyingi za kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia
kupitisha wakati mingi pamoja na wahubiri wengine na kubadilishana vitia-moyo.—Rom 1:11, 12