UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | METHALI 12-16
Hekima Ni ya Maana Kuliko Zahabu
Maandishi
Sababu gani hekima yenye kutoka kwa Mungu ni ya maana sana? Inasaidia watu wenye kuwa nayo wasifanye mabaya na inalinda uzima wao. Inawasaidia wakuwe na mawazo, maneno, na matendo mazuri
Hekima inatusaidia tusikuwe na kiburi
16:18, 19
Mutu mwenye hekima anakubali kama hekima inatoka kwa Yehova
Watu wenye kufanikiwa ao wenye kupewa madaraka fulani wanapaswa kuepuka kiburi na majivuno
Hekima inatusaidia kusema maneno yenye kujenga
16:21-24
Mutu mwenye hekima hatafute makosa ya wengine lakini anasema mambo mazuri juu yao
Maneno yenye hekima yanagusa moyo na ni matamu kama asali, haiko ya kuumiza ao ya kubishana