Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr17 Mwezi wa 8 uku. 1
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2017)
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 7-​13/08
  • TAREHE 14-​20/08
  • TAREHE 21-​27/08
  • TAREHE 28/08–3/09
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2017)
mwbr17 Mwezi wa 8 uku. 1

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 7-​13/08

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | EZEKIELI 28-​31

“Yehova Analipa Taifa la Wapagani”

it-2 uku. 1125 fu. 3

Tiro

Kuharibu Muji. Nebukadneza alizunguka Muji kwa siku nyingi sana mupaka vichwa vya maaskari “vilifanywa kuwa vipara” kwa sababu kofia zao na mabega yao ‘yalikwaruzwa’ kwa kubeba vyombo vya kutumia ili kufanya kazi za kuzunguka muji. Kwa sababu Nebukadneza hakupewa “malipo” kwa kazi yenye alifanya ya kutumiwa na Yehova ili kutimiza hukumu Yake juu ya Tiro, Yehova aliahidi kumupatia mali ya Misri. (Eze 29:17-​20) Josèphe, mwanahistoria Muyahudi anaeleza kama kuzunguka muji kulichukua miaka 13 (Contre Apion, I, 156 [21]), na Wababiloni waliteseka sana. Wanahistoria wengine hawazungumuzie wazi-wazi ukubwa na uwezo wa shambulio la Nebukadneza. Lakini, upande wa watu wa Tiro pia, inawezekana walikufa wengi.​—Eze 26:​7-​12.

it-1 uku. 713 fu. 5

Misri, Wamisri

Maandishi ya Wababiloni ya mwaka wa 37 wa utawala wa Nebukadneza (588 M.K.Y.) yenye kuzungumuzia kushambuliwa kwa Misri imepatikana. Haijulikane kama inazungumuzia shambulio la kwanza la muji, ao shambulio lingine la majeshi. Lakini, tunajua kama Nebukadneza alipewa mali ya Misri kuwa malipo kwa kazi yenye majeshi yake yalifanya ili kutimiza hukumu la Yehova juu ya Tiro, adui wa watu wa Mungu.​—Eze 29:18-​20; 30:10-​12.

g86 8/11 uku. 27 fu. 4-5

Tunapaswa Kulipa Kila Kodi?

Ili kujibia ulizo hilo, tuone namna muumbaji yeye mwenyewe alilipa serekali ya wanadamu kwa kazi yenye serikali hiyo ilimufanyia. Wakati Yehova alikasirikia sana muji wa zamani wa Tiro, alikamata mupango ili muji huo uharibiwe. Alitumia majeshi yenye nguvu ya Wababiloni yenye kuongozwa na mufalme Nebukadneza ili kutimiza mupango huo. Hata kama Wababiloni walipata ushindi, haikuwa mwepesi. Kwa hiyo, Yehova aliona kama walistahili kupata malipo kwa ajili ya kazi yenye walifanya. Alisema hivi katika Ezekieli 29:18, 19: “Mwana wa binadamu, Nebukadreza mwenyewe, mufalme wa Babiloni, alitumikisha jeshi lake utumishi mukubwa juu ya Tiro. . . . Lakini kuhusu malipo, hapakuwa na malipo yoyote kwa ajili yake na jeshi lake kutoka Tiro kwa ajili ya utumishi aliokuwa amefanya juu yake. Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninamupa Nebukadreza mufalme wa Babiloni inchi ya Misri, naye atauchukua utajiri wake na kuteka nyara kubwa kutokana nayo na kuipora kwa wingi sana; nayo itakuwa malipo kwa ajili ya jeshi lake.’”

Wanafunzi wa Biblia wanajua kama Nebukadneza alikuwa mufalme mupagani, mwenye kiburi na muchoyo. Majeshi ya Babiloni ilijulikana sana kwa sababu ya kuwatesa watu wenye walikamata kwenye vita. Yehova hakukubali mwenendo kama huo, lakini kwake, deni ilikuwa deni, na aliilipa yote.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-2 uku. 550 fu. 3-4

Ukamilifu

Mutenda-zambi wa kwanza na mufalme wa Tiro. Kwa kweli, zambi na kukosa kukamilika kulianzia katika ulimwengu wa roho mbele kufike kwa wanadamu kama vile Yesu anasema katika Yohana 8:​44 na habari yenye kuelezwa katika Mwanzo sura ya 3. Wimbo wa huzuni katika Ezekieli 28:12-​19, hata kama ulimuhusu mwanadamu, ‘mufalme wa Tiro,’ ni wazi kama unaonyesha pia kujiendesha kwa mwana wa Mungu, mutu wa roho wa kwanza kufanya zambi. Kiburi cha ‘mufalme wa Tiro,’ yeye kujiita kuwa ‘mungu,’ kuitwa “kerubi,” na kutajwa kwa “Edeni, bustani ya Mungu,” mambo hayo yote yanafanana sana na maelezo ya Biblia juu ya Shetani Ibisi, mwenye alijivuna kwa kiburi, mwenye kufananishwa na nyoka wa Edeni, na mwenye kuitwa ‘mungu wa mufumo huu wa mambo.’​—1Tim 3:6; Mwa 3:​1-5, 14, 15; Ufu 12:9; 2Kor 4:4.

Huyo mufalme wa Tiro mwenye hajulikane, mwenye anaishi katika muji wenye kujiita kuwa ‘mukamilifu wa uzuri,’ alikuwa mwenyewe kitu “kinachojaa hekima na kikamilifu [neno lenye kufanana na neno la Kiebrania ka·lalʹ] katika uzuri,” na ‘hakuwa na kosa [Heb., ta·mimʹ]’ katika njia zake tangu siku ya kuumbwa kwake mupaka wakati ukosefu wa haki ulionekana ndani yake. (Eze 27:3; 28:12, 15) Utimizo wa kwanza wa moja kwa moja wa nyimbo za huzuni zenye kupatikana katika kitabu cha Ezekieli unahusu pengine kizazi cha wafalme wa Tiro, hapana mufalme fulani wa pekee. (Linganisha na unabii wenye ulitolewa juu ya ‘mufalme wa Babiloni’ mwenye hatajwe jina katika Isaya 14:​4-​20.) Kama ni hivyo, pengine ni urafiki wenye wafalme wa Tiro walionyesha mwanzoni wakati wa utawala wa wafalme Daudi na Sulemani, wakati Tiro alichangia ili kujenga hekalu la Yehova kwenye Mulima Moria. Kwa hiyo, mwanzoni serikali ya Tiro ilitendea muzuri Israeli, taifa la Yehova. (1Fal 5:​1-​18; 9:​10, 11, 14; 2Nya 2:​3-​16) Lakini, wafalme wenye walitokea nyuma, waliacha mwelekeo huo wenye ‘haukuwa na kosa’, na kwa hiyo manabii Yoeli, Amosi, na Ezekieli wakatoa unabii wa hukumu ya Mungu juu yake. (Yoe 3:​4-8; Amo 1:​9, 10) Zaidi ya kufananisha mwenendo wa “mufalme wa Tiro” na mwenendo wa adui mukubwa wa Mungu, unabii huo unaonyesha tena kama neno “ukamilifu” na “utimilifu” yanaweza kutumiwa katika maana mengine.

w03 1/7 uku. 32 fu. 1-3

Ni Nini Kilipata Miji ya Nofu na No?

NOFU na No ni majina ya miji mikubwa miwili ya Misri ya zamani yenye kupatikana katika Biblia, Memfisi na Thebesi. Miji hiyo ilijulikana sana. Nofu (Memfisi ao Memphis) ilikuwa kwenye kilometre 23 hivi kusini mwa Cairo, upande wa kaskazini ya Muto Nile. Hata hivyo, mwishowe, Memfisi haikuwa tena muji mukubwa wa Misri. Mwanzoni mwa miaka ya 1400 M.K.Y., No (Thebesi ao Thèbes) muji wenye ulikuwa kwenye kilometre 500 hivi kusini mwa Nofu ukakuwa muji Mukubwa wa Misri. Kati ya mabomoko mengi ya mahekalu ya Thebesi ni mabomoko ya hekalu la Karnak, lenye kuzaniwa kuwa nyumba ya mukubwa kuliko zote zenye zimejengwa kwa nguzo. Thebesi na hekalu lake Karnak lilitolewa kwa ibada ya Amoni, mungu mukubwa wa Wamisri.

Unabii wa Biblia ulitabiri nini juu ya Memfisi na Thebesi? Ulitabiri kuhukumiwa kwa Farao wa Misri na miungu yake, zaidi sana “Amoni na No.” (Yeremia 46:25, 26) Watu wengi sana wenye walienda huko ili kuabudu ‘wangekatiliwa mbali.’ (Ezekieli 30:14, 15) Na jambo hilo lilitimia. Kuhusu ibada ya Amoni, leo, kunabakia tu mabomoko ya hekalu zake. Muji wa sasa wa Luxor unapatikana upande mumoja wa mahali kulikuwa muji wa Thebesi wa zamani, na miji mingine midogo-midogo inapatikana kati ya mabomoko yake.

Kuhusu Memfisi, makaburi yake tu ndiyo ingali leo. Louis Golding, mwenye kujua sana mambo ya Biblia, anasema: “Kwa mamia ya miaka, Waarabu washindi kutoka Misri walichimbula majiwe ya mabomoko makubwa ya Memfisi ili kujenga muji mukubwa wa [Cairo] ngambo ya muto. Wajenzi hao Waarabu walichimbula sana na kisha muchanga wa muto Nile ukafunika muji huo wa zamani hivi kwamba hakuna jiwe lenye kuonekana tena kwenye kilometre nyingi juu ya udongo mweusi.” Namna Biblia ilitabiri, Memfisi imekuwa ‘kitu cha kushangaza’ bila ‘mukaaji.’—Yeremia 46:19.

TAREHE 14-​20/08

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | EZEKIELI 32-​34

“Mulinzi Alikuwa na Daraka Kubwa”

it-1 uku. 1044 fu. 3

Mulinzi

Matumizi ya Mufano. Yehova alitokeza manabii wenye, kwa njia ya mufano, walifanya kazi ya walinzi wa taifa la Israeli (Yer 6:​17). Na kwa upande wao manabii hao, walizungumuzia walinzi wa mufano. (Isa 21:​6, 8; 52:8; 62:6; Hos 9:8) Manabii-walinzi hao walikuwa na daraka la kuonya waovu juu ya uharibifu wenye ulikaribia. Lakini, kama hawakufanya kazi yao, walikuwa na hatia. Lakini, kama watu walikataa ujumbe na kukataa kufuata maonyo, damu yao ilikuwa juu ya vichwa vyao. (Eze 3:​17-​21; 33:​1-9) Nabii mwenye kukosa uaminifu alionwa kuwa wa bure kama vile mulinzi kipofu na imbwa bubu.​—Isa 56:10.

w88 1/1 uku. 28 fu. 13

Tuendelee Kuhubiri Ufalme

Tuepuke Deni ya Damu

Tunaweza kufananisha daraka la Mashahidi wa Yehova la kuwaonya watu juu ya hukumu ya Yehova yenye kuwa karibu na daraka lenye nabii Ezekieli alipewa. Alifanywa kuwa mulinzi wa taifa la Israeli na alikuwa na daraka la kuwaonya Waisraeli waachane na njia zao za mubaya ili Mungu asilete hukumu yake juu yao. Kama hawakuwaonya waovu, hukumu ya Yehova ingekuja juu ya waovu hao, lakini damu yao ingekuwa juu ya vichwa vya walinzi hao wenye kuzarau mambo. Kwa kufanya hivyo, Yehova alikuwa anaonyesha namna anaona hukumu yenye analeta juu ya waovu: ‘Ninapendezwa, si na kifo cha muovu, bali kwamba mutu muovu ageuke na kuiacha njia yake na kwa kweli aendelee kuishi. Geukeni, geukeni muziache njia zenu mbaya, maana kwa nini mukufe, Ee nyumba ya Israeli?’—Eze 33:1-11.

w12 15/3 uku. 15 fu. 3

Tuendelee Kutambua Uhitaji wa Kutenda Kwa Haraka

SABABU GANI KAZI YETU YA KUHUBIRI NI YA HARAKA?

Wale wanakubali ujumbe wa Ufalme wataokolewa na wale wenye wanaukataa wataharibiwa. Kuchunga hilo katika akili kutatusaidia tuone kuwa ni jambo la haraka kuhubiria watu habari njema. (Rom 10:13, 14) Neno la Mungu linasema hivi: ‘Ninapomuambia muovu: Hakika utakufa, naye kwa kweli anageuka na kuiacha zambi yake na kuendelea kutenda haki na uadilifu, hakika ataendelea kuishi. Yeye hatakufa. Hakuna yoyote kati ya zambi zake alizozitenda itakayokumbukwa juu yake.’ (Eze 33:14-16) Ndiyo sababu, sisi wahubiri wa Ufalme, Biblia inatuambia hivi: “Utajiokoa wewe mwenyewe na [kuokoa] wale wanaokusikiliza pia.”—1 Tim 4:16; Eze 3:17-21.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w91 15/3 uku. 17 fu. 16-​17

Endelea Sambamba Pamoja na Gari la Yehova la Kimbingu

Hatuzuiliwi na Kutojali kwa Watu

Ezekieli pia alituachia mufano muzuri: Alitii na hakurudia nyuma hata kama watu walimuzihaki na hawakujali. Sisi pia, kwa kufuata karibu-karibu kuendelea kwa luga safi, tunaenda njia moja na Mufalme Muendeshaji Gari. Kwa hiyo, tunapata vifaa ili kutii amri zake, na tunatiwa nguvu ili hata kama watu wenye tunatangazia ujumbe wa hukumu ya Yehova wanatuzihaki ao hawajali, hilo halituzuie. Kama vile alimufanyia Ezekieli, Mungu ametangulia kutuonya kama watu fulani wenye vichwa vigumu na mioyo migumu wangetupinga sana. Wengine hawangesikia kwa sababu hawataki kumusikiliza Yehova. (Ezekieli 3:7-9) Wengine pia wangekuwa wanafiki, kama vile Ezekieli 33:31, 32 inasema: ‘Nao wataingia ndani kwako, kama wanavyoingia watu, na kuketi mbele yako kama watu wangu; nao hakika watayasikia maneno yako lakini hawatayatenda, kwa maana wanaonyesha tamaa zenye uchu kwa kinywa chao nao moyo wao unafuatilia pato lao lisilo la haki. Na, tazama! kwao wewe ni kama wimbo wa mapendo yenye hisia, kama mutu mwenye sauti nzuri na mwenye kupiga kinanda vizuri. Nao hakika watayasikia maneno yako, lakini hakuna yeyote anayeyatenda.’

Matokeo ingekuwa nini? Mustari wa 33 unaongezea hivi: “Na yatakapotimia—tazama! lazima yatatimia—wao pia watalazimika kujua kwamba nabii alikuwa katikati yao.” Maneno hayo yanaonyesha kama Ezekieli hakuacha kazi yake hata kama hakupata matokeo ya muzuri. Hata kama watu hawakujali, Ezekieli hakuvunjika moyo. Wamusikilize ao hapana, yeye alimutii Mungu na kutimiza kazi yake.

w07 1/4 uku. 26 fu. 3

Tujitiishe kwa Unyenyekevu Kwa Wachungaji Wenye Upendo

Unabii wa Isaya 40:10, 11 unakazia namna Yehova anahangaikia kwa upendo mwingi watu wake wakati anawachunga. (Zaburi 23:1-6), Wakati alikuwa katika dunia, Yesu alionyesha pia kama aliwahangaikia wanafunzi wake na watu wengine kwa upendo mwingi. (Mathayo 11:28-30; Marko 6:34) Yehova na Yesu hawakufurahia ukosefu wa huruma wa wachungaji, ao viongozi wa Israeli wenye, bila haya, walizarau makundi yao na kuyatumikisha kwa faida zao. (Ezekieli 34:2-10; Mathayo 23:3, 4, 15) Yehova aliahidi hivi: ‘Nitawaokoa kondoo zangu, nao hawataendelea kuwa tena kitu cha kuporwa; nami nitahukumu kati ya kondoo na kondoo. Nami nitasimamisha juu yao muchungaji mumoja, naye atawalisha, ndiyo, mutumishi wangu Daudi. Yeye mwenyewe atawalisha, na yeye mwenyewe atakuwa muchungaji wao.’ (Ezekieli 34:22, 23) Wakati huu wa mwisho, Yesu Kristo, Daudi Mukubwa, ndiye ‘muchungaji mumoja’ mwenye Yehova ameweka juu ya watumishi Wake wote katika dunia, Wakristo watiwa-mafuta na “kondoo wengine.”—Yohana 10:16.

TAREHE 21-​27/08

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | EZEKIELI 35-​38

“Gogu wa Magogu Ataharibiwa Karibuni”

w15 15/5 uku. 29-​30

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Kwa hiyo, Gogu wa Magogu ni nani? Ili kujibu ulizo hilo, ni lazima tuchunguze Maandiko ili tujue ni nani mwenye anashambulia watumishi wa Mungu. Biblia inazungumuzia shambulizi la ‘Gogu wa Magogu.’ Lakini pia, inazungumuzia shambulizi la ‘mufalme wa kaskazini’ na shambulizi la “wafalme wa dunia.” (Eze. 38:2, 10-13; Dan. 11:40, 44, 45; Ufu. 17:14; 19:19) Mashambulizi hayo inatofautiana? Jibu ni hapana. Bila shaka Biblia inatumia majina hayo ili kuzungumuzia shambulizi lilelile. Sababu gani tunasema hivyo? Kwa sababu Biblia inatuambia kwamba mataifa yote ya dunia itajiunga pamoja ili kufanya shambulizi hilo la mwisho lenye litatokeza vita ya Har-Magedoni.—Ufu. 16:14, 16.

Wakati tunalinganisha Maandiko hayo yote yenye kuzungumuzia shambulizi la mwisho juu ya watumishi wa Mungu, tunaelewa muzuri kwamba Gogu wa Magogu haiko Shetani, lakini ni muungano wa mataifa. Je, muungano huo wa mataifa ndio utakuwa ‘mufalme wa kaskazini’? Hatuwezi kuhakikisha jambo hilo. Lakini inaonekana kwamba mawazo hayo inapatana na maneno yenye Yehova anasema juu ya Gogu. Yehova anasema hivi: ‘Na wewe hakika utakuja kutoka mahali pako, kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini, wewe na vikundi vingi vya watu pamoja na wewe, hao wote wakiwa wamepanda farasi, kutaniko kubwa, naam, jeshi kubwa sana.’—Eze. 38:6, 15.

w12 15/9 uku. 5-6 fu. 8-9

Namna Ulimwengu Huu Utakavyofikia Mwisho Wake

Kisha dini ya uongo kuharibiwa, watumishi wa Mungu wataonekana kama wangali ‘wanakaa kwa usalama’ na “bila ukuta.” (Eze. 38:11, 14) Wao wataendelea kumuabudu Yehova, lakini wataonekana kama hawana mutu wa kuwapigania. Ni jambo gani litawapata? Inaonekana kama watashambuliwa na “vikundi vingi vya watu.” Biblia inaita shambulio hilo shambulio la ‘Gogu wa inchi ya Magogu.’ (Soma Ezekieli 38:​2, 15, 16.) Je, tunapaswa kuogopa shambulio hilo?

Kujua mbele ya wakati namna watu wa Mungu watashambuliwa hakutuogopeshe sana. Jambo lenye tunahangaikia sana haiko wokovu wetu, lakini ni kuona jina la Yehova linatakaswa na pia watu wajue kama yeye ndiye anastahili kutawala ulimwengu wote muzima. Kwa kweli, Yehova anasema zaidi ya mara 60: ‘Nanyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ (Eze. 6:7) Kwa hiyo, tunangojea kwa hamu sana kuona wakati unabii huo wa Ezekieli utatimia, na tunaamini kama “Yehova anajua jinsi ya kuwakomboa watu wenye ujitoaji-kimungu kutoka katika jaribu.” (2 Pet. 2:9) Wakati tunangojea utimizo wa unabii huo, tunatumia kila nafasi kuitia imani yetu nguvu ili tuweze kubakia waaminifu kwa Yehova hata kutokee jaribu la namna gani. Tufanye nini basi? Tunapaswa kusali, kujifunza na kuwaza sana juu ya Neno la Mungu, na kuwaelezea wengine ujumbe wa Ufalme. Kwa kufanya hivyo, tumaini letu la uzima wa milele halitatikisika na litakuwa kama “nanga.”—Ebr. 6:19; Zab. 25:21.

w14 15/11 uku. 27 fu. 16

“Sasa Nyinyi ni Watu wa Mungu”

Kisha Babiloni Mukubwa kuharibiwa, watu wa Yehova watashambuliwa. Wakati huo tutakuwa na lazima ya ulinzi wenye Yehova atatolea watumishi wake. Kwa sababu shambulio hilo litaanzisha sehemu ya mwisho ya ‘ziki kubwa,’ ni Yehova mwenyewe ndiye atatokeza shambulio hilo na ni yeye ndiye atachagua wakati kwa ajili ya shambulio hilo. (Mt. 24:21; Eze. 38:2-4) Wakati huo, Gogu atashambulia “watu waliokusanywa pamoja kutoka katika mataifa,” ni kusema, watu wa Yehova. (Eze. 38:10-12) Shambulio hilo litaonyesha kwamba Yehova anataka kuleta hukumu juu ya Gogu pamoja na wale wenye wanamuunga mukono. Yehova atatukuza utawala wake mukubwa na atalitakasa jina lake, kwa sababu anasema hivi: ‘Nami hakika . . . nitajijulisha mwenyewe mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’—Eze. 38:18-23.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w02 15/6 uku. 20 fu. 12

Ujifunze na Uwafundishe Wengine Kanuni za Mwenendo wa Kikristo

Mutume Paulo alikazia sababu moja ya maana sana ya kujifunza na kufuata kanuni za Biblia za mwenendo. Mwenendo mubaya wa Wayahudi ulimuvunjia Yehova heshima: “Wewe, unayejivunia sheria, je, kwa kuivunja Sheria unamuvunjia Mungu heshima? Kwa maana ‘jina la Mungu linafanyiwa makufuru katikati ya mataifa kwa sababu yenu’; kama ilivyoandikwa.’” (Waroma 2:23, 24) Hali iko hivyo leo. Wakati tunazarau kanuni za mwendeno wa Kikristo, tunamuvunjia heshima Yehova mwenye alianzisha kanuni za mwenendo huo. Na wakati tunafuata kwa uaminifu kanuni zake za mwenendo tunamuletea heshima. (Isaya 52:5; Ezekieli 36:20) Kujua jambo hilo kunaweza kukusaidia uendelee kuwa muaminifu wakati unakutana na majaribu ao hali zenye zinaweza kukufanya ufikiri kama kuzarau kanuni za mwenendo wa Kikristo ndio jambo mwepesi ao lenye kufaa zaidi kufanya. Maneno ya Paulo yanatufundisha jambo lingine pia. Zaidi ya kujua kama mwenendo wako muzuri unamuletea Mungu heshima, uwasaidie pia watu wenye unafundisha waelewe kama wanamuletea Yehova heshima wakati wanafuata kanuni za mwenendo zenye wanajifunza. Wakati tunafuata kanuni za mwenendo wa Kikristo tunakuwa na afya ya muzuri na tunapata furaha ya kweli; na tena, tunamuletea heshima Yule mwenye alianzisha kanuni hizo, mwenye anatia moyo watu wazifuate.—Zaburi 74:10; Yakobo 3:17.

w88 15/9 uku. 24 fu. 11

“Watalazimika Kujua Kwamba Mimi ni Yehova”

Kisha Wayahudi kurudia huko Yuda, inchi hiyo yenye haikuwa tena na watu iligeuka kuwa “Bustani ya Edeni” yenye kutoa chakula. (Soma Ezekieli 36:33-​36). Vile vile, tangu 1919, Yehova aligeuza hali ya Wakristo watiwa-mafuta kuwa paradiso ya kiroho, mahali kwenye “umati mukubwa” unakaa pia leo. Kwa sababu Yehova amejaza paradiso ya kiroho na watu watakatifu, kila Mukristo mwenye kubatizwa anapaswa kujikaza sana ili kuilinda safi.—Ezekieli 36:37, 38.

TAREHE 28/08–3/09

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | EZEKIELI 39-​41

“Hekalu Lenye Ezekieli Aliona Linatufundisha Nini?”

w99 1/3 uku. 11 fu. 16

‘Weka Katika Moyo Wako’ Hekalu la Mungu!

Ili kupata jibu, turudilie maono yenyewe. Ezekieli aliandika: ‘Katika maono ya Mungu alinileta katika inchi ya Israeli na hatua kwa hatua akaniweka juu ya mulima murefu sana, ambao juu yake palikuwa na kitu kama muundo wa jiji kuelekea kusini.’ (Ezekieli 40:2) Mahali penye mambo hayo yanapitika, ni kusema, kwenye ‘mulima murefu sana,’ panatukumbusha Mika 4:1: ‘Na itatukia katika siku za mwisho kwamba mulima wa nyumba ya Yehova utawekwa imara juu ya kilele cha milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na vikundi vya watu vitamiminika huko.’ Unabii huo unaanza kutimizwa wakati gani? Mika 4:5 inaonyesha kama unaanza kutimizwa wakati mataifa ingali inaabudu miungu ya uongo, ni kusema, wakati wetu huu wa “siku za mwisho,” siku zenye ibada safi imeinuliwa juu, imerudishwa mahali pake penye kufaa katika maisha ya watumishi wa Mungu.

w07 1/8 uku. 10 fu. 2

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli—II

40:3–​43:17​—Kupima hekalu kunamaanisha nini? Kupima hekalu ni alama yenye kuonyesha kama kusudi la Yehova kuhusu ibada safi litatimizwa kabisa.

w07 1/8 uku. 11 fu. 4

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli—II

40:14, 16, 22, 26. Michongo ya miti ya mitende yenye ilikuwa kwenye miingilio ya hekalu hilo inaonyesha kama ni wale tu wenye kuwa na mwenendo muzuri ndio wanaruhusiwa kuingia. (Zaburi 92:12) Hilo linatufundisha kama Yehova anakubali ibada yetu kama tu tunatenda kwa haki.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w12 1/9 uku. 21 fu. 2

“Mataifa Watalazimika Kujua Kwamba Mimi Ni Yehova”

Yehova anasema hivi: “Sitaliacha tena jina langu litiwe [uchafu].” Wakati watu wanasema kama ukosefu wa haki ni mapenzi ya Mungu, wanalichafua jina lake. Sababu gani tunasema hivyo? Katika Biblia, mara nyingi “jina” linamaanisha sifa. Kitabu kimoja kinasema kama jina la Mungu linatumiwa ili kumaanisha ‘namna anajulikana, namna anatambuliwa; na pia sifa yake na utukufu wake.’ Kwa hiyo, jina la Yehova linamaanisha sifa yake. Basi, Yehova anajulikana kuwa na sifa gani juu ya ukosefu wa haki? Yeye anachukia ukosefu wa haki! Na tena anawasikilia huruma watu wenye wanateseka kwa sababu ya ukosefu wa haki. (Kutoka 22:22-24) Kama Mungu anachukia sana mambo hayo ya mubaya, lakini watu wanasema kama hayo ni mapenzi yake, hauone kama wanamuharibishia sifa? Kwa kufanya hivyo, ‘wanalizarau jina lake.’—Zaburi 74:10.

w89 15/8 uku. 14 fu. 20

Kufungua Mulango Wenye Kuongoza Tena Kwenye Paradiso

Lakini itakuwa namna gani kuhusu silaha zenye mataifa itaacha? Kulingana na miaka ya mufano yenye itaomba ipite ili kuunguza sehemu zenye zinaweza kuungua za silaha hizo, inaonekana itakuwa silaha nyingi sana (Ezekieli 39:8-10). Pengine wale wenye wataokoka Har-magedoni watageuza sehemu yenye itabakia ya silaha hizo za vita za mataifa kuwa majembe.—Isaya 2:2-4.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine