Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 3-9/6
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAGALATIA 4-6
“Maana ya ‘Tukio la Mufano’”
it-1-F uku. 56 fu. 1
Hagari
Kulingana na mutume Paulo, Hagari alitimiza daraka fulani mu tukio la mufano: Alifananisha taifa la Waisraeli wa kimwili, wenye walifanya agano la Sheria na Yehova ku mulima Sinai. Agano la Sheria lilizaa “watoto kwa ajili ya utumwa.” Juu Waisraeli hawakukuwa wakamilifu, hawakuweza kuheshimia sheria za ile agano. Ile agano haikusaidia Waisraeli wakuwe huru. Lakini walihukumiwa kuwa watenda-zambi wenye wanastahili kifo; kwa hiyo, walikuwa watumwa. (Yoh 8:34; Ro 8:1-3) Yerusalemu ya wakati wa Paulo ilifananisha Hagari, juu ile muji mukubwa, yenye ilifananisha tengenezo la Waisraeli wa kimwili, ilikuwa mu utumwa pamoja na watoto wake. Lakini, Wakristo wenye kutiwa mafuta na roho, wao ni watoto wa “Yerusalemu la juu,” bibi ya Mungu wa mufano. Sawa vile Sara, mwanamuke mwenye alikuwa huru, “Yerusalemu la juu” haliyakuwaka mu utumwa. Tena, sawa vile Ishmaeli alikuwa anatesa Isaka, vilevile watoto wa Yerusalemu lenye kuwa katika utumwa walikuwa wanatesa watoto wa “Yerusalemu la juu.” Kwa mwisho, sawa vile Abrahamu alifukuzaka Hagari na mutoto wake mwanaume, vilevile Yehova alikataa taifa la Wasiraeli wa kimwili.—Gal 4:21-31; ona pia Yoh 8:31-40.
Ukuwe na Imani Yenye Nguvu Katika Ufalme
11 Agano na Abrahamu lilitimia kwa njia ya kimwili wakati wazao wa Abrahamu waliingia katika Inchi ya Ahadi. Hata hivyo, Biblia inaonyesha kwamba agano hilo lilipaswa pia kutimia kwa njia ya kiroho. (Gal. 4:22-25) Kuhusu utimizo huo wa pili, roho ya Mungu ilimuongoza mutume Paulo afasirie kwamba sehemu ya kwanza ya uzao wa Abrahamu ni Kristo na kwamba sehemu ya pili ni Wakristo watiwa-mafuta 144000. (Gal. 3:16, 29; Ufu. 5:9, 10; 14:1, 4) Mwanamuke ambaye anatokeza uzao huo ni ‘Yerusalemu wa juu,’ ni kusema, sehemu isiyoonekana ya tengenezo la Mungu ambayo inafanyizwa na viumbe waaminifu wa kiroho. (Gal. 4:26, 31) Kulingana na ahadi ambayo ilitolewa kupitia agano na Abrahamu, uzao wa mwanamuke utawaletea wanadamu baraka nyingi.
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
w09 1/4 uku. 13
Ulijua?
Juu ya nini Yesu alimuita Yehova “Abba, Baba,” wakati alikuwa anasali?
Neno la Kiaramu ʼab·baʼʹ linaweza kumaanisha “baba” ao “Ee Baba.” Linapatikana mara tatu katika Maandiko mu sala mbalimbali na linamaanisha Baba wa mbinguni, Yehova. Wakati Yesu alikuwa ku dunia, neno ʼab·baʼʹ lilikuwa na maana gani?
Kitabu kimoja (The International Standard Bible Encyclopedia) kinasema: “Mu mazungumuzo ya kawaida mu siku za Yesu, neno ʼabbāʼ ni neno la kirafiki na la heshima lenye watoto walikuwa wanatumia ili kuzungumuza na baba zao.” Neno ʼabbāʼ lilitumiwa na mutoto mwenye alikuwa anapenda sana baba yake na lilikuwa kati ya maneno ya kwanza yenye mutoto alijifunza. Yesu alitumia neno ʼabbāʼ wakati alikuwa anamulilia Baba yake mu sala. Mu bustani ya Getsemane, saa kidogo mbele akufe, Yesu alitumia maneno “Abba, Baba,” wakati alikuwa anasali kwa Yehova.—Marko 14:36.
Kitabu chenye tulitaja pale juu kinasema: “Vitabu vya Wayahudi vya wakati wa utawala wa Wagiriki na Waroma, havitumie sana neno ʼabbāʼ wakati vinazungumuzia Mungu. Pengine ni juu kutumia lile neno la kirafiki wakati wa kuomba Mungu ingeonekana kuwa kukosa heshima.” Lakini, “wakati Yesu anatumia lile neno katika sala . . . ile inaonyesha mu njia yenye haiko ya moja kwa moja kwamba Yesu hakudanganya wakati alionyesha kama alikuwa rafiki wa sana wa Mungu.” Mu maandishi ya Paulo tunapata maandiko mbili yenye iko na neno “Abba.” Ile inaonyesha kama Wakristo wa karne ya kwanza pia walikuwa wanatumia neno “Abba” mu sala zao.—Waroma 8:15; Wagalatia 4:6.
w10 1/11 uku. 15
Ulijua?
Mutume Paulo alimaanisha nini wakati alisema kama alikuwa na “alama za mutumwa wa Yesu” ku mwili wake?—Wagalatia 6:17.
Pengine wasikilizaji wa karne ya kwanza walielewa maneno ya Paulo mu njia mingi. Kwa mufano, zamani, walitumia chuma cha moto juu ya kutia alama wafungwa wa vita, watu wenye waliiba mu mahekalu, na watumwa wenye walitoroka. Wakati walitia alama ya vile ku mwili wa mutu, watu waliona kuwa inamuzaraulisha.
Lakini, watu hawakuona kila alama kuwa ya kuzaraulisha. Watu mingi wa zamani walitumia zile alama ili kuonyesha kama wao ni wa kabila ao dini fulani. Kwa mufano, kulingana na kamusi moja, (Theological Dictionary of the New Testament), “Wasiria walionyesha kama wamejitoa kwa mungu Hadadi na mungu Atargatisi kwa kutia alama ku kifundo cha mikono ao ku shingo . . . Muabudu wa Dionisio alitiwa alama ya majani ya muti wa mwefeu.”
Wachunguzi mingi wa leo wanafikiri kama Paulo alikuwa anazungumuzia makovu yenye alipata wakati walimupiga na iko anafanya kazi ya umisionere. (2 Wakorinto 11:23-27) Lakini, pengine Paulo alimaanisha kama namna yake ya kuishi njo ilikuwa alama yenye ilimutambulisha kuwa Mukristo, hapana alama fulani ku mwili wake.
TUJITOE KABISA KATIKA KAZI YA KUHUBIRI
Hotuba
Maulizo ya Wasomaji Wetu
Je, Mukristo aliye na zoezi la kutazama ponografia (picha ao habari za ngono) anaweza kufikia kutengwa na ushirika?
Ndiyo. Hilo linaonyesha kwa nini ni lazima kuepuka kabisa kila namna ya ponografia. Hilo linatia ndani kusoma vitabu, magazeti, kutazama filme, video, na programu za internet zinazoonyesha ponografia.
Ponografia inaenea mahali pote ulimwenguni. Hesabu ya watu wanaotazama ponografia inaongezeka kwa kuwa internet inafanya iwe rahisi kutazama ponografia. Watu fulani, vijana na wazee, wameona mambo ya ponografia bila kukusudia wanapofungua internet. Wengine wanafungua kwa makusudi programu ya internet iliyo na mambo ya ponografia, wanajisikia kuwa huru zaidi kwa kuwa wanaweza kusoma ao kutazama mambo hayo kwa uficho nyumbani ao katika biro kazini. Kwa nini Wakristo hawapaswi kuona ponografia kuwa jambo la muchezo?
Sababu inapatikana katika onyo hili la Yesu: ‘Kila mutu ambaye anaendelea kumutazama mwanamuke na kumutamani tayari amefanya uzinzi pamoja naye moyoni mwake.’ (Mt. 5:28) Ni kweli kwamba mume na muke waliooana wanaruhusiwa kufanya ngono, na hilo linawaletea furaha. (Mez. 5:15-19; 1 Ko. 7:2-5) Lakini ponografia inakusudi lingine. Ponografia inakazia ngono isiyoruhusiwa inayoamusha mawazo mabaya ambayo Yesu alituonya tuepuke. Kwa kweli, kusoma ao kutazama mambo ya ponografia ni kinyume na muongozo huu wa Mungu: ‘Kwa hiyo, viueni viungo vya mwili wenu vilivyo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono, tamaa yenye mazara, na kutamani, ambako ni ibada ya sanamu.’—Kol. 3:5.
Namna gani ikiwa Mukristo alitazama ponografia mara moja ao mara mbili tu? Hali yake inaweza kufananishwa na hali ya hatari ambayo wakati fulani mutunga-zaburi Asafu alipatikana ndani: “Mimi nami karibu miguu yangu igeuke kando, hatua zangu zilikuwa karibu kuteleza.” Namna gani Mukristo aliyeangalia kwa muda mambo ya ponografia, yaani, picha za wanawake ao wanaume walio uchi ao watu wenye kufanya uasherati, anaweza kuwa na zamiri safi na kuwa na amani pamoja na Mungu? Asafu alikosa amani, yeye alisema: ‘Nami nikapata mapigo muchana kutwa, na rekebisho langu ni la kila asubuhi.’—Zb. 73:2, 14.
Mukristo anayetazama ponografia anapaswa kuamuka kiroho na kutafuta musaada. Musaada huo unapatikana katika kutaniko: ‘Hata mutu akijikwaa katika kosa fulani kabla ya yeye kulijua, ninyi mulio na sifa za kustahili kiroho jaribuni kumurekebisha upya mutu huyo katika roho ya upole, huku kila mumoja wenu akiendelea kujiangalia.’ (Gal. 6:1) Muzee mumoja ao wazee wawili wanaweza kumutolea musaada. Wanaweza kutoa ‘sala ya imani inayoweza kumuponya huyo asiyejisikia vizuri, na zambi yake inaweza kusamehewa.’ (Yak. 5:13-15) Wale waliotafuta musaada ili kuondoa uchafu wa ponografia katika maisha yao wametambua kama Asafu, kwamba ni jambo la lazima sana kufanya hivyo ili kumukaribia Mungu.—Zb. 73:28.
Hata hivyo, mutume Paulo alisema kwamba watu fulani waliotenda zambi hawakutubu ‘kutokana na unajisi wao na uasherati na mwenendo mupotovu.’ (2 Ko. 12:21) Profesa Marvin R. Vincent alisema kwamba neno la Kigiriki lililotumiwa hapo ili kutafsiri neno “unajisi,” ni “uchafu wenye kuchukiza sana.” Ni jambo la huzuni sana kuona kwamba picha zingine za ponografia zinaonyesha mambo machafu sana kupita picha za wanawake walio uchi ao mwanaume na mwanamuke wakifanya uasherati. Ni ponografia yenye kuchukiza sana, yenye kinyaa, inayotia ndani ngono ya wanaume kwa wanaume ao wanawake kwa wanawake, kikundi cha watu wenye kufanya ngono ao kulalana kwa kubadilishana, kufanya ngono na wanyama, kufanya ngono na watoto wadogo, wanawake wakilalwa kinguvu na kikundi cha watu wengi, kuwatesa wanawake kingono, ao kuwatesa kinyama. Wakati wa mutume Paulo watu fulani waliokuwa ‘katika giza kiakili waliishiwa ufahamu wote wa maadili na wakajitoa wenyewe ili kuwa na mwenendo mupotovu na kufanya ukosefu wa usafi wa kila namna kwa pupa.’—Efe. 4:18, 19.
Mutume Paulo alizungumuzia pia neno “uchafu” kwenye Wagalatia 5:19. Mutu fulani mwenye elimu ya Biblia alionyesha kwamba neno hilo linaweza kumaanisha zaidi sana “tamaa ya ngono isiyo ya kawaida.” Ni Mukristo gani anayeweza kukataa kwamba mambo hayo machafu ya ponografia yanayotajwa hapo juu ni ‘tamaa ya ngono isiyo ya kawaida’ na ni yenye kuchukiza sana? Katika andiko la Wagalatia 5:19-21 Paulo alimalizia kwa kusema kwamba “wale walio na mazoea” ya kufanya mambo hayo machafu ‘hawatauriti Ufalme wa Mungu.’ Kwa hiyo, ikiwa mutu fulani amekuwa na zoezi la kutazama mambo machafu na yenye kuchukiza ya ponografia, labda mara nyingi, na hatubu na kugeuka, ataondolewa katika kutaniko. Anaweza kutengwa ili kulinda usafi na hali nzuri ya kutaniko.—1 Ko. 5:5, 11.
Ni vizuri kujua kwamba ndugu fulani waliotazama mambo yenye kuchukiza ya ponografia waliwaendea wazee na kupokea musaada wa kiroho waliohitaji ili kufanya mabadiliko makubwa. Yesu aliwasihi Wakristo katika kutaniko la Sardi hivi: ‘Uyatie nguvu mambo yanayobaki yaliyokuwa tayari kufa, endelea kukazia akilini jinsi ulivyopokea na jinsi ulivyosikia, nawe uendelee kulishika, na utubu. Hakika usipoamuka, nawe hautajua hata kidogo saa nitakayokuja juu yako.’ (Ufu. 3:2, 3) Inawezekana kutubu na kunyakuliwa kutoka katika moto.—Yud 22, 23.
Kwa hiyo, itakuwa vizuri kabisa ikiwa kila mumoja wetu anaazimia kutokukaribia hatari hiyo. Ndiyo, tunapaswa kuepuka kabisa kila namna ya ponografia!
TAREHE 10-16/6
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAEFESO 1-3
“Mambo Yenye Usimamizi wa Yehova Unafanya”
it-2-F uku. 858 fu. 2
Siri Takatifu
Ufalme wa Kimasiya. Mu maandishi yake, Paulo anazungumuzia kwa ujumla namna siri takatifu ya Kristo ilifunuliwa. Mu Waefeso 1:9-11, anaeleza kama Mungu alijulisha “siri takatifu” ya mapenzi yake na kusema: “Yeye mwenyewe alikusudia kulingana na vile ilimupendeza kwa ajili ya usimamizi kwenye mwisho kabisa wa nyakati zenye ziliwekwa, ili kukusanya pamoja vitu vyote katika Kristo, vitu vyenye kuwa mbinguni na vitu vyenye kuwa duniani. Ndiyo, katika yeye mwenye tuko katika umoja naye na tulihesabiwa kuwa wariti, kwa kuwa tulichaguliwa mbele ya wakati kulingana na kusudi la ule mwenye anatimiza mambo yote kama vile anaamua kulingana na mapenzi yake.” Ile “siri takatifu” inahusu serikali, ni kusema Ufalme wa Mungu wa Kimasiya. “Vitu vyenye kuwa mbinguni” vyenye Paulo anazungumuzia ni wale wenye watariti Ufalme wa mbinguni na Kristo. “Vitu vyenye kuwa duniani” ni raia wa ule Ufalme wenye wataishi ku dunia. Yesu alionyesha wanafunzi wake kama siri takatifu inahusu Ufalme wakati aliwaambia: “Ninyi mumepewa siri takatifu ya Ufalme wa Mungu.”—Mk 4:11.
Yehova Anakusanya Tena Familia Yake
3 Musa aliwaambia Waisraeli hivi: ‘Yehova Mungu wetu ni Yehova mumoja.’ (Kum. 6:4) Yehova anatenda siku zote kulingana na kusudi lake. Kwa hiyo, “kwenye kikomo kamili cha nyakati zilizowekwa rasmi,” Mungu ameweka “usimamizi,” ni kusema, mupango wa kuunganisha viumbe vyake vyote vyenye akili. (Soma Waefeso 1:8-10.) Usimamizi huo utatimiza kusudi lake katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza: kuwatayarisha Wakristo watiwa-mafuta watakaoishi mbinguni chini ya uongozi wa Yesu Kristo, aliye Kichwa chao. Jambo hilo lilianza siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33, wakati Yehova alianza kukusanya wale ambao watatawala pamoja na Kristo mbinguni. (Mdo. 2:1-4) Kwa kuwa Wakristo watiwa-mafuta wameonyesha imani katika zabihu ya ukombozi ya Kristo, Yehova anawatangaza ao anawaona kuwa wenye haki wanaostahili kupata uzima. Kwa hiyo, wanatambua kama wamefanywa kuwa “watoto wa Mungu.”—Ro. 3:23, 24; 5:1; 8:15-17.
4 Sehemu ya pili: kutayarisha wale watakaoishi katika Paradiso duniani wakiongozwa na Ufalme wa Kristo. Ule ‘Umati mukubwa’ ndio sehemu ya kwanza ya wale watakaoishi duniani. (Ufu. 7:9, 13-17; 21:1-5) Wakati wa Utawala wa Miaka Elfu Moja, wale watakaofufuliwa watakuja kujiunga nao. (Ufu. 20:12, 13) Wazia namna ufufuo utakavyoonyesha kama tuko katika umoja ao tumeunganishwa! Mwishoni mwa ile miaka elfu moja, “vitu vilivyo duniani,” maana yake, watumishi wa Yehova walio duniani, watapata jaribu la mwisho. Wale watakaobaki waaminifu watafanywa kuwa “watoto wa Mungu” wa duniani.—Ro. 8:21; Ufu. 20:7, 8.
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
Usiruhusu Kitu Chochote Kikuzuie Kupata Utukufu
15 Tunawasaidia wengine wapokee utukufu wa Mungu kwa kuendelea kufanya mapenzi yake. Paulo aliandikia kutaniko la Efeso hivi: ‘Kwa hiyo nawaomba ninyi musife moyo kwa sababu ya hizi ziki zangu kwa ajili yenu, kwa maana hizi zinamaanisha utukufu kwenu.’ (Efe. 3:13) Ni katika maana gani ziki ao mateso ya Paulo ‘yalimaanisha utukufu’ kwa Waefeso? Kwa kuwa Paulo alikuwa tayari kuendelea kuwatumikia ijapokuwa majaribu, hilo liliwaonyesha Waefeso kwamba pendeleo lao la kuwa Wakristo lilikuwa nzito na la samani kubwa sana. Ikiwa Paulo angeshindwa kuvumilia mateso, hilo lingeonyesha kwamba hakuona urafiki wake na Yehova, kazi yake ya kuhubiri, na tumaini lake kuwa vitu vya samani, sivyo? Uvumilivu wa Paulo ulitukuza Ukristo na ulionyesha kwamba kuwa mwanafunzi wa Kristo ni jambo ambalo mutu anastahili kutesekea.
cl uku. 299 fu. 21
“Kujua Upendo wa Kristo”
21 Neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa ‘kujua’ linamaanisha “kujua kupitia matendo, kupitia uzoefu.” Juu tufikie kujua upendo wa Yesu, inaomba kupenda watu sawa vile Yesu aliwapenda, kwa kutumikia wengine na roho ya kujitoa, kwa kuwahurumia na kuwasaidia, na kuwasamehe kwa moyo wote. Ni kupitia ile matendo njo tunafikia “kujua upendo wa Kristo, wenye unapita ujuzi.” Tusisahau hata kidogo kama kadiri tunaendelea kuiga Kristo, ni vile njo tutamukaribia zaidi Mungu wetu mwenye upendo, Yehova, juu Yesu alionyesha kwa ukamili sifa za Yehova.
TAREHE 17-23/6
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAEFESO 4-6
“Muvae Silaha Zote Kutoka kwa Mungu”
Vijana Musimame Imara na Kumupinga Ibilisi
MUTUME PAULO alilinganisha Wakristo na maaskari. Tunapigana vita, na maadui wetu hawako watu wa kuwazia tu! Hatupigane vita na wanadamu, tunapigana vita na Shetani na mashetani wake. Wamepigana vita kwa maelfu ya miaka na wanajua muzuri kupigana vita. Kwa hiyo, inaweza kuonekana kama hatuwezi kupata ushindi katika vita hiyo, zaidi sana ikiwa tuko vijana. Vijana wanaweza kupata ushindi katika vita hiyo yenye wanapigana na maadui hao wenye nguvu nyingi? Ndiyo wanaweza, na wanaendelea kupata ushindi! Sababu gani? Kwa sababu wanapata nguvu kutoka kwa Yehova. Pia, kama maaskari wenye wamezoezwa muzuri, ‘wanavaa mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu’ ili wakuwe tayari kwa ajili ya vita.—Soma Waefeso 6:10-12.
w18.05 uku. 28-29 fu. 4, 7, 10
Vijana Musimame Imara na Kumupinga Ibilisi
4 Kama mukaba, kweli yenye tunajifunza katika neno la Mungu inatulinda juu ya mafundisho ya uongo. (Yoh. 8: 31, 32; 1 Yo. 4:1) Na kadiri tunaendelea kujifunza kupenda kweli zenye kuwa katika Neno la Mungu, itakuwa mwepesi zaidi kwetu kuishi kulingana na kanuni za Mungu, ao kuvaa “bamba [letu] la kifuani.” (Zb. 111:7, 8; 1 Yo. 5:3) Pia, ikiwa tunaelewa muzuri zaidi kweli hizo, itakuwa mwepesi zaidi kuzitetea mbele za maadui wetu.—1 Pe. 3:15.
7 Kanuni za uadilifu ao za haki za Yehova zenye kulinda “moyo” wetu, ao mutu wetu wa ndani, zinaweza kulinganishwa na bamba hilo la kifuani. (Mez. 4:23) Askari hangebadilisha hata kidogo bamba lake la kifuani na bamba lenye kufanywa na vyuma vyenye haviko nguvu. Vilevile, hatuwezi hata kidogo kubadilisha kanuni za Yehova za mambo yenye kuwa sawa na mawazo yetu wenyewe juu ya mambo yenye kuwa sawa. Hatuna hekima ya kutosha ili kulinda moyo wetu wenyewe. (Mez. 3:5, 6) Ndiyo sababu tunapaswa kuchunguza mara kwa mara “bamba [letu] la kifuani” ili kuona ikiwa linaendelea kulinda moyo wetu.
10 Viatu vya askari wa Roma vilimusaidia kupigana vita muzuri, viatu vya mufano vyenye tunavaa vinatusaidia kutangaza “habari njema ya amani.” (Isa. 52:7; Ro. 10:15) Lakini, wakati fulani inaomba kuwa na ujasiri mwingi ili kuhubiri. Bo, mwenye kuwa na miaka 20, anasema hivi: “Niliogopa kuhubiria wanafunzi wenzangu. Ninawaza kama nilikuwa ninasikia haya. Wakati ninakumbuka, sijue ni sababu gani nilikuwa ninasikia haya. Sasa ninafurahia kuhubiria vijana wenzangu.”
w18.05 uku. 29-31 fu. 13, 16, 20
Vijana Musimame Imara na Kumupinga Ibilisi
13 Ni “mishale” gani “inayowaka moto” yenye Shetani anaweza kukutupia? Pengine anakushambulia kwa kusema mambo ya uongo juu ya Yehova. Shetani anapenda ujisikie kama Yehova hakupendi na kama hakuna mutu mwenye kukuhangaikia. Ida, mwenye kuwa na miaka 19, anasema hivi: “Mara nyingi nimejisikia kama Yehova haiko karibu na mimi na kama hapendi kuwa Rafiki yangu.” Ida anafanya nini wakati anajisikia hivyo? Anasema hivi: “Mikutano inasaidia sana imani yangu ikomae. Nilizoea tu kukaa kwenye mikutano bila hata kutoa maelezo, kwa sababu nilikuwa ninawaza kama hakuna mutu mwenye anapenda kusikia mambo yenye nitasema. Lakini sasa, ninatayarisha mikutano na kujikaza kujibia mara mbili ao mara tatu. Haiko mwepesi, lakini ninajisikia muzuri zaidi wakati ninafanya hivyo. Na ndugu na dada wananitia moyo sana. Sikuzote wakati ninatoka kwenye mikutano, ninajua kama Yehova ananipenda.”
16 Kama vile kofia ya chuma inalinda ubongo wa askari, “tumaini [letu] la wokovu” linalinda mawazo yetu. (1 Te. 5:8; Mez. 3:21) Tumaini linatusaidia kukaza akili yetu juu ya ahadi za Mungu na kuepuka kuvunjika moyo kwa sababu ya magumu yetu. (Zb. 27:1, 14; Mdo. 24:15) Lakini, ikiwa tunapenda tumaini letu litulinde, tunapaswa kuona tumaini hilo kuwa la kweli kabisa. Tunapaswa kuvaa “kofia [yetu] ya chuma” kwenye kichwa chetu, hapana kuibeba katika mukono!
20 Mutume Paulo alisema kama Neno la Mungu liko kama upanga. Yehova ametupatia Neno hilo. Lakini tunapaswa kujifunza kutumia Neno hilo kwa ufundi ili kutetea imani yetu ao ili kubadilisha namna yetu ya kuwaza. (2 Ko. 10:4, 5; 2 Ti. 2:15) Namna gani unaweza kukomalisha ufundi wako? Sebastian, mwenye kuwa na miaka 21, anasema hivi: “Ninaandika andiko moja kutoka katika kila sura katika usomaji wangu wa Biblia. Ninajifanyia liste ya maandiko yenye ninapenda sana.” Hilo linanisaidia kuelewa muzuri zaidi mawazo ya Yehova. Daniel anaongezea hivi: “Katika usomaji wangu wa Biblia, ninaandika pembeni maandiko fulani yenye ninaona kama yanaweza kusaidia watu wenye ninakutana nao katika kazi ya kuhubiri. Nimetambua kama watu wanaitikia muzuri wakati wanaona kama unapenda sana Biblia na kama unajikaza sana ili kuwasaidia.”
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 859-860 fu. 7
Utakatifu
Roho takatifu. Yehova njo anaongozaka ile roho, ao nguvu yake ya utendaji na inafanyaka tu mambo yenye inapatana na kusudi lake. Ile roho iko safi, takatifu, na imetiwa pembeni juu ifanye tu kazi ya Mungu. Njo maana inaitwa “roho takatifu” na “roho ya utakatifu.” (Zb 51:11; Lu 11:13; Ro 1:4; Efe 1:13) Wakati roho takatifu inatenda juu ya mutu fulani inamusaidia akuwe na matendo ya utakatifu na yenye iko safi. Wakati ule mutu anatenda tendo chafu ao la mubaya, pale anapinga ao ‘anahuzunisha’ ile roho. (Efe 4:30) Hata kama roho takatifu haiko mutu, lakini inaonyesha sifa takatifu za Mungu na njo maana inaweza ‘kuhuzunika.’ Kuzoea kufanya mambo ya mubaya kunaweza ‘kuzimisha moto wa roho.’ (1Te 5:19) Kama ile zoezi inaendelea, roho takatifu ya Mungu ‘inahuzunika’ mu njia fulani, na ile inaweza kufanya Mungu ageuke na kuwa adui ya ule mutu mwenye anazoea kufanya mambo ya mubaya. (Isa 63:10) Mutu mwenye anahuzunisha roho takatifu anaweza kufikia kufanya zambi ya kutukana roho takatifu. Yesu Kristo alisemaka kama ile zambi haiwezi kusamehewa mu mupangilio wa mambo wa sasa na ule wenye utakuja.—Mt 12:31, 32; Mk 3:28-30; ona ROHO.
it-1-F uku. 237 fu. 10
Pupa
Inaonekanaka mu matendo. Pupa inaonekanaka mu matendo yenye mutu anafanya. Ile matendo njo inaonyeshaka kama ule mutu iko na tamaa ya mubaya na yenye haifae. Yakobo, muandikaji wa Biblia, alisema kama tamaa ya mubaya, wakati inapata mimba, inazaa zambi. (Yak 1:14, 15) Kwa hiyo, tunaweza kujua mutu wa pupa kwa kuangalia matendo yake. Mutume Paulo anasema kama kuwa na pupa ni sawa na kuwa muabudu-sanamu. (Efe 5:5) Ile ni kweli juu mutu wa pupa anafanya jambo lenye anatamani kuwa mungu wake, kwa kuliona kuwa la maana kupita kutumikia na kuabudu Muumbaji wake.—Ro 1:24, 25.
TAREHE 24-30/6
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAFILIPI 1-4
‘Musihangaike Juu ya Kitu Chochote’
“Amani ya Mungu . . . Inazidi Fikira Zote”
10 Ni nini inaweza kutusaidia ili tusihangaike juu ya kitu chochote na tukuwe na “amani ya Mungu”? Maneno yenye Paulo aliwaandikia Wafilipi yanaonyesha kuwa dawa ya mahangaiko ni sala. Kwa hiyo, wakati tuko na mahangaiko, tunapaswa kusali sana. (Soma 1 Petro 5:6, 7.) Wakati unasali, ukuwe na imani kabisa kwa Yehova, na ujue kuwa anakuhangaikia. Usali kwake kwa “kutoa shukrani,” juu ya baraka zenye umepata. Tumaini letu kwake litatiwa nguvu wakati tunakumbuka kuwa anaweza ‘kufanya kwa wingi zaidi kupita mambo yote tunayoomba ao tunayofikiri.’—Efe. 3:20.
“Amani ya Mungu . . . Inazidi Fikira Zote”
7 Bila shaka wakati ndugu wa Filipi walisoma barua yenye Paulo aliwaandikia, walikumbuka mambo yenye yalikuwa yamemufikia na namna hakuna hata mumoja wao mwenye alitazamia kuwa Yehova angetenda namna alitenda. Paulo alipenda kuwafundisha nini? Kwa kweli, alipenda kuwafundisha kuwa wasihangaike. Wasali na kisha watapata amani ya Mungu. Paulo aliwaambia kuwa ‘amani ya Mungu . . . inazidi fikira zote.’ Hilo linamaanisha nini? Watafsiri fulani wanatafsiri maneno hayo kuwa “inapita matumaini yote” ao “inapita mipango yote ya mwanadamu.” Kwa kweli, Paulo alikuwa anasema kuwa “amani ya Mungu” ni ya ajabu zaidi kuliko namna tunaweza kuwazia. Kwa hiyo, hata kama sisi wanadamu, tunaweza kuona kuwa hakuna namna ya kumaliza matatizo yetu, Yehova yeye anaona na anaweza kufanya mambo yenye hatutazamie.—Soma 2 Petro 2:9.
“Amani ya Mungu . . . Inazidi Fikira Zote”
16 Tunapata matokeo gani wakati tunapata “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote”? Maandiko yanatoa jibu kwa kusema kama ‘italinda mioyo yetu na nguvu zetu za akili kwa njia ya Kristo Yesu.’ (Flp. 4:7) Neno la zamani lenye kutafsiriwa “kulinda” lilitumiwa katika jeshi. Lilizungumuzia kikundi cha askari wenye walipewa kazi ya kulinda muji wenye kuzungukwa na kuta wakati wa zamani. Muji wa Filipi ulikuwa hivyo. Wakaaji wa Filipi walilala salama usiku kwa sababu walijua kuwa maaskari walikuwa wanalinda milango ya muji wao. Vilevile, wakati tuko na “amani ya Mungu,” mioyo yetu na akili zetu zinatulia. Tunajua kama Yehova anatuhangaikia na anataka tukuwe na maisha ya muzuri. (1 Pe. 5:10) Kujua hilo kunatusaidia tusihangaike sana na tusivunjike moyo.
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 850 fu. 1
Matoleo
Matoleo ya kinywaji. Matoleo ya kinywaji ilikuwa inatolewa na zabihu zingine, zaidi sana kisha Waisraeli kuingia mu Inchi ya Ahadi. (Hes 15:2, 5, 8-10) Ile matoleo ilikuwa divai (“pombe”), na walikuwa wanaimwanga ku mazabahu. (Hes 28:7, 14; ona pia Kut 30:9; Hes 15:10) Mutume Paulo aliandikia Wakristo wa Wafilipi hivi: “Hata kama ninamwangwa kama toleo la kinywaji juu ya zabihu na utumishi mutakatifu kwenye imani yenu imewaongoza, ninafurahi na kushangilia pamoja na ninyi wote.” Kwa kutumia mufano wa toleo la kinywaji, Paulo alionyesha kama alikuwa tayari kujitoa kwa ajili ya ndugu zake Wakristo. (Flp 2:17) Siku fulani mbele Paulo akufe, aliandikia Timoteo hivi: “Mimi tayari ninamwangwa kama toleo la kinywaji, na wakati wangu wa kufunguliwa umekaribia sana.”—2 Ti 4:6.
w07 1/1 uku. 26-27 fu. 5
“Ufufuo wa Kwanza”—Unaendelea Sasa!
5 Kisha, ni lazima washiriki watiwa-mafuta wa “Israeli wa Mungu” waungane na Bwana Yesu Kristo katika utukufu wa mbinguni, kwenye ‘watakuwa pamoja na Bwana sikuzote.’ (Wagalatia 6:16; 1 Watesalonike 4:17) Ile tukio inaitwa “ufufuo wa kwanza.” (Wafilipi 3:10, 11; Ufunuo 20:6) Wakati ule ufufuo utamalizika, mamilioni ya watu wataanza kufufuliwa ku dunia wakiwa na tumaini la kupata uzima wa milele mu Paradiso. Kwa hiyo, ikuwe tuko na tumaini la kuishi mbinguni ao duniani, inaomba tuelewe muzuri “ufufuo wa kwanza.” Ni ufufuo wa aina gani? Utatokea wakati gani?