MAISHA YA MUKRISTO
Uumbaji Unatufundisha Nini juu ya Uhodari?
Yehova anatumia mifano ya wanaume na wanamuke wenye kuzungumuziwa mu Biblia ili kutufundisha namna ya kuonyesha sifa zake. Lakini uumbaji wake unaweza pia kutufundisha mambo mingi ya maana. (Yob 12:7, 8) Tunaweza kujifunza nini juu ya uhodari kupitia simba, farasi, munyama mudogo mwenye kuitwa nguchiro, ndege mwenye kuitwa muvumaji, na tembo?
MUANGALIE VIDEO UJIFUNZE UHODARI KUPITIA UUMBAJI, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Namna gani simba jike wanaonyesha uhodari wakati wako wanalinda watoto wao?
Namna gani farasi wanazoezwa ili wakuwe hodari katika vita?
Namna gani munyama mudogo mwenye kuitwa nguchiro haogope nyoka mwenye sumu?
Namna gani ndege wadogo sana wenye kuitwa wavumaji wanaonyesha uhodari?
Namna gani tembo wanalinda kwa uhodari tembo wengine wenye kuwa mu kundi?
Wale wanyama wanakufundisha nini juu ya uhodari?